wise the lady kimey hajamaliza tu "mipango yake ya nje"
Haaha ha ha unanivunjia heshima mama mwenye nyumba unalijua hilo??
Yaani we unachekesha kweli mie niachane na BE tangu lini na haiwezekani hata siku moja Desi namna gani bwan???
Na ikitokea tu umeachana na BE, mimi nakufanya kama mpango wangu wa nje, au unaonaje DA?
Mpango wa nje au kando?? Sihitaji kwa sasa Mkuu tafadhali. Halafu nyie mbona mnapenda sana mambo ya kuachana kwanini lakini??? Mie sina mpango wa kumuacha BE hata kidogo
Usinikumbushe kimey wangu maana nnavyommis,,,,halafu ukome na udaku wako muone vile
Mi namwonea wivu kweli kweli Kimey naweza kumpindua?
Kazi upo hapa sasa. Kimey uko wapi mkuuu unaibiwa huku huyu WL hajatulia kabisa
WL wewe umekuwa Fidel leo?? Kwani umeamkaje leo mbona sikuelewi?? Ushakunywa ulanzi nini saa hizi
Ndiyo shida ya kujidai kuchagua wachumba lazima uingie mkenge tu tuulizeni sisi tuliochaguliwa wachumba na wazazi wetu wapenzi hatupati shida na hakuna hata fikra kwamba kuna siku tutaachana. Mnatumia principal za kizungu kupata wachumba weusi! Jua wazungu upendo hupungua kadri muda unavyokwenda ndiyo maana kuna taraka nyingi, wakati waafrika unaoa bila upendo sana ndipo upendo unaongezeka kadri muda uendavyo ndiyo maana ndoa za aina hiyo kutengana au talaka ngumu mno. Mmeiacha asili hamna budi kuibeba misalaba yenu mizito hiyo.
Dena nimekosea wapi na wewe???umeanza kuwa kama fainest eeh!huyu kishili hapo hajui kama huko aliko tulishatoka??saa hizi tuna:whoo::whoo: