Wakwetu03
Senior Member
- Sep 15, 2010
- 194
- 87
T-Motion ilianza rasmi katikati ya mwaka 2014 ikiwa na idara mbili 1) Music audio ikiitwa Tumanyene records 2) Video production ikiitwa T-Motion films works. Baadaye katikati ya mwaka 2015 T-motion ikaunganishwa na kuwa kitu kimoja ikaitwa T-Motion Entertainment. Meshamazing alisainiwa rasmi mwishoni mwa mwaka 2015 baada ya kusota kwenye viunga vya T-Motion kwa zaidi ya mwaka mmoja bila kusainiwa akipewa mkataba wa muda mrefu sana ambao vipengele vingi vilimbana kuhusiana na mambo yake ya shule vikimtaka ahakikishe anamaliza na anafaulu. Wimbo wa kwanza kumtambulisha kwenye ulimwengu wa burudani uliitwa HAWA ukifuatiwa na KODOA halafu BASI SAWA mpaka saivi akitamba na wimbo wa SINA THAMANI na kolabo aliyofanya na MTAFYA pamoja na GREEN BOY inayoitwa ZUNGUSHA. Meshamazing ameshashinda kwenye mashindano mbalimbali kama SUPER NYOTA 2017 na BSS 2018 pia alishawahi kutajwa kwenye vipengele viwili kwenye tuzo za MMA 2015 1)Msanii chipukizi 2)Wimbo bora wa R&B (Hawa) ambazo hazikufanyika.