Research Solutions TZ
Member
- Jul 11, 2020
- 66
- 145
Bila shaka tunatambua ustawi wa jamii unaanzia kwenye ngazi ya familia, kwa hiyo ni jukumu la ustawi wa jamii kuwa na sera inayoyaangazia matatizo yote yanayoikumba ngazi ya familia ili kuiweka sawa
Ngazi ya familia ina kitu wanaita TARAKA, ambaye sababu yake kuu kwa tafiti zilizopo ni mtu kushindwa kumtia mtu mimba au mwanamke kushika mimba, baada ya sababu hiyo ndio inafuata usaliti. Kwa hiyo sababu kuu za migogoro ya ndoa ni Kushindwa kuzaa/kuzalisha ikifuatiwa na usaliti ndio unafuata sababu nyingine zikiwemo za kiuchumi
Tatizo la kushindwa kuzaa ni tatizo zaidi kwa mwanamke kwa kuwa manyanyaso huwa ni mengi ikiwemo unyanyapaa. Kama mmeisikia ile kesi ya Mauaji kule Mbezi jamaa alikuwa anamsaliti mkewe waziwazi kwa sababu kuwa mkewe hawezi kumzalia mtoto, pia personaly nimeona wanaume wanavyowanyanyasa wanawake kisa tu kushindwa kupata mtoto
Baadhi ya maneno wanayoambiwa ni kuwa wametoa mimba, kwa hiyo walikuwa malaya kiasi cha kuharibu vizazi vyao, ila si kweli kuwa mwanamke asiyeshika mimba husababishwa na kutoa mimba tu, wengine huwa ni tatizo la kualiwa au mparanganyiko kwenye mfumo wa uzazi
Kwa hiyo watu hawa huonekana walikuwa malaya kiasi cha kutoa mimba nyingi
Pia bado jamii inaona asiyeweza kuzaa kama ana laana. Hapa ndio manyanyaso huwa mengi kwa ngazi zote hata kwenye familia yake mwenyewe sio kwa sehemu aliyoolewa tu. Unakuta mzazi anamuuliza mwanae, 'mwanangu mwaka wa pili huu nataka mjukuu, changamka'
Marafiki na jamaa nao wanamaswali yanayoumiza rafiki zao bila kujua, utasikia he! bado?
Katika watu wenye msongo wa mawazo basi hawa watu naona wanaumia zaidi
Hata wanaume pia hukumbana na matusi, kuambiwa kama hauna mkojo, wewe bado mtoto..nk. ila kijamii mwanamke anaumia zaidi
Ushauri
Kwa kuwa tatizo hili linawaumiza sana wanawake hasa wanapoingia kwenye mapenzi, ni vyema kuwa na mtu ambaye anajiweza kisaikolojia ili asije akawa chanzo cha maumivu
Pili muwe wawazi na msitafute dawa kwa waganga mkaishiwa kutapeliwa, magonjwa mengine hujitibu kwa muda, aidha matatizo mengine huanza na saikolojia, kama reaction kwa kitu ulichokiweza(Scientifically proven) kwamba kuna matatizo huja kweli bila kuwa na chanzo halisi bali hofu ya mtu husika
Tatu, zingatia masuala ya chakula na epuka msongo wa mawazo kwa kuwa na mpenzi au watu watakaokufurahisha ili kama una tatizo lijitibu taratibu, sio ajabu mtu akapata mtoto baada ya miaka kadhaa
Poleni wote!
Tunaelimishana kuhakikisha hatuyumbishwi na stresses
Ngazi ya familia ina kitu wanaita TARAKA, ambaye sababu yake kuu kwa tafiti zilizopo ni mtu kushindwa kumtia mtu mimba au mwanamke kushika mimba, baada ya sababu hiyo ndio inafuata usaliti. Kwa hiyo sababu kuu za migogoro ya ndoa ni Kushindwa kuzaa/kuzalisha ikifuatiwa na usaliti ndio unafuata sababu nyingine zikiwemo za kiuchumi
Tatizo la kushindwa kuzaa ni tatizo zaidi kwa mwanamke kwa kuwa manyanyaso huwa ni mengi ikiwemo unyanyapaa. Kama mmeisikia ile kesi ya Mauaji kule Mbezi jamaa alikuwa anamsaliti mkewe waziwazi kwa sababu kuwa mkewe hawezi kumzalia mtoto, pia personaly nimeona wanaume wanavyowanyanyasa wanawake kisa tu kushindwa kupata mtoto
Baadhi ya maneno wanayoambiwa ni kuwa wametoa mimba, kwa hiyo walikuwa malaya kiasi cha kuharibu vizazi vyao, ila si kweli kuwa mwanamke asiyeshika mimba husababishwa na kutoa mimba tu, wengine huwa ni tatizo la kualiwa au mparanganyiko kwenye mfumo wa uzazi
Kwa hiyo watu hawa huonekana walikuwa malaya kiasi cha kutoa mimba nyingi
Pia bado jamii inaona asiyeweza kuzaa kama ana laana. Hapa ndio manyanyaso huwa mengi kwa ngazi zote hata kwenye familia yake mwenyewe sio kwa sehemu aliyoolewa tu. Unakuta mzazi anamuuliza mwanae, 'mwanangu mwaka wa pili huu nataka mjukuu, changamka'
Marafiki na jamaa nao wanamaswali yanayoumiza rafiki zao bila kujua, utasikia he! bado?
Katika watu wenye msongo wa mawazo basi hawa watu naona wanaumia zaidi
Hata wanaume pia hukumbana na matusi, kuambiwa kama hauna mkojo, wewe bado mtoto..nk. ila kijamii mwanamke anaumia zaidi
Ushauri
Kwa kuwa tatizo hili linawaumiza sana wanawake hasa wanapoingia kwenye mapenzi, ni vyema kuwa na mtu ambaye anajiweza kisaikolojia ili asije akawa chanzo cha maumivu
Pili muwe wawazi na msitafute dawa kwa waganga mkaishiwa kutapeliwa, magonjwa mengine hujitibu kwa muda, aidha matatizo mengine huanza na saikolojia, kama reaction kwa kitu ulichokiweza(Scientifically proven) kwamba kuna matatizo huja kweli bila kuwa na chanzo halisi bali hofu ya mtu husika
Tatu, zingatia masuala ya chakula na epuka msongo wa mawazo kwa kuwa na mpenzi au watu watakaokufurahisha ili kama una tatizo lijitibu taratibu, sio ajabu mtu akapata mtoto baada ya miaka kadhaa
Poleni wote!
Tunaelimishana kuhakikisha hatuyumbishwi na stresses