Wasiokuwa na chakupoteza wanapongezeka haki ndio kinga pekee

Wasiokuwa na chakupoteza wanapongezeka haki ndio kinga pekee

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Watu wenye mali kama nyumba, mashamba, magari, kazi, mifugo, viwanda, biashara kubwa na mali nyinginezo ni watu wenye uwezo mkubwa sana wa kuvumilia mambo, kutafakari na kusamehe. Idadi ya watu wa aina hii wakiwa wengi kwenye familia, mtaa, kitongoji, kijiji, kata, tarafa. wilaya, mkoa na nchini migogoro inakuwa michache sana, watavumilia hata kama hawapendi ili kunusuru mali zao. kwao wao "present is known"

Kinyume chake watu ambao wasiomiliki vitu vingi vya thamani kama vile familia, nyumba, mashamba, mifugo, ajira au kitu chochote cha thamani ni rahisi sana kuchokozeka na kufanya mambo bila ya kutafakari sana. Hawa ni watu ambao riziki zao wanazipata kwa taabu nyingi sana. Kama ukipakana na watu wa aina hii kwenye mtaa wako itakubidi kukaa chonjo na chukua tahadhari, maana wanao uwezo mkubwa wa kufanya chochote na lolote wakati wowote. Na mabadiliko makubwa sana ya mifumo duniani huwa yanasababishwa na kundi hili la watu.

Wakati makundi haya ya watu wasiokuwanacho yakiongezeka duniani kutokana na mifumo ya utawala, hali ya hewa na utandawazi njia pekee ya kuzuia machafuko zaidi na migogoro ni kuimarisha mifumo ya kutoa haki na kupunguza matumizi ya nguvu za dola kwa wananchi.

Ni haki pekee inayoweza kuwatuliza watu wenye njaa waliokata tamaa.
 
Ogopa mtu asiye hata na buku g mfukoni anaweza akakuua halafu akajisalimisha mwenyewe kituoni
 
Ogopa mtu asiye hata na buku g mfukoni anaweza akakuua halafu akajisalimisha mwenyewe kituoni
Iko siku tutakuja kulaumiani sisi wote kwa kufanya au kutofakufa hili na lile, hiki na kile, hivi na vile, haya au yale. Wakati huo itakuwa too late
 
Miaka 59 ya UHURU tuna vyote hivi;

Mount Kilimanjaro

Serengeti National Park

Mikumi

Ziwa Victoria, Tanganyika

Makaa ya mawe Songea

Bandari ya DSM

Gesi ya Mtwara

Almasi

Tanzanite

Dhahabu

Bado CCM imeshindwa kumpa mwananchi MAJI ya kunywa safi na salama tu
 
Miaka 59 ya UHURU tuna vyote hivi;

Mount Kilimanjaro

Serengeti National Park

Mikumi

Ziwa Victoria, Tanganyika

Makaa ya mawe Songea

Bandari ya DSM

Gesi ya Mtwara

Almasi

Tanzanite

Dhahabu

Bado CCM imeshindwa kumpa mwananchi MAJI ya kunywa safi na salama tu
CCM iliua viwanda sasa wanataka tuisifu kwa kujenga viwanda, imetutia umaskini Sasa tuisifu kwa kuondoa umaskini, imeua reli Sasa wanataka tuisifu kwa kufufua reli. Miaka 60 haikupeleka umeme kwa wananchi Sasa wanataka tuisifu kwa kupeleka umeme.
 
Back
Top Bottom