Wasiokuwa waislam, hamtaki maisha haya?

Wasiokuwa waislam, hamtaki maisha haya?

Pepo (Jannah) ni sehemu ya maisha ya akhera katika imani ya Kiislamu, inayotambuliwa kama malipo ya mwisho kwa wale waliotenda mema na kumcha Mwenyezi Mungu katika maisha yao ya dunia.

Nani Atakayeishi Peponi?​

  1. Wale Walio Na Imani na Watendaji Wema: Katika Qur'an, watu wa Peponi wanatambulika kama wale waliokuwa na Imani ya kweli katika Mwenyezi Mungu, waliishi maisha ya haki, na walitenda mema. Watu hawa walikuwa na tabia nzuri, walimcha Mwenyezi Mungu, na walijitahidi kwa bidii katika kutenda matendo mema.
  2. Mwenye Kumcha Mwenyezi Mungu: Sura ya 3:133 inasema: "Na shindanisheni kwa msamaha wa Mola wenu na Pepo iliyo pana kama mbingu na ardhi, iliyoandaliwa kwa wale wanaomcha Mwenyezi Mungu."
MAISHA YA PEPONI
  • Furaha Isiyo Na Mateso: Furaha katika Peponi itakuwa safi na isiyo na kifani
  • . Katika dunia, furaha mara nyingi huja na changamoto, maumivu, na huzuni. Kinyume chake, Peponi itakuwa sehemu ambapo huzuni, maumivu, na mateso yote yataondolewa, kama ilivyoelezwa katika Qur'an na Hadith.

  • Utajiri wa Kudumu: Katika dunia, utajiri unaweza kuleta furaha, lakini mara nyingi hubadilika na kutegemea hali ya kifedha, ambayo inaweza kuwa na changamoto na hatari. Peponi, hata hivyo, utajiri na starehe zitakuwa za kudumu na zisizo na mwisho, na zitafikia kiwango ambacho hakiwezi kulinganishwa na utajiri wa dunia.
  • Ugonjwa na Kifo: Katika dunia, ugonjwa na kifo ni vyanzo vya maumivu na huzuni. Peponi, ugonjwa na kifo havitakuwepo. Watu wataishi milele bila matatizo yoyote ya kiafya au hatari ya kifo, kama ilivyoelezwa katika Hadith.
  • Mahusiano ya Kijamii: Katika dunia, mahusiano yanaweza kuleta furaha lakini pia yanaweza kuwa na migogoro, chuki, na matatizo. Peponi, mahusiano yatajaa upendo, amani, na ushirikiano. Hakutakuwa na chuki wala maadui, na watu watakuwa na ushirikiano mzuri na maswahaba bora.
  • Mikono ya Baraka: Qur'an inaelezea kwamba Peponi kutakuwa na vitu ambavyo nafsi na macho yatafurahia, na kwamba watu watapambwa kwa mavazi ya hariri na dhahabu, wakifurahia starehe zote. Hii inaonyesha uzuri na ukamilifu wa baraka za Peponi ambazo ni zaidi ya kile tunachoweza kufikiria hapa duniani.
Mabikira 72 ndio tunapata huko mkuuu
 
Not the black, the muslims.

Wanaposema utakua tajiri peponi, kwa hiyo hakuna masikini, kama hakuna masikini hakuna maana ya utajiri. Wote tuko same level utasemaje ni matajiri, utajiri mnajilinganisha na nani? Doesn't make sense kabisa.

Halafu huko peponi tutaishi milele, tutakua na umri gani, ama hakuna umri? Yaani tutaingia peponi na umri gani? Wote tutakua vijana ama wazee ama watoto? Je kutakua na rika kama watoto, vijana wazee?

Wale wanawake 72 tunaopewa watakua wanazaa ama hawazai, kwa hiyo shahawa zetu xitakua zinafanya kazi gani, ama itakua ni kazi bure kukojoa?

Huo utajiri wa peponi utatusaidia nini? Yaani tutakua tunautumia kufanya nini?

Hii dini unahitaji kua na akili ya kiwango cha chini sana kua muumini wake.
Unahitaji kueleweshwa zaidi maana huna ujualo
 
Back
Top Bottom