Wasiovaa pete za ndoa kunyimwa komunio

Wasiovaa pete za ndoa kunyimwa komunio

Haya mambo kanisa inabidi liyaangalie kwa mapana laweza kujipotezea mvuto watu wakatimukia kwenye ulokole.
Hivi pete inauhusianno gani na upendo wa mtu moyoni?

mbona wengi wamekimbilia kwenye ulokole na katoliki imezidi kusonga mbele?kila kanisa na utaratibu wake.
 
Hii imepitiliza sasa. Upate wale wenye imani finyu wanahama kanisa. Hata sikumoja Siamini kiongozi yeyote yule wa dini alazimishe watu kufanya Wao watakavyo ..
Zingatia hapo ni watu wazima sasa si watoto wa Sunday school. Hii imekaa vibaya sana.

Hata Yesu mwenyewe alipo letewa yule mwanamke mzinzi aliwaambia makutano yeyote aliye msafi awe wa kwanza kumpiga mawe mwanamke mzinzi akainama chini alipo inuka akakuta watu wote wamekula kona amebaki yule mwanamke akaamwambia nenda zako usitende dhambi tena.
 
mbona wengi wamekimbilia kwenye ulokole na katoliki imezidi kusonga mbele?kila kanisa na utaratibu wake.

Ngoja waanzishe huu utaratibu parokia zote uone mwamko wake
 
Hapo watachemka tu. Kwanza hakuna uhusiano wowote kati ya pete na ndoa, mtu anaweza kuwa anavaa pete na akafanya uzinzi akiwa na pete yake kidoleni. Mimi enzi hizo kabla sijampokea Yesu kwa kumaanisha niliwahi kufanya uzinzi na mwanamke akiwa amevaa pete, na wala alikuwa hashutuki. Yaani mpaka sasa unaniuma sana. Lakini namshukuru Mungu alinitoa katika shimo hilo la maangamizi.

Cha kufanya hilo kanisa liwafundishe vizuri watu kuhusu kuheshimu ndoa zao hata kama hawavai pete. Ila wokovu halisi ndani ya Yesu ndio suluhisho murua; hata mimi wakati huo nilikuwa Mkatiliki tena ex candidate for priesthood. Thank you my JESUS
ndo zenu nyie tumewazoea.
 
Kaka Fidel, niliibiwa pete yangu na kibaka na sina uwezo wa kununua pete ingine, wataninyima komunio? Au ndio itakua maswali na majibu halafu ndio unapitishwa alishwe/asilishwe??!!!
 
Back
Top Bottom