Wakuu,
Mambo yanazidi kuchanganya, ni vuta n' kuvute.
Wasira anasema sheria za uchaguzi ni matokeo ya maridhiano, ambapo wananchi wote wakiwemo CHADEMA walishirikishwa kutoa maoni kabla ya miswada kupelekwa bungeni na baadaye kupitishwa baada ya kupitiwa kuwa sheria.
Wasira anaongeza CHADEMA kushupaza shingo wakati mabadiliko yameshafanyika sio demokrasia ni udikteta, maana wanagomea jambo ambalo watanzania wote walishiriki kutoa maoni na likapitishwa.