Pre GE2025 Wasira: Wanaosema tumekaa miaka 60 hakuna tulichofanya tuwasamehe hawajui wanachosema

Pre GE2025 Wasira: Wanaosema tumekaa miaka 60 hakuna tulichofanya tuwasamehe hawajui wanachosema

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wakuu,

Wassira amesema wanaoesema hakuna kilichofanyika kwa miaka 60 ya uhuru wanatakiwa kusamehewa kwani hawajui walisemalo.

Amesema zamani kulikuwa na barabara tatu pekee Dar -Moro, tanga korogwe, na moshi kwenda arusha na sababu zilikuwa zinaendelea kwenye mashamba ya biashara, elimu ilikuwa 1 mpaka 4, kulikuwa na wandisi 2 pekee, madaktari 12 walioazimwa kutoka nje, hakukua na umeme bali kuliwa na mtambo wa kusupplu umeme kwa watoto wa kishua oysterbay, upanga huku waswahili wakiwa maeneo ya karioakoo, ilala kwenye giza totoro

Pia soma: Pre GE2025 - Wassira: Hatukuahidi kuachia madaraka baada ya muda tulipopata uhuru. Hatutumii jeshi kubaki madarakani, tunachaguliwa

Leo nchi imeendelea, umeme bwerere na maendeleo kedede, sasa hao wanaonanga hakuna walichofanya na hawataki kujifunza wanatakiwa kusamehewa maana hawajui lolote.

Na ndio maana wataendelea kushika dola/madaraka sababu wana jukumu ka kuifanya tanzania iwe bora.

Wamefanya
IMG-20250125-WA0006.jpg
 
Back
Top Bottom