WASIWASI: Dawa aina ya PANADOL inaua?

mende 2014

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2014
Posts
763
Reaction score
131
Kijana mmoja amefariki kwa sababu ya kumeza dawa aina ya panadol. Baada ya kumeza dawa hiyo ya panadol tu alikunywa soda aina ya 7up, na akafa hapohapo.

Baada ya kuchunguzwa na wataam kifo chake, ikagunduliwa kuwaKidonge/dawa aina ya panadol ikifuatiwa kuchanganyishwa katika muda wa karibu na kinywaji cha gesi, dawa hiyo hugeuka na kuwa sumu.

Tafadhali wajulishe watu ujumbe huu ili wachukue tahadhari.
 
Tunaomba ithibati za kitabibu ili tuweze kujua ukweli wake katika hili
Jina halisi la marehemu na address yake kamili
Hospital aliyotibiwa mpaka mauti kumfika I mean baada ya kunywa hiyo dawa na hayo soda
Ripoti kamili ya daktari postmortem
Uthibitisho wa kaburi lake nk nk
 

hahaha, akileta nitakutumua hata salio la muda wa maongezi...
 
...mhh..!?, ngumu kumesa...
 
Huu ni uzushi tu..... hamna kitu kama hicho!
 
Kuna tafiti zingine prove yake haihitaji bajeti kubwa kukamilika,kama humuamini mtoa mada chukua mia yako kanunue panadol kisha chukua mia sita yako kanunue hiyo soda unywe ithibati itapatikana kwa wepesi zaidi.

kuna vitu vingine huhitaji kutumia 600 yako..
 
Kweli lakini mana kunawagonjwa wengine bila soda hawaponi me pia zamani nilikua nameza dawa na soda au juice
 
Kuna tafiti zingine prove yake haihitaji bajeti kubwa kukamilika,kama humuamini mtoa mada chukua mia yako kanunue panadol kisha chukua mia sita yako kanunue hiyo soda unywe ithibati itapatikana kwa wepesi zaidi.

Kwa hiyo unamshauri ajiue kwa sh 700 Tetete ikiwa kaamini akifanya hivyo atauded!
 
Peleka ujinga wako huko huko mnapoforwadiana message!! Contents za 7up unazijua? Contents za panadol unazijua? Tupe reaction iliyotengeneza sumu!
 

Akileta nishtue na mimi nije nisome
 
Last edited by a moderator:

Zamani nikiwa mdogo tulikuwa tunaonywa kula asali halafu baada ya muda mfupi ukila ndimu unakufa, tuliamini, lakini sikun hizi asali na ndimu kumbe ni dawa inayotibu vitu vingi.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…