Wasomi wa SUA wanalisaidia nini Taifa?

Wasomi wa SUA wanalisaidia nini Taifa?

LICHADI

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2015
Posts
4,491
Reaction score
12,560
Ni muda muafaka sasa tujadili hizi taasisi zinatusaidia nini kama Taifa maana kila kukicha bei za vyakula ni juu hasa mafuta ya kupikia na Ngano, serikali inaingia garama kubwa kuwalipa mishahara minono waprofesa na wataalam wengine wa kilimo katika hizi taasisi lakini sijui wanamchango gani kwa Taifa hawa.

Mpaka sasa Mafuta ya kula tunaagiza Nnje ya nchi kitu ambacho kimefanya matuta yamepanda sio mchezo kile kipimo kidogo cha sh 200 kwa sasa ni 700 hadi 800, ndoo ya lita 20 kwa sasa ni 110,000 hadi 120,000

Na bado tunajivunia tuna Chuo cha wataalam kilimo na tuna wasomi wa kilimo sasa hawa watu wanalisaidiaje Taifa wakati vitu muhim kama mafuta ya kula tunaagiza nnje wakati tuna Ardhi ya kutosha kulima mawese na na mimea mingine ambayo itatuletea mafuta ya kututosheleza bila kuagiza nnje

Ngano imetoka 1200 kwa sasa ni 2000, sababu tunaagiza nnje na huko nnje vita ya urusi na Ukraine ni sababu moja wapo maana inasemekana wanazalisha ngano kwa kiasi kikubwa kwa sasa hawauzi popote kwasababu ya vita na vikwazo alivyowekewa Urusi

Ukiingia mtaani chapati na vitu vingine bie ni juu sababu mafuta na ngano vimepanda kwa kasi ya ajabu,yote hayo ni kwa sababu vitu vya muhim kama hivi tunaagiza nnje hatuzalishi sisi wenyewe kwa kiwango kikubwa na kututosheleza wakati uwezo tunao

Hivi wasomi wetu wa sua kwa Ardhi tuliyonayo hatuwezi kulima ngano ikatutosha bila kuagiza nnje? Tatizo ni nyie au ni Serikali haitoi bajeti kubwa kwenu

Sua mnalisaidia nini Taifa kama bado tunaagiza vitu muhim nnje na nyie wataalam wa kilimo mpo?
 
Na sisi tunauliza taifa lina mpango gani na wasomi wa SUA? Maana limewasomesha then limeajiri asilimia kiduchu na wengine wameachwa watafute ajira kwenye soko huria.

Kama serikali ingetaka kuiokomboa nchi hii na njaa ingetenga mikopo maalum kwa wasomi hawa wakishindwa ndio unaweza kuwalaumu lakini hujawahi ona mpango kama huo ukifanyika.

Wasomi hawa wapo mtaani na wengine wanafanya kazi zisizohusu taaluma zao kama vile bodaboda n.k.
 
Na sisi tunauliza taifa lina mpango gani na wasomi wa SUA?maana limewasomesha then limeajiri asilimia kiduchu na wengine wameachwa watafute ajira kwenye soko huria. Kama serikali ingetaka kuiokomboa nchi hii na njaa ingetenga mikopo maalum kwa wasomi hawa wakishindwa ndio unaweza kuwalaumu lakini hujawahi ona mpango kama huo ukifanyika.Wasomi hawa wapo mtaani na wengine wanafanya kazi zisizohusu taaluma zao kama vile bodaboda n.k.
Acha liajiri tu kiduchu hawana msaada wowote kwa taifa naona wanaleta hasara tu
 
Elimu ya Tanzania kwa zaidi ya 80% haina manufaa yoyote na haiendani na matakwa wala maendeleo ya teknolojia.

Ni elimu duni yenye kulazimisha kukariri kuliko ubunifu.

Amini ukiwaachia nchi wachina miaka miwili tu kwenye sekta ya kilimo Tanzania inakuwa giant ya uzalishaji wa mazao ya kilimo.

Kiufupi sisi watanzania tuko duni kuanzia viongozi wetu, wataalamu wetu, na wananchi wenyewe.

Ni wavivu wa kufikiri, kuamua na kutenda.
 
Kuna Professor Mashingo kule.....Kazi kweli kweli
 
Kwa hiyo hoja yako nini funguka.
Haja yangu ni hawa wasomi wanaisaidia vipi nchi maana hawa ndio walitakiwa waishauri serikali lakini wapo bado tunaagiza vitu nnje badala ya kuzalisha wenyewe
 
Leo hii binafsi serikali ingekuwa inaweza kunikopesha walau trekta kwa dhamana ya cheti changu nakuhakikishia nipo tayari kuacha kazi ya serikali ya laki tisa maana fursa za kilimo zipo nyingi sana mtaani lakini nashindwa mtaji tu,

lakini kwa serikali hii ili ukopeshwe lazima uwe na collateral za maana hususani nyumba iliyopo mjini bila boost ya mkopo ni ngumu sana kuona mchango wetu tangible maana kilimo cha kujikimu(subsistence farming)tunafanya lakini kilimo cha kusaidia taifa na kutoa ajira kinahitaji mkono wa serikali.
 
Taja kwanza chuo chako tuone kimesaidia nini taifa.
Mimi ni msomi wa darasa la saba nimehitimu mwaka 1999, baada ya hapo nikaingia kwenye kilimo cha mpunga huku mlMbeya kuanzia mwaka 2003 hadi sasa nalima mpunga mimi sio msomi lakini nimelisaidia Taifa kutoagiza mchele nnje upo wa kutosha yani

Sasa nyie wasomi mtueleze elilu yenu mmeisaidia nini serikali kutoagiza mafuta ya kula na ngano nnje ya nnchi
 
Leo hii binafsi serikali ingekuwa inaweza kunikopesha walau trekta kwa dhamana ya cheti changu nakuhakikishia nipo tayari kuacha kazi ya serikali ya laki tisa maana fursa za kilimo zipo nyingi sana mtaani lakini nashindwa mtaji tu,lakini kwa serikali hii ili ukopeshwe lazima uwe na collateral za maana hususani nyumba iliyopo mjini bila boost ya mkopo ni ngumu sana kuona mchango wetu tangible maana kilimo cha kujikimu(substance farming)tunafanya lakini kilimo cha kusaidia taifa na kutoa ajira kinahitaji mkono wa serikali.
Acha tu yani
 
Haja yangu ni hawa wasomi wanaisaidia vipi nchi maana hawa ndio walitakiwa waishauri serikali lakini wapo bado tunaagiza vitu nnje badala ya kuzalisha wenyewe
Ulishawahi sikia nchi yetu pamoja na umasikini wetu tumekumbwa na baa la njaa kiasi cha kuagiza chakula nje ukiacha kipindi kile nchi imeingia vitani na Uganda?

Basi kama hilo halijatokea tambua wasomi hawa wamesaidia, na kama unabisha njoo na takwimu.
 
Back
Top Bottom