Wasomi wetu na mustakabali wa Tanzania yetu ya baadaye

Wasomi wetu na mustakabali wa Tanzania yetu ya baadaye

Wazo la kabwela

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2013
Posts
1,812
Reaction score
1,373
Maisha yalibadilika, wasomi (wetu) wakaanza kuziona thamani zao katika ombwe la utupu. Walishindwa kuthamini hata vyungu vilivyowapika wakajiona wameiva. Wengine waliamua kujiita wamepikwa matopeni. Lakini kubwa ni kwamba tuna falsafa. Itikadi ambazo zinafumbatwa katika lugha zetu. Pengine matopeni tutokako ni falsafa inayofumbatwa katika lugha.

Usomi ulituburuza na kutuingiza katika usasa. Tukaona kila kitu ni kipya. Tukafurahia uvumbuzi wao wa neno uhalisiajabu ( magic realism) na kuona tumeletewa dhana na mtindo mpya. Wengine waligundua hila za kujitukuza kwao lakini wenye akili zao wakasema: tuliwawahi kitambo katika fasihi nenwa yetu. Huo ni urejelezi tu.

Wakaendelea kutufanya tuone upya katika tathmini ya uzuri na ubaya wa falsafa yetu. Wakaleta ujumi mweusi. Eti wakadhani wanatuengua na miktadha ya uzuri na ubaya was falsafa yetu tuliyoifumbata toka nyakati zileeeeeee za mila desturi na tamaduni zetu. Hivi hawajui katika fumbato la istilahi hizo tunaweza rejelea falsafa zetu kwa jina la omorembe? Wamefanikiwa kucheza na akili zetu za kutofautisha vitu visivyotofautika Pengine ni uenguaji wa majambo kitaaluma) au ubinafsi wa kukumbatia maarifa?

Nimebaki naduwaa. Naendelea kuwaza ufutuhi, uramsa, utanzia nao umeleta upya? Pengine upya nikatika uga wa kitaaluma.

Lakini bado nasafiri. Natafuta majibu. Natamani mdahalo wa kifalsafa. Inshalaah! Wapo wanafalsafa wachanga watayavumbua haya.

Wataleta upya uliofumbatwa katika urazini wenye asili yetu na sio wa mwigo!
 
Usomi ni usomi na Siasa ni siasa.

Ukimuona mwanasiasa msomi ujue ana kofia mbili.

1. Usomi
2. Siasa

Kila kitu kinatumika kwa wakati wake. Bahati mbaya sana wakati wa kufanya Elimu siasa haihitajiki na wakatiwa kufanya Siasa, elimu haihitajiki.
 
Kuna msemo naupenda sana huu hapa:

:~ Mwanasiasa akikwambia nje kuna giza toka ndani ukahakikishe kweli kuna giza!
:~ Msomi akikwambia jua limezama huwezi kuhesabu namba jaribu kwa ukimya ili uhakikishe ulichoambiwa.

note: AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO.
 
Back
Top Bottom