Wassira amgomea JPM, asema halipi deni la Commodity Import Support. Akataa wito, Task Force kutuma Polisi. Yeye adai yuko tayari kupigwa pingu!

Wassira amgomea JPM, asema halipi deni la Commodity Import Support. Akataa wito, Task Force kutuma Polisi. Yeye adai yuko tayari kupigwa pingu!

kama mnajenga chuki dhidi yake naye atajenga chuki dhidi yenu
Kukujibu kipande hiki tu kifupi, na kuacha hayo mengine ambayo pia sio kweli.
Kiongozi hatakiw i"kujenga chuki" dhidi ya kundi lolote. Sitaona ajabu usipoelewa nilichosema hapa.

Kujenga chuki kwa kiongozi ndiko kunakosababishi mitafaruku hii na mivuruganyo kati ya sisi kwa sisi. Sifa hii ndio inayomwondolea heshima kubwa ambayo angekuwa amekwishaipata baada ya kufanya haya mengi unayosifia hapo juu.
 
Kukujibu kipande hiki tu kifupi, na kuacha hayo mengine ambayo pia sio kweli.
Kiongozi hatakiw i"kujenga chuki" dhidi ya kundi lolote. Sitaona ajabu usipoelewa nilichosema hapa.
Kujenga chuki kwa kiongozi ndiko kunakosababishi mitafaruku hii na mivuruganyo kati ya sisi kwa sisi. Sifa hii ndio inayomwondolea heshima kubwa ambayo angekuwa amekwishaipata baada ya kufanya haya mengi unayosifia hapo juu.
Hizo ni kanuni tu...lakini kama mwanadamu mf ww je ungeendelea kujenga urafiki na hao? Watu wasiokubaliana na unachofanya,watu wanaosambaza sumu kwa watu dhidi yako...bila shaka kuna chuki fulani utajenga dhidi yao...huwezi mfurahia mpinzani wa namna hii...japo demokrasia inabidi ifuatwe..
 
Hizo ni kanuni tu...lakini kama mwanadamu mf ww je ungeendelea kujenga urafiki na hao? Watu wasiokubaliana na unachofanya,watu wanaosambaza sumu kwa watu dhidi yako...bila shaka kuna chuki fulani utajenga dhidi yao...huwezi mfurahia mpinzani wa namna hii...japo demokrasia inabidi ifuatwe..
Hakuna lazima ya 'kujenga urafiki' na hao wanaokushambulia ukiwa kiongozi, kama isivyohitaji 'kujenga chuki' zidi yao.
Kama kiongozi anafanya kazi yake na raia kwa ujumla wanaiona, kuna lazima gani ya kuhangaika na hayo ya 'urafiki' na kujengeana chuki?
Hukuona iliposemekana 'watu wanakwenda kuunga mkono juhudi', au hizi pia zilikuwa mbwewmbwe za chuki?
 
Hapo sidhani kama rafiki yake Mzindakaya atakosekana!
Si ulimuona akijitambulisha kama mfanyabiashara mzee kuliko wote? Walizoea kukopa na kutokomea na madeni kwa jina la siasa. Sasa yabidi walipe hata kama ni kwa pressure ya kutoa roho, warithi wadaiwe.
 
Kumekucha!

Steven Wasira,mmoja wa wadaiwa sugu wa mfuko wa Commodity Import Support amesema hatalipa deni hilo kamwe na kwamba yeye si mmoja wa wadaiwa wa mabilioni hayo.

Wasira ambaye anakiri kukopa milioni mia moja miaka ya tisini,anasema alikuwa na makubaliano ya kulipa benki ya T.I.B, na kwamba makubaliano hayo yalifanywa wakati Mkurugenzi wa Benki hiyo,na mtuhumiwa wa ufisadi,bwana Peter Noni akiwa mamlakani.

Cha ajabu,Benki hakuna kumbukumbu za kulipa deni kama Wasira anavyosema alilipa, na hana hata barua ya Benki kuonyesha kwamba imethibitisha kwamba kalipa na hadaiwi, wasira ana maneno tu hana documents za benki kuonyesha uthibitisho kwamba hadaiwi,je mchezo ulichezwa hela ikarudi kwa wasira,hivyo Wasira anaweza kuwa ametakatisha pesa?

Muda wote anaimba "noni,noni,noni"

Je Wasira na kundi lake la awamu ya tano walikuwa wanashinikiza na kuwatisha watendaji wawafutie madeni yao kiaina? Anasema aliachana na kampuni iliyokopa akaenda kufanya siasa,sasa kwa nini Benki au yeye aambiwe na Benki aiandikie ili ifute deni wakati yeye si mtumishi wa kampuni ya SIZYA COLD STORAGE?

Wasira alikopa milioni 100 miaka ya tisini,anataka alipe hizo pesa hivyo hivyo bila riba! Amekopa miaka 30 iliyopita?!

Haiwezekani, akamatwe na apewe kesi ya uhujumu uchumi,tena anamgomea Rais wa Jamhuri ya Muungano ! Anajiamini nini huyu mtu?hajui hii ni awamu ya tano!

Asomeshwe namba,

Unadhani ni kwa nini watu aina ya Wassira hujiunga ccm?
 
Hivi nyinyi mnawajua ccm au mnawasikia ,mle nani sio mwizi ? Nani sio fisadi ? ccm ni kundi la wapigaji wanaokula kwa zamu hakuna msafi hata mmoja .Wote wana kashfa za hatari hata huyu mpigaji mzalendo ndio hatari zaidi .
 
Chuma hufua chuma, ni mwendo wa Roho mkononi
 
Bongo kama Ulaya awamu hii..kwa watu kukumbushwa madeni na ukatishaji pesa na kutolipa kodi...
 
Ukikuta mtu kafanya jambo akaungwa mkono kwa asilimia mia moja ujue hiyo jamii imepoteza uwezo wa kufikiri. Halafu mimi sio msemaji wa upinzani.
Labda ungeniluliza mimi namuunga mkono kwenye yapi. Elimu bure hili namuunga mkono ila angeenda mpaka form 6, kisha huko vyuoni watu wapate mikopo. Kutokukatika hovyo kwa umeme kwa eneo nililopo. Kuwatimua Nape na mwigulu uwaziri kwani ni watu waliopandikiza siasa za ukatili na hila na sasa yeye anaziendeleza.
Simuungi mkono kwenye ununuzi wa ndege kwa sasa kwani ni biashara Mtambuka, bali alipaswa awekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji au kujenga viwanda wangalau kila mkoa au kila kanda vya 30b-50b vitoe ajira kwa vijana. Kwa hiyo kwamba anapingana kila kitu ni lugha ya upotoshaji. Ufahamu hata saa mbovu kuna wakati inasema sawa.
Sawa mkuu nimekuelewa ndo maana nikasema baadhi ya wapinzani na sio wote ambapo wengi wao ni wale walionywesha sumu na kukaririshwa hasa vijana wa siku hizi...
But nashindwa kuelewa kwa nn mnamfananisha na vitu vibovu...sijui saa mbovu mara shetani..,hii ndo chuki ninayoisemea sasa..
 
Hakuna lazima ya 'kujenga urafiki' na hao wanaokushambulia ukiwa kiongozi, kama isivyohitaji 'kujenga chuki' zidi yao.
Kama kiongozi anafanya kazi yake na raia kwa ujumla wanaiona, kuna lazima gani ya kuhangaika na hayo ya 'urafiki' na kujengeana chuki?
Hukuona iliposemekana 'watu wanakwenda kuunga mkono juhudi', au hizi pia zilikuwa mbwewmbwe za chuki?
Je,mliwachukuliaje hao waliosema wanakwenda kuunga mkono juhudi za rais??.....mlikubaliana nao kwa moyo mnyoofu kweli?
 
Fisiem ni fisiem tu
Wanakula nchi saaaaaana
 
Back
Top Bottom