Wassira: Ieleweke wazi tunapoandika Katiba Mpya Sera ya CCM ni Serikali 2 kuelekea 1 na Siyo vinginevyo

Wassira: Ieleweke wazi tunapoandika Katiba Mpya Sera ya CCM ni Serikali 2 kuelekea 1 na Siyo vinginevyo

Mzee Wassira kupitia mahojiano maalum yaliyofanywa na TBC yakimuhusisha pia Zitto Kabwe wa ACT Wazalendo amesema Sera ya CCM kuhusu muundo wa Serikali haitabadilika.

Wassira amemwambia Zitto Kabwe kwamba Ukitaka Serikali 3 ujue hakuna Katiba Mpya itakayopatikana.

Ukweli Mchungu!
Ningekuwa na uwezo hiki kisiwa ningekitupilia mbali, marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
 
Mzee Wassira kupitia mahojiano maalum yaliyofanywa na TBC yakimuhusisha pia Zitto Kabwe wa ACT Wazalendo amesema Sera ya CCM kuhusu muundo wa Serikali haitabadilika.

Wassira amemwambia Zitto Kabwe kwamba Ukitaka Serikali 3 ujue hakuna Katiba Mpya itakayopatikana.

Ukweli Mchungu!
Ila huyu mzee tokea enzi za Nyerere hadi kwa madam bado ana sauti na ushawishi haya aliyoyasema kayatoa wapi, mzee huyu hana tofauti na mzee Makamba wote ni walamba asali.
 
Ila huyu mzee tokea enzi za Nyerere hadi kwa madam bado ana sauti na ushawishi haya aliyoyasema kayatoa wapi, mzee huyu hana tofauti na mzee Makamba wote ni walamba asali.
Lakini ndio ukweli wenyewe huo!
 
Nawaza nikiwa na phd kama ya babutale na msukuma..... hivi haiwezekani kuandaa uchaguzi ambao tutaweka katiba tatu 1. Ya Warioba 2. Iliyopendekezwa na bunge la Sitta 3. Ya 1977 ili tujue wananchi wanapenda ipi sio wanasiasa wanapenda ipi kama ilivyo sasa
 
Ningekuwa na uwezo hiki kisiwa ningekitupilia mbali, marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Alishawajua ni wabishi walalamishi na sio wa kuburutwa burutwa kirahisi rahisi au aliwaonaje hasa mpaka akasema vile ?? 🤣🤣🤣
 
CCM na Yanga Ndio Wananchi wenyewe!
Wananchi wa Nchi gani?Maana hafahamu kuwa kabla ya 1964 lilikuwa na Tanganyika Huru na Zanzibar Huru,Muungano ulikujaje vile?
Kwanini Tanganyika ipoteze vyote kwa sirini Zanzibar ikibakiziwa kila kitu isipokuwa mamlaka?
Muungano wetu unawakandamiza na kuwapendelea wahusika wake?CCM ni zao la TANU&ASP na Muungano ni kwa Watanzania bila kujali wenye vyama na wasio na vyama,kwanini CCM itusemee tusiokuwa wanachama wake?
Tunataka Katiba itakayoweka aina ya Muungano wenye maslahi ya Wananchi na siyo vyama vya Siasa.
 
Lengo ni kuelekea kwenye serekali moja, ukiongeza ya tatu, itakuwaje? Hapa kwenye mbili ndio rahisi kuelekea kwenye moja!, yenye maendeleo yenye uwiano sawa! Kwa kila kipande ndani ya muungano wetu.
Kwenda kwenye serikali moja ni kuuwa nchi moja jambo ambolo hakuna upande utakaokubali
 
Huyo ni

Mjumbe wa kamati kuu ya chama,huenda ndiyo msimamo wa chama,lakini chama hakiwezi kuwa na nguvu zaidi kuliko Watanzania akiwepo na yeye. Upeo wa kuzeeka kifikra na kimwili kumbe viko sawa.
Huenda yeye kwa hili ni supika tu !
 
Hakuna nch
Sio kweli, unajua rasi wa zanzibr anateuliwa/kupendekezwa na Tanzania bara?
Hakuna nchi inaitwa Tanzania bara,tuna nchi inaitwa Tanzania. Nchi ya Tanganyika iliuwawa na Muungano wa nchi ya Zanzibar. Leo Muungano ukifa hatuna nchi,sijajua tutasimamia wapi,na hakuna aliyewahi kuuliza hivi Muungano ukifa sisi tutabaki na nini?
 
Hakuna nch

Hakuna nchi inaitwa Tanzania bara,tuna nchi inaitwa Tanzania. Nchi ya Tanganyika iliuwawa na Muungano wa nchi ya Zanzibar. Leo Muungano ukifa hatuna nchi,sijajua tutasimamia wapi,na hakuna aliyewahi kuuliza hivi Muungano ukifa sisi tutabaki na nini?
Pweinti
 
Sio kweli, unajua rasi wa zanzibr anateuliwa/kupendekezwa na Tanzania bara?
Hakuna nchi inaitwa Tanzania bara tuna nchi inaitwa Tanzania. Muungano ukivunjika hatuna tutakachobaki nacho,kwa sababu zanzibar na Tanganyika ndiyo iliyozalisha Tanzania na kuuwa Tanganyika,lakini Zanzibar imeendelea kusimama imara mpk kesho. Tuna rais wa JMT na Zanzibar wana rais wa serikali ya mapinduzi,sisi marehemu Tanganyika hatuna rais,tumejificha kwenye kwapa la Muungano.
 
Back
Top Bottom