DOKEZO Wastaafu wa TAZARA tunasotea stahiki zetu huu Mwaka wa 20, Rais Samia tusaidie

DOKEZO Wastaafu wa TAZARA tunasotea stahiki zetu huu Mwaka wa 20, Rais Samia tusaidie

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mama kumbe anatoa milioni 10 kuununua kila goli la simba na Yanga wakati Kuna watu wanadai fedha zao?

Huyu rais vipi hana vipaumbele??
 
Pesa zipo za magoli tu na kuwa safirisha mashabiki kushangilia team
Nyie wazee wa Tazara mtulie tu

Ova
 
Mzazi wangu ni mmoja wa Wazee ambao wamestaafu utumishi katika Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), mzee wangu na wenzake wengi waliostaafu Mwaka 2004, 2005 na 2006 hawajalipwa stahiki zao licha ya kufanya jitihada kubwa ya kushughulikia.

Naandika andiko hili kwa maelekezo ya Mzee wangu ambapo anachokisema ndicho nakiandika...

Mimi na Wazee wenzangu tupo zaidi ya 180 tumefanya jitihada kubwa tangu wakati huo hadi leo ikiwa ni takribani miaka 20 bila mafanikio huku Serikali ikituzungusha.

Wazee wachache ambao wana ndugu kwenye nafasi za juu Serikalini wao walifanikiwa kupata msaada na wakalipwa.

Waliolipwa walikuwa na ndugu au jamaa katika nafasi za Uwaziri na nyinginezo lakini sisi huku ambao naweza kusema ‘hatujuani na Wakubwa’ tumeambulia patupu bado tunateseka kufuatilia.

Kuna wenzangu kadhaa wameshapoteza maisha bila kupata stahiki zao, familia zao zimepambana nazo hazijafanikiwa.

Uhakiki wa madai yetu ulishafanyika na Serikali ikathibitisha tangu kipindi cha Rais Jakaya Kikwete hadi cha hayati Magufuli, ambapo tulionana hadi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikathibitishwa kuwa tunatakiwa kulipwa lakini hilo halijatekelezeka.

Suala letu lilifika hadi Mahakamani tukashinda shauri, baada ya hapo tukaonana na Waziri Mkuu kuwasilisha malalamiko yetu, akatusikiliza na akatukabidhi kwa maafisa wake washughulikie lakini tangu wakati huo danadana zimekuwa nyingi.

Wengi wetu wanaendelea kuteseka, wengine wanaumwa, jasho letu tulilolitoa kwa ajili ya Taifa linapotea, tunamasononeko, familia zetu zinamasononeko dhidi ya Serikali yetu kwa hiki kinachoendelea.

Mara kadhaa nimewashawishi wenzangu twenden kwenye Vyombo vya Habari kueleza changamoto zetu, hawataki kwa kuwa wengi wetu ni Wazee wa CCM na wakereketwa hasa, wenzangu wanaamini tukisema kwa Waandishi tunaweza kukiharibia chama, jambo ambalo mimi napingana nalo kwa kuwa ukimya wetu ndio anguko letu hadi tunakufa.

Taarifa zilizopo ni kuwa fedha tunazotakiwa kulipwa zipo Hazina na kuna wakati inadaiwa zimekuwa zikitoka na kurejea, kwa maana zinaingia katika matumizi mengine kisha zinarejeshwa.

Tumejuaje hilo? Harakati hizi za kwenda huku na huku zimetuwezesha kukutana na baadhi ya watu wa karibu na Mamlaka za juu wa Serikali ambao wanajua sakata hilo na wamekuwa wakitudokeza kuhusu hilo, kama ni kweli au la hilo sina uhakika.

Sisi Wastaafu wengi tuna hali mbaya sana kiuchumi, wengi tupo Dar na wengine wapo mikoa tofauti, tumeenda huku na huku bila mafanikio, yaani kwa ufupi tunatapatapa na imekuwa kawaida kuombaomba nauli kwa watu tofauti, ni aibu lakini hatuna jinsi.

Inaniuma sana kuona Watanzania tuliopambana kwa nguvu zetu zote kwa ajili ya Taifahiki haya ndio matunda.

Tumaini letu pekee limebaki kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwani kauli yake inaweza kuwa na nguvu ya kuweza kutusaidia kupata haki yetu.
Tazara Ina changamoto kubwa sana,ni sawa na mtoto aliekosa walezi...hadi kufikia Leo April 3 mishahara ya march haijalipwa na hakuna maelezo yakueleweka.
 
Mara kadhaa nimewashawishi wenzangu twenden kwenye Vyombo vya Habari kueleza changamoto zetu, hawataki kwa kuwa wengi wetu ni Wazee wa CCM na wakereketwa hasa, wenzangu wanaamini tukisema kwa Waandishi tunaweza kukiharibia chama, jambo ambalo mimi napingana nalo kwa kuwa ukimya wetu ndio anguko letu hadi tunakufa.
Na hili ndilo tatizo kuu..
Binafsi mzee wangu ni muhanga ktk hilo na nadhani yupo pa1 na mzee wako ktk kufuatilia suala hili.
Nilimwambia wakitaka kufanikiwa ktk hili waache kujinasibisha na ccm, badala yake wawatumie upinzani wenye sauti kuwapgia kelele.
Laah..
Nimeonekana mjinga na mtoto mdogo nisie mzalendo.
 
Kuna mzee wangu mmoja pia yumo kwenye hii issue , hawa wazee wanataabika sana . Mh. Rais tunaomba uangalie hawa wazee wanataabika sana.
 
Push back ya kupata katiba mpya,issue hii ingeenda kwenye mahakama huru na yenye kujitegemea na haki ingetolewa,waziri mhusika angewekewa garnish ya kimahakama na kuwajibishwa yeye binafsi kwa uchelewesho kwa sasa wazee wangu wa TAZARA mpo kaput moja na wazee wa EAC ,mtakufa mmoja baada ya mwingine
 
Mzazi wangu ni mmoja wa Wazee ambao wamestaafu utumishi katika Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), mzee wangu na wenzake wengi waliostaafu Mwaka 2004, 2005 na 2006 hawajalipwa stahiki zao licha ya kufanya jitihada kubwa ya kushughulikia.

Naandika andiko hili kwa maelekezo ya Mzee wangu ambapo anachokisema ndicho nakiandika...

Mimi na Wazee wenzangu tupo zaidi ya 180 tumefanya jitihada kubwa tangu wakati huo hadi leo ikiwa ni takribani miaka 20 bila mafanikio huku Serikali ikituzungusha.

Wazee wachache ambao wana ndugu kwenye nafasi za juu Serikalini wao walifanikiwa kupata msaada na wakalipwa.

Waliolipwa walikuwa na ndugu au jamaa katika nafasi za Uwaziri na nyinginezo lakini sisi huku ambao naweza kusema ‘hatujuani na Wakubwa’ tumeambulia patupu bado tunateseka kufuatilia.

Kuna wenzangu kadhaa wameshapoteza maisha bila kupata stahiki zao, familia zao zimepambana nazo hazijafanikiwa.

Uhakiki wa madai yetu ulishafanyika na Serikali ikathibitisha tangu kipindi cha Rais Jakaya Kikwete hadi cha hayati Magufuli, ambapo tulionana hadi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikathibitishwa kuwa tunatakiwa kulipwa lakini hilo halijatekelezeka.

Suala letu lilifika hadi Mahakamani tukashinda shauri, baada ya hapo tukaonana na Waziri Mkuu kuwasilisha malalamiko yetu, akatusikiliza na akatukabidhi kwa maafisa wake washughulikie lakini tangu wakati huo danadana zimekuwa nyingi.

Wengi wetu wanaendelea kuteseka, wengine wanaumwa, jasho letu tulilolitoa kwa ajili ya Taifa linapotea, tunamasononeko, familia zetu zinamasononeko dhidi ya Serikali yetu kwa hiki kinachoendelea.

Mara kadhaa nimewashawishi wenzangu twenden kwenye Vyombo vya Habari kueleza changamoto zetu, hawataki kwa kuwa wengi wetu ni Wazee wa CCM na wakereketwa hasa, wenzangu wanaamini tukisema kwa Waandishi tunaweza kukiharibia chama, jambo ambalo mimi napingana nalo kwa kuwa ukimya wetu ndio anguko letu hadi tunakufa.

Taarifa zilizopo ni kuwa fedha tunazotakiwa kulipwa zipo Hazina na kuna wakati inadaiwa zimekuwa zikitoka na kurejea, kwa maana zinaingia katika matumizi mengine kisha zinarejeshwa.

Tumejuaje hilo? Harakati hizi za kwenda huku na huku zimetuwezesha kukutana na baadhi ya watu wa karibu na Mamlaka za juu wa Serikali ambao wanajua sakata hilo na wamekuwa wakitudokeza kuhusu hilo, kama ni kweli au la hilo sina uhakika.

Sisi Wastaafu wengi tuna hali mbaya sana kiuchumi, wengi tupo Dar na wengine wapo mikoa tofauti, tumeenda huku na huku bila mafanikio, yaani kwa ufupi tunatapatapa na imekuwa kawaida kuombaomba nauli kwa watu tofauti, ni aibu lakini hatuna jinsi.

Inaniuma sana kuona Watanzania tuliopambana kwa nguvu zetu zote kwa ajili ya Taifahiki haya ndio matunda.

Tumaini letu pekee limebaki kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwani kauli yake inaweza kuwa na nguvu ya kuweza kutusaidia kupata haki yetu.
Mkiambiwa muandamane ili katiba irekebishwe tupate viongozi wenye hekima mnajifungia ndani.
 
Nafurahia msaatfu kuteseka kwasababu ndo hao walisababishia vijana wao wa Leo khali ngumu ya Maisha,(ndo walikuwa watunga Sera, wala RUSHWA, Wapiga vigelegele usalama wa TAIFA, watunga Sera). Leo vijana wanakosa shukran kwao kwasaba nao hawakuona kesho ya TAIFA lao . Huu utaratib ndo M40 pekee utakapo ibua vinyongo Kwa JAMII nakuweka vizur TAIFA. Tunateswa na imana kuwa serikali iko kwa maslah ya watu wake kumbe sio kweli NI kwamaslahi ya familia zao na mabeberu walifaidi nchi hii..tufika hatua ya kuwa tunaumizwa na matatizo yaliyoko Kwa jirani /IDARA,ofisi kwa uzalendo bwa kweli TAIFA litasshinda.
Nakubaliana na wewe
 
Huo mchezo mchafu ,wa kunyima wastaafu haki ya msingi upo siku nyingi sana,kuna wale pia wazee wa kiwanda cha viatu(Bora) wamedai mpaka basi na hakuna aliyesikiliza kilio chao na kwa Sasa wengi wao ni marehemu.
Wakome mpk waanze kuandamana
 
Mzazi wangu ni mmoja wa Wazee ambao wamestaafu utumishi katika Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), mzee wangu na wenzake wengi waliostaafu Mwaka 2004, 2005 na 2006 hawajalipwa stahiki zao licha ya kufanya jitihada kubwa ya kushughulikia.

Naandika andiko hili kwa maelekezo ya Mzee wangu ambapo anachokisema ndicho nakiandika...

Mimi na Wazee wenzangu tupo zaidi ya 180 tumefanya jitihada kubwa tangu wakati huo hadi leo ikiwa ni takribani miaka 20 bila mafanikio huku Serikali ikituzungusha.

Wazee wachache ambao wana ndugu kwenye nafasi za juu Serikalini wao walifanikiwa kupata msaada na wakalipwa.

Waliolipwa walikuwa na ndugu au jamaa katika nafasi za Uwaziri na nyinginezo lakini sisi huku ambao naweza kusema ‘hatujuani na Wakubwa’ tumeambulia patupu bado tunateseka kufuatilia.

Kuna wenzangu kadhaa wameshapoteza maisha bila kupata stahiki zao, familia zao zimepambana nazo hazijafanikiwa.

Uhakiki wa madai yetu ulishafanyika na Serikali ikathibitisha tangu kipindi cha Rais Jakaya Kikwete hadi cha hayati Magufuli, ambapo tulionana hadi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikathibitishwa kuwa tunatakiwa kulipwa lakini hilo halijatekelezeka.

Suala letu lilifika hadi Mahakamani tukashinda shauri, baada ya hapo tukaonana na Waziri Mkuu kuwasilisha malalamiko yetu, akatusikiliza na akatukabidhi kwa maafisa wake washughulikie lakini tangu wakati huo danadana zimekuwa nyingi.

Wengi wetu wanaendelea kuteseka, wengine wanaumwa, jasho letu tulilolitoa kwa ajili ya Taifa linapotea, tunamasononeko, familia zetu zinamasononeko dhidi ya Serikali yetu kwa hiki kinachoendelea.

Mara kadhaa nimewashawishi wenzangu twenden kwenye Vyombo vya Habari kueleza changamoto zetu, hawataki kwa kuwa wengi wetu ni Wazee wa CCM na wakereketwa hasa, wenzangu wanaamini tukisema kwa Waandishi tunaweza kukiharibia chama, jambo ambalo mimi napingana nalo kwa kuwa ukimya wetu ndio anguko letu hadi tunakufa.

Taarifa zilizopo ni kuwa fedha tunazotakiwa kulipwa zipo Hazina na kuna wakati inadaiwa zimekuwa zikitoka na kurejea, kwa maana zinaingia katika matumizi mengine kisha zinarejeshwa.

Tumejuaje hilo? Harakati hizi za kwenda huku na huku zimetuwezesha kukutana na baadhi ya watu wa karibu na Mamlaka za juu wa Serikali ambao wanajua sakata hilo na wamekuwa wakitudokeza kuhusu hilo, kama ni kweli au la hilo sina uhakika.

Sisi Wastaafu wengi tuna hali mbaya sana kiuchumi, wengi tupo Dar na wengine wapo mikoa tofauti, tumeenda huku na huku bila mafanikio, yaani kwa ufupi tunatapatapa na imekuwa kawaida kuombaomba nauli kwa watu tofauti, ni aibu lakini hatuna jinsi.

Inaniuma sana kuona Watanzania tuliopambana kwa nguvu zetu zote kwa ajili ya Taifahiki haya ndio matunda.

Tumaini letu pekee limebaki kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwani kauli yake inaweza kuwa na nguvu ya kuweza kutusaidia kupata haki yetu.
Kwani ni shilingi ngapi kwa ujumla wake wanadai wazee hawa? Je, bilioni 10, 20 au 60?

Hata iwe shilingi ngapi, hivi hii serikali ya CCM inashindwa kweli kuondoa kelele za wazee hawa kiasi cha kuleta laana na balaa kwa taifa hili kwa kushindwa kulipa bilioni 20 au 60 tu katika hazina ya taifa tajiri kama hili la Tanganyika?

Hivi kweli wana CCM nyie hamuoni aibu wala haya kudaiwa na wazee hawa wakati waziri mmoja tu wa CCM anaweza kununua nyumba mbili au tatu Dubai na Johannesburg - South Africa kwa bilioni 20?

CCM hamuoni aibu? Hawa vigogo wa CCM na serikali yenu wanatoa wapi pesa nyingi kiasi hiki ndani ya muda mfupi wakiwa viongozi wa umma kama sio kuwaibia Watanganyika wakiwemo hawa wazee wastaafu wa TAZARA, wa umma na taasisi zingine za umma?

Jamani epukeni hasira ya Mungu. Tendeni haki. Acheni dhuluma. Vinginevyo, tambueni kuwa machozi na vilio vya wazee hawa na Watanganyika kwa wingi wao kimeshamfikia Mungu huko juu mbinguni anakoketi na yuko tayari kushuka na kuachilia ghadhabu yake dhidi ya viongozi wa serikali hii na taifa letu kwa ujumla..

Tafadhali CCM, watu tumeshaomba sana Mungu ili aachilie rehema zake. Lakini mbona hamsikii wala kutenda yawapasayo kutenda?

Tafadhali, hebu nyie CCM liepusheni taifa hili na balaa hii toka ktk ghadhabu ya Mungu. Fanyeni yanayowapasa kutenda sasa. Mna muda mchache sana uliosalia..!!
 
Nyinyi ndiyo wapiga kura nambari moja wa CCM, hongereni sana
 
Back
Top Bottom