Wastara arejea, asema fedha za matibabu hazikutosha

Wastara arejea, asema fedha za matibabu hazikutosha

Dar es Salaam. Msanii wa filamu, Wastara Juma amerejea nchini leo akitokea Mumbay nchini India alikokuwa anapatiwa matibabu ya mgongo na mguu na kuwashukuru Watanzania kwa namna walivyojitokeza kumchangia fedha za matibabu, ingawa hazikutosha na kulazimika kuuza baadhi ya mali zake.
View attachment 703149
Akizungumza na MCL Digital leo Machi 1, 2018 nyumbani kwake Tabata ikiwa ni saa chache baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, amesema baada ya kufika hospitali alikutwa na matatizo mengine zaidi ya aliyokuwa nayo jambo lililosababisha gharama za matibabu kuwa kubwa.

Wastara alifanikiwa kwenda kwenye matibabu hayo, Februari 3, 2018 baada ya kupata michango kutoka kwa watu mbalimbali akiwemo Rais John Magufuli aliyemchangia Sh15 milioni.

Amebainisha kuwa matatizo aliyokutwa nayo ni pamoja na uvimbe chini ya kalio na kwamba, ndilo lilikuwa sababu ya kukaukiwa damu pamoja na kubainika kuwa na uvimbe kichwani uliotokana na kupata ajali zaidi ya mara tatu.

“Kutokana na matatizo haya ilifika mahali pesa nilizokwenda nazo ziliniishia na kulazimika kuwaomba ndugu zangu wauze baadhi ya mali zangu, ikiwemo kamera ili niweze kuendelea na matibabu,” amesema.

“Mtu umeshafika kwenye matibabu tena nchi za watu unafanyaje? Kurudi bila kutibiwa huwezi. Nililazimika kuwasiliana na ndugu zangu ili wauze baadhi ya vitu vyangu niweze kutibiwa maana afya yangu ni muhimu kuliko kamera.”
Sijui kwa nini huwa napataga shida kumuamini huyu mama,japokuwa sura yake imekaa kihuzuni huzuni tu!
 
Huyu dada huwa anashangaza sana, hivi hajui kuwa kuna watanzania maelfu walio hoi wasioweza hata kuongea au kuinuka vitandani?

Kwa Mtu mstaarabu anayejali kusaidiwa asingepaswa athubutu kusema hayo.

Ni kama wakati ule alipoumwa mwanzoni na kujitangaza akasaidiwa sana kisha akaenda tena kukata mauno na kujitonesha.

Kazi kujitonesha tu.

Asimkufuru Mungu.
Huyu dada hakuwahi kushukuru jamani kila siku yeye hatosheki tu. Simsemi vibaya lkn anawavunja moyo wanaomsaidia.
 
Hahaha
Wastara bwana... Inaonekana alitumia hela nyingi sana
 
Huyu binti bado hajitambui,wala kulikuwa hakuna haja ya kuzungumza habari za kamera hapa ,kuna watanzania wanakufa kwa kukosa laki tano tu,sembuse yeye au anajiona yeye ni wa thamani kuliko mtanzania mwingine???
 
Si nyie ndo mnapaga, ndio maana just kauza camera tu analaumu kwelu kweli inamuuma hajui anaemchangia kauza nini had kumchangia hiyo pesa! Kuna hela watu walimchangia ya karo ya mtoto na mwenye mtoto kakubali mtoto wake achelewe masomo.
Yeye camera tu kaita Media.
Hahaa
Jinga kabisa
 
Back
Top Bottom