Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,746
ha haaa, mdogo wangu.....dada kubwa we hutaki zilionea??
hela zinakuwa zingi zingi!!
Wastara Juma. IKIWA ni takribani mwaka mmoja tangu alipoondokewa na mumewe, marehemu Juma Kilowoko Sajuki, staa wa filamu Bongo, Wastara Juma amesema sasa yupo tayari kuolewa lakini sharti la kwanza la muoaji lazima awe mtu mwenye fedha zake. Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, wikiendi iliyopita jijini Dar es Salaam, Wastara alisema, amekuwa mpweke kwa muda mrefu na sasa ni wakati muafaka wa kumpata mtu wa kuziba pengo la marehemu mume wake.
Inatosha sasa, nadhani muda wa kuwa na mwenzangu umefika. Napenda huyo mwanaume awe mwenye huruma, upendo na kutambua thamani ya mke lakini ni vizuri akiwa mwenye kujituma na awe na fedha nyingi.
Natamani kuolewa na bilionea. Najua nikiwa na mwanaume wa aina hiyo sitateseka, nitapata kila ninachokitaka. Unajua mimi kama mwanamke nina mambo mengi. Siyo siri natamani itokee siku moja niendeshe Hummer au Prado (aina za magari) kulingana na hadhi yangu.
Kiukweli nitafurahi sana nikimpata mwanaume wa aina hiyo, maana nitakuwa na uhakika wa kufanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na kunisaidia katika shughuli zangu za sanaa, alisema Wastara.
naipenda nchi yangu! ina kila aina ya maajabu.
Nipo hapa,bilionea wa mapenzi[/QUOTE]
Wewe pumzika tu bwana,mapenzi aliyapata kwa Sajuki sasa hivi pesa ndio mpango mzima.......
Nipo hapa,bilionea wa mapenzi
Hii inaitwa busara mingi mingi!!!!!ha haaa, mdogo wangu.....
kwani Mungu aliponiumba na akili na utashi kama hao wanaume alikuwa kichaa? si alijua na mimi naweza tafuta hizo zilionea zangu mwanyewe?
yaani kabisa nalala nasubiri mtu wa kunilitea hela zingi zingi kwa ujira wa k? kabisaaaaaaa!
kweli tumetofautiana aisee
ha haaa, rafiki lazima ku-acknowledge mapenzi mingi mingi ya Mungu kwetu......Hii inaitwa busara mingi mingi!!!!!
Wastara..mbona Sajuki akiwa hai hukuwahi kumwambia kuwa unataka ajitume awe bilionea?? by the way mimi ni bilionea ila navusha ngada!! uko tayari??? maana tatizo si ni ubilionea tu na haijalishi umekujaje?
Wasanii wanahitaji washauri kabla ya kuongea kwenye media....
Neno moja linaweza kukushusha kabisaaaa...