Wataalam, Nahitaji uhakika wa umeme kwa vifaa vidogo kama laptop, simu, router, n.k. ikiwa kuna mgao wa siku 2, Je itanigharimu kiasi gani ?

Wataalam, Nahitaji uhakika wa umeme kwa vifaa vidogo kama laptop, simu, router, n.k. ikiwa kuna mgao wa siku 2, Je itanigharimu kiasi gani ?

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Inatokea Tanesco wamekata umeme kwa siku 2

Nahitaji vitu gani mfano battery au power bank,n.k. niweze kukidhi mahitaji ya umeme kwa siku 2 kwa vifaa vidogo kama
  • Smart phone 4 zinazochajiwa mara 2 kwa siku, hutumia lisaa kujaa
  • Router 1 inayotakiwa iwe kwenye umeme muda wote
  • Laptop 1 ya Dell
 
Tafuta power backup ila bei zake kidogo hua zimechangamka ila ni bora zaidi make nyingi hus na betri za Lithium, ukiwa na 800K - 1000Kutapata system itakayo kaa miaka mingi, hata ukisema utengeneze pia, kwa kununua inverter, battery, charge control na AC to DC charger bado ita range humo humo.
NB: Sijapigia solar make umedai una umeme, hii ni faida kwako.
 
Powerbank ya Laptop inafanya hio kazi, sema bei zake zinakua ndefu, kama Baba Rhobi alivyoshauri tafuta powerstation zipo hadi zenye kilo watts moja ama mbili vitu kama Laptop na simu utachaji hata mara 25-50.

Kwa ambazo zinaishia volt 9 mpaka laki 2 unapata sema itabidi uangalie na laptop yako kama inachajika na hizo volt na ina type C kupokea umeme, kama ni laptop ya zamani haitakubali.

Powerstation kubwa zinatoa Volt 220-240 kama umeme wa kawaida majumbani sema bei ndefu bei rahisi labda laki 5 na haitafika KW 1 kwa hio bei labda watts 500-600.
 
Back
Top Bottom