John mungo
JF-Expert Member
- Dec 8, 2013
- 1,008
- 1,028
Habari za Jumapili,
Kuna mtu alikuwa anamsafirisha mgonjwa ambae tayari alikua Mwathirika wa VVU. Sasa kwa bahati mbaya gari likapata ajali na wote kuumia vibaya kiasi cha kuvuja damu nyingi.
Sasa baada ya kutoa msaada kwa majeruhi na kukimbizwa hospital sasa, kuna kijana aliumizwa na bati katika pilika za uokozi na akawa amepata jeraha na aligusa zile damu za majeruhi.
Watu wakaanza kusikitika kuwa jamaa atakuwa ameathirika. Ila wakati tunajadili juu ya hilo, kuna dada mmoja akamweleza yule jamaa kuwa aende hospital ya Serikali, aende kitengo cha UKIMWI kabla ya masaa 72 atapatiwa dawa ya kukinga virusi kwa njia ya sindano na inaitwa PEP, hataathirika.
Sasa Madokta naomba mtufahamishe kuwa; Je, hiyo sindano ipo? Na ni kweli mtu ukiwahi kupata kinga hiyo ndani ya masaa 72 kuna uwezekano wa kupona?
Tafadhali Madokta tujuzeni nasi tujue jambo hilo kama lipo kweli.
Siku njema.
Kuna mtu alikuwa anamsafirisha mgonjwa ambae tayari alikua Mwathirika wa VVU. Sasa kwa bahati mbaya gari likapata ajali na wote kuumia vibaya kiasi cha kuvuja damu nyingi.
Sasa baada ya kutoa msaada kwa majeruhi na kukimbizwa hospital sasa, kuna kijana aliumizwa na bati katika pilika za uokozi na akawa amepata jeraha na aligusa zile damu za majeruhi.
Watu wakaanza kusikitika kuwa jamaa atakuwa ameathirika. Ila wakati tunajadili juu ya hilo, kuna dada mmoja akamweleza yule jamaa kuwa aende hospital ya Serikali, aende kitengo cha UKIMWI kabla ya masaa 72 atapatiwa dawa ya kukinga virusi kwa njia ya sindano na inaitwa PEP, hataathirika.
Sasa Madokta naomba mtufahamishe kuwa; Je, hiyo sindano ipo? Na ni kweli mtu ukiwahi kupata kinga hiyo ndani ya masaa 72 kuna uwezekano wa kupona?
Tafadhali Madokta tujuzeni nasi tujue jambo hilo kama lipo kweli.
Siku njema.