Wataalamu wa mifupa, ushauri tafadhali

Samboko

JF-Expert Member
Joined
Oct 30, 2011
Posts
5,420
Reaction score
7,788
Nina maumivu makali sana ya kiuno kwa muda sasa nimeenda hospital nimefanyiwa vipimo mbalimbali hadi XRAY nikapewa dawa kadhaa za kupaka na kumeza, leo cku ya tatu tangu nianze dozi lkn sioni mabadiliko yoyote,



Hayo ni majibu ya xray,
Naomba mnisaidie jinsi ya kufanya nipone haraka maana hata kazi nimesimama kwa mda kwa sababu ya ugonjwa,
Nijuzeni aina za tiba na mazoezi yanayohitajika ili nipone haraka,
Nawasilisha kwenu ma Dr wa humu jf.
 
jinsia yako? umri?
unafanya kazi gani?
umewahi kupata ajali?

mara nyingi matatizo ya mgongo kuuma hutokana ma imbalance ya forces zinazosababisha joints za mgongo ziwe stable.

forces hizo huunganishwa kutoka sehemu za misuli, mifupa nk.
hizo husababisha mwili uweze kubalance uzito in relation to the joint.

ikitokea shida sehemu mojawapo basi uzito wa mwili huelemea upande mmoja na kusababisha mtu awe anapata maumivu makali kwa ule upande ulioelemewa.

matibabu yake ni mazoezi maalumu na dawa za kupunguza maumivu.
hakuna matibabu ya kuondoa tatizo kwani limeanza muda mrefu na imbalance imeshatokea.
tiba inayotolewa ni kumfanya mtu aishi comfortable life!!
 
jinsia yako? umri?
unafanya kazi gani?
umewahi kupata ajali?

Ya kiume,
Umri miaka 32,
Uzito kg 67
Nafanya Kazi ya kuuza duka na kupanga mizigo ya wateja kwenye box, kufunga mabox, pia droo ya kuwekea hela ipo chini hali inayonilazimu kuinama kila mara kuhudumia Wateja.
Sikuwahi kupata ajali ya aina yoyote, lkn nishawahi kufanya mazoezi gym ya kubeba vyuma vizito sio kwa mda mrefu sana na niliacha miaka minne iliyopita.
Pia mi mvutaji sigara kiasi sio sana pia yaweza kuchangia hili tatizo langu?

Asante kwa maelezo mazuri na pia naomba kujua aina ya mazoezi yanayohitajika kufanya ili yanisaidie kupunguza hii hali ya maumivu.
Na vipi kuhusu kumpa haki yake mke wangu nayo ina madhara endapo km nitaendelea kufanya sana?
 
mara nyingi kazi za kuinama sana huwa inapelekea tatizo la kuumwa mgongo.
unajua kazi tunazozifanya na mazingira ya kufanyia kazi hayako friendly ndio maana tunapatwa na matatizo ya kiafya yatokanayo na kazi tunazofanya.
kwa wenzetu wanawake uzazi pia ni moja ya visababishi vya kupata maumivu ya mgongo.

kufanya mapenzi na mkeo hakuna shida ila kuba wakati unaweza pata maumivu ya mgongo yanayoweza kusababisha ukajikuta unashindwa kuendelea.

kuna mazoezi maalumu ya kufanya ambayo husaidia maumivu kupungua na kupata ahueni.
kuna watu maalumu wa vitengo vya mazoezi huwa wanajua mazoezi ya kumfanyia mgonjwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…