Wataalamu wa sheria za soka hebu tutoeni tongotongo kuhusiana na BUYOUT CLAUSE na RELEASE CLAUSE,maana tunachanganywa mno

George Job kapost Instagram kwamba Yanga wameirudisha ile 112M kwenye account ya Feitoto hii ina maana gani? Kulazimisha punda Kunywa maji? Na huko Msimbazi Inonga nae anataka kwenda Azam hataki kusaini mkataba mpya.
Wamuache aende

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Kwa ufupi tofauti ya Release clause na buy out clause ni hii;
Release clause inawekwa wakati mnasaini mkataba, inakuwa fixed value, haitabadilika kutokana na muda ambao tayari mchezaji ameshautumikia mkataba au value ya mchezaji kuongezeka au kupungua, release clause itabaki vile vile kama kwenye mkataba, mchezaji muda wowote akiamua kuondoka au timu ikimuhitaji inaweza vunja mkataba kwa kutoa pesa sawa na release clause kwenye mkataba.

- Buy out clause- hii si kuvunja mkataba bali unaununua mkataba wote uliyobakia, mfano mchezaji amesaini mkataba wa miaka 5, ametumikia mkataba kwa mwaka mmoja, una uwezo wa kununua mkataba uliobaki kwa kulipa kiasi chote ambacho alitakiwa kulipwa miaka minne. Hii ni njia ya gharama zaidi hivyo ndio maana timu kujilinda wanaweka release clause kubwa sana ili walazimishe mchezaji akitaka kuondoka ndani ya muda wa mkataba wake, timu pinzani ifanye mazungumzo ya kununua mkataba na sio kutumia “Release clause “.

- Inshu ya Fei Toto, kwa maandishi mbalimbali kwenye mitandoa, Yanga waliweka Release clause ya Fei Toto 100m plus mishahara ya miezi 3, kama Fei Toto amelipa pesa yote ya Release clause hakuna suala la makubaliano mengine hapo ya buy out clause, huo mkataba umeshavunwa na Fei Toto ni mchezaji huru kujiunga na timu yoyote kama atakavyotaka, Yanga wawaambie mashabiki wao ukweli, wasilete siasa kwenye vitu vilivyo wazi.
 
Ahsante,ila naomba kujua kilichofanywa na Faysal si ndio inaitwa BUYOUT CLAUSE????maana kanunua mkataba,kinachochanganya wanasema licha ya hivyo bado inawapasa Azam wawafuate Yanga ili kukubaliana bei ya mchezaji wamnunue hapa ndio sielewi,
sasa nasikia yanga wamerudisha pesa ambayo fei amewapa
 
Hahahaaa kwa hiyo tusimwani kabisa. Yaani ni empty kabisa
Ogopa matapeli hakuna wakili hapo,hao wote walishindwa na morrison tu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Reactions: K11
Hapana, kilichofanywa na Fei Toto ni release clause sio buy out clause, release clause amount yake ipo fixed tayari kwenye mkataba ila buy out clause ndio kuna negotiations. Ni sawa kilochofanywa kwa Halaand kuchukuliwa na Man City kwa ku trigger release clause yake tu toka Dortmund.
- Viongozi wa Yanga wanachofanya saivi ni upotoshaji tu ili walinde sura zao mbele ya mashabiki ila hakuna makubaliono yoyote ambayo Azam atahitaji kutoka kwa Yanga kwa sasa.
 
George Job kapost Instagram kwamba Yanga wameirudisha ile 112M kwenye account ya Feitoto hii ina maana gani? Kulazimisha punda Kunywa maji? Na huko Msimbazi Inonga nae anataka kwenda Azam hataki kusaini mkataba mpya.
Inonga akienda Azam atatusaidia sana wanasimba siku hizi ana maboko mengi
 
Ndio tunaomba msaada kuhusu hilo,yaani ukinunua mkataba (BUYOUT) Ina maana gani?unakuwa huru au bado unakuwa mali ya klabu na unapaswa kuuzwa?
Ukinunua mkataba una kuwa huru...! Hauendeshwi wala kufungwa na mkataba wa awali maana haupo tena...

Na mna weza kuingia mkataba mpya na hao ulio nunua mkataba wao...

Hivyo Yanga wakimtaka ana weza tangaza dau la Bilions au akasema kama walivyo sema manara kuwa sina thamani hiyo.. thamani yangi ni kubwa kuliko kawaida...
 
George Job kapost Instagram kwamba Yanga wameirudisha ile 112M kwenye account ya Feitoto hii ina maana gani? Kulazimisha punda Kunywa maji? Na huko Msimbazi Inonga nae anataka kwenda Azam hataki kusaini mkataba mpya.
Kurudisha haisaidii... hata kwa morrison walifanya hivyo...!
 
Huyu alikuwepo kipindi kile akagalagazwa na Morrison,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hana cha usomi wala nini
Ni msomi huyo, ukishakuwa Wakili tayari ni Msomi, haijalishi umeshinda kesi au hujashinda.
 
Wachezaji hawanunui mikataba kwa staili hiyo wadau, tujipe muda na uelewa wa mambo yanavyokwenda.
UNAPOTAKA KUNUNUA MCHEZAJI, TIMU HUSIKA NDIO HUTOA BEI HUSIKA YA MCHEZAJI HUYO NA SIO MCHEZAJI MWENYEWE.

FIESAL kama amenunua mkataba, aliapaswa kulipa thamani ya mkataba mzima, Signing fee, salary, allowances nk. Huo ndio utaratibu kuununua mkataba wake.

Kama amevunja mkataba, basi sheria za FIFA ziko open lazima kuwe na sababu kuu 3.
1. Kutolipwa msharawa kwa miezi 3
2. Kutocheza angalau game 10 kwa msimu (kulinda kipaji chako)
3. Kutotelelezwa kwa makubaliano ya kimkataba.

Tofauti na hapo YANGA wanapaswa kumpa thamani yake halisi ili timu au yy mwenyewe ajilipie asepe.

Maoni yangu, kwa hili naona wazi, Bench likimuhusu FEISAL na automatically mtu kama AZIZ KI atachukuliwa kwa uzito wa juu sana.
 
Huyu alikuwepo kipindi kile akagalagazwa na Morrison,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hana cha usomi wala nini
Huyu wakili kipindi kile alipewa kazi ya kuiwakilisha yanga lakini kosa lilishafanyika kwa yanga yeye Kama wakili ilikuwa kazi yake ni kutetea yanga. Kwa hili la fei kaeleza vizuri kabisa kuwa faeisal anaweza kununua mkataba wake. Hivi kweli yanga unamlipa Aziz k n Morison million za kutosha ala Feisal unamlipa 4ml
 
Sasa Azam wamfuate Yanga ya kazi gani wakati Feisal sio mchezaji wa Yanga tena? Ni mchezaji huru baada ya kununua mkataba
 
Pia trip na trap
 
Maelezo yako yanelekea kueleweka lakini unaposema viongozi wa Yanga wanapotosha je ni kiongozi gani umeona kapotosha? Au umeamua kutupa lawama tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…