Wataalamu wa sheria za soka hebu tutoeni tongotongo kuhusiana na BUYOUT CLAUSE na RELEASE CLAUSE,maana tunachanganywa mno

Kuna mwandishi mmoja ameelezea suala la saga la Faisal hivi.....

Feisal Salum kama katekeleza kipengele cha kununua mkataba wake hilo halina shaka linawezekana duniani kote, lakini inasalia Azam ...

Rejea sakata la Neymar Jr, ktk mkataba wake Barca waliweka kipengele cha yeye kununua mkataba wake na Yanga nao waliweka hicho kipengele cha Fei kununua mkataba....pindi akiununua tu anakua mchezaji huru.
 
Maelezo yako yanelekea kueleweka lakini unaposema viongozi wa Yanga wanapotosha je ni kiongozi gani umeona kapotosha? Au umeamua kutupa lawama tu?
Tamko la Yanga na post ya Simon Mwanasheria wa Yanga linapotosha kuwa kilichofanyika sio sahihi, ni kama watu walio katika denial hawajui nini cha kufanya juu ya sakata hili wakitegemea wanaweza kupindua meza kihuni kwa kumshawishi Fei toto pesa sawa na ya Azam ili abaki Yanga, very unprofessional.
 
Huyu alikuwepo kipindi kile akagalagazwa na Morrison,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hana cha usomi wala nini
kwa ujanja ujanja wao sidhani kama wanamikataba standard kiasi hicho
 
Hiyo 100M na mshahara wa miezi 3 Yanga ndio walioweka mkuu, Feisal yeye katimiza tu matakwa
Barua yake umeisoma?? Amesema Kuterminate mkataba wake, sheria na vifungu vilivyopo kwenye kuuvunja mkataba ni tofauti na vifungu vya kuununua mkataba huo.
 
Tamko linapotoposha nini? Weka mkataba wa Fei hapa tuusome.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…