Wanafunzi 1332 kati ya 3853 waliofanya mitihani ya Bodi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu nchini (NBAA) watarudia mitihani hiyo baada ya kufanya VIBAYA mitihani hiyo iliyofanyika Novemba mwaka huu.
Watahiniwa 703 sawa na 18.2% ndio waliofaulu, watahiniwa 1818 sawa na 47% hawakufaulu.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, Pius Maneno alisema watahiniwa 188 wamefaulu mtihani wa shahada ya juu ya Uhasibu nchini CPA, idadi hiyo inafanya watahiwa waliofaulu mitihani ya CPA mpaka sasa kufikia 4323 tangu kuanzishwa kwa mitihani hiyo mwaka 1975.
Source by Mwananchi.
[FONT=century
gothic]Duh! Yaani katika miaka 37 tangu kuanzishwa mitihani ya
CPA waliofaulu mitihani ya CPA ni 4323 tu! au sawa na wanafunzi 116.84
kwa mwaka!!! Idadi ndogo sana hasa ukitilia maanani upungufu mkubwa wa
wahasibu ambao unaikabili nchi.[/FONT]
Ni ukiritimba tu ndio unaisumbua nbaa, wenzao wa sheria wameshabadilika...
Duh! Yaani katika miaka 37 tangu kuanzishwa mitihani ya CPA waliofaulu mitihani ya CPA ni 4323 tu! au sawa na wanafunzi 116.84 kwa mwaka!!! Idadi ndogo sana hasa ukitilia maanani upungufu mkubwa wa wahasibu ambao unaikabili nchi.
Duh! Yaani katika miaka 37 tangu kuanzishwa mitihani ya CPA waliofaulu mitihani ya CPA ni 4323 tu! au sawa na wanafunzi 116.84 kwa mwaka!!! Idadi ndogo sana hasa ukitilia maanani upungufu mkubwa wa wahasibu ambao unaikabili nchi.
..., mkuu tusisahau na wahimu wa CPA waliofariki tangia wakati huo!
Wanafunzi 1332 kati ya 3853 waliofanya mitihani ya Bodi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu nchini (NBAA) watarudia mitihani hiyo baada ya kufanya VIBAYA mitihani hiyo iliyofanyika Novemba mwaka huu.
Watahiniwa 703 sawa na 18.2% ndio waliofaulu, watahiniwa 1818 sawa na 47% hawakufaulu.
Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, Pius Maneno alisema watahiniwa 188 wamefaulu mtihani wa shahada ya juu ya Uhasibu nchini CPA, idadi hiyo inafanya watahiwa waliofaulu mitihani ya CPA mpaka sasa kufikia 4323 tangu kuanzishwa kwa mitihani hiyo mwaka 1975.
Source by Mwananchi.
kama kweli hizi takwimu zina ukweli ndani yake, itabidi hadi huku kwetu kwenye elimu nako kuwe kuna board ya kuwatungia waalimu mitihani ili angalau tuondoe hawa abrubakacha kwenye elimu.
upungufu upi unaouzungumzia mkuu? Mbona kuna lundo la wahasibu mtaani?