Watakaogeuka Kuwa Maadui Wakubwa wa Mbowe na CHADEMA, ni Wanachama na Wapenzi wa CHADEMA wa Sasa

Watakaogeuka Kuwa Maadui Wakubwa wa Mbowe na CHADEMA, ni Wanachama na Wapenzi wa CHADEMA wa Sasa

swali: wakati mbowe anabadilisha katiba na kuondoa ukomo wa uongozi (nafikiri ilikuwa ni mlimani city) tundu lisu & co. walikuwa wapi kupinga? why now? matter of fact waliohoji mbowe kujiwekea uongozi wa kudumu walishambuliwa vikali na wanaomshambulia mbowe leo hii, swali langu la msingi ni hilo kwa nini tundu lisu hakupinga kwa nguvu zote kuondolewa kwa ukomo wa uongozi chadema? alishiriki kwenye zoezi na alisapoti sasa tatizo la mbowe kugombea liko wapi kama anaona bado ana uwezo? katiba inamruhusu, shida iko wapi ?
Aliyesimamia mabadiliko hayo ili kujiongezea muda, ni Mbowe mwenyewe.

Jiulize, leo hii kwa kuzingatia machawa waliopo, Samia akitaka kubadilisha katiba ili kujiongezea muda, kuna mtu ndani ya CCM ataweza kulizuia hilo? Unatarajia wanufaika wote wanaomzunguka, kuna watakaosa kumwunga mkono dhidi ya, pengine mtu mmoja tu anayekataa?
 
Hakuna aliyetarajia kuwa Mbowe angekosa hekima katika kufikia maamuzi ya ama kugombea au kupumzika, mpaka iliposhuhudiwa leo.

1. Kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, Lisu alistahili kushindani katika nafasi anayogombea, lakini mpinzani huyo hakustahili kuwa MBOWE.

2. Mbowe, kiuhalisia, hata kuwepo kwenye nafasi hiyo kwa miaka 21, tayari ame-over stay. Angekuwa na hekima asingeendelea kuing'ang'ania nafasi hiyo tena.

3. Wanachama na wapenzi wengi wa CHADEMA, wataanza kumwona Mbowe kuwa ni adui mkubwa wa demokrasia, mbinafsi anayeamini kuwa hakuna mtu mwenye uwezo kama wa kwake au kumzidi yeye.

4. Kung'ang'ania kwake madaraka kunapeleka ujumbe muhimu kwa wananchi kwamba Mbowe alipokuwa anasema kuwa uongozi kwenye vyama vya upinzani ni mateso, labda anaongelea watu wengine, lakini kwake binafsi, uongozi huo unamnufaisha na kumfaidisha. Kiuhalisia ni kwamba huwezi kung'ang'ania mateso. Tena akitokea mwingine kuwa tayari kuyabeba hayo mateso, utashukuru sana.

5. Mvurugano na mpasuko alioutengeneza Mbowe ndani ya CHADEMA, unaimaliza CHADEMA, hivyo wanachama wa CHADEMA ambao waliitaka CHADEMA iwe na nguvu zaidi ili kupambana na CCM, watamchukia Mbowe kwa kiwango ambacho hakukitarajia. Mbowe atageuka kuwa adui mkubwa wa wanachama wa CHADEMA, naye atakuwa rafiki mkubwa wa CCM, japo kwa siri, kwa maana ameweza kusaidia kufanikisha malengo ya CCM ya kuua upinzani. Lakini asichokijua ni kuwa baada ya kuisaidia CCM kuiua CHADEMA, CCM hawatakuwa na muda naye kwa sababu CHADEMA haitakuwa threat wala kuwa competitor. CCM itaelekeza nguvu zake kwa kiongozi atakayekuwa akiongoza chama cha upinzani chenye nguvu, inaweza kuwa ni CHAUMA au ACT, kama Lisu atahamia kwenye chama kimojawapo. Itakapofikia hatua hiyo, Mbowe atapozwa na cheo cha Parole, kama ilivyokuwa kwa marehemu Mrema.
Siasa ni sayansi! Mbowe amechelewa kuchukua fomu, akisubiri kujitokeza mtu makini.
 
Mbowe, kiuhalisia, hata kuwepo kwenye nafasi hiyo kwa miaka 21, tayari ame-over stay. Angekuwa na hekima asingeendelea kuing'ang'ania nafasi hiyo tena.

.
Leo Mbowe kathibitisha pasipo na shaka kwamba yeye ni pandikizi na afisa mtiifu wa watu flani. Same caliber na akina Momose Cheyo, Lipumba na Lyatonga Mrema

Ewe mwana CHADEMA, shtuka na usikubali tena kupigwa bomu au kuvunjwa mguu kukitetea Chama ambacho kiongozi mkuu alishakuwa signed na mfumo toka zamani
 
Mbowe na hao wahuni wenzake wana project na CCM. Mbowe ni mhuni na ukimzingatia unapoteza muda wako bure. Sasa angalia na wanaomshabikia ndipo utachoka kabisa
Jambazi la kisiasa
 
Aliyesimamia mabadiliko hayo ili kujiongezea muda, ni Mbowe mwenyewe.

Jiulize, leo hii kwa kuzingatia machawa waliopo, Samia akitaka kubadilisha katiba ili kujiongezea muda, kuna mtu ndani ya CCM ataweza kulizuia hilo? Unatarajia wanufaika wote wanaomzunguka, kuna watakosa kumwunga mkono dhidi oengine ya mtu mmoja tu anayekataa?

nilitegemea nguvu inayotumika leo hii kupinga mbowe kugombea (tena) ingetumika kupinga kuondoa ukomo wa uongozi, tena tundu lisu angeongoza lkn kipindi kile alisapoti na walitafuta explaination kujustify mbowe kuiondolea ukomo wa uongozi, sasa leo hii ameamua kugombea hakuna kifungu cha katiba alichovunja.

domokrasia ni ngumu sana kuiishi …
 
Leo Mbowe kathibitisha pasipo na shaka kwamba yeye ni pandikizi na afisa mtiifu wa watu flani. Same caliber na akina Momose Cheyo, Lipumba na Lyatonga Mrema

Ewe mwana CHADEMA, shtuka na usikubali tena kupigwa bomu au kuvunjwa mguu kukitetea Chama ambacho kiongozi mkuu alishakuwa signed na mfumo toka zamani
Yaani siwezi hata kujigusa eti nisapototi chadema
 
Tatizo la box la kura ni kilicho nyuma ya Mbowe. Angekuwa anapambana na Mbowe per se isingekuwa shida na CHADEMA ingebaki moja regardless ya nani atashinda. Mbowe anasaidiwa na Samia, Samia mwenye polisi na TISS na fedha. CHADEMA itakuwa salama iwapo tu Lissu atashinda. Vinginevyo Mbowe akiweza kutumia ghilba alizopanga na akashinda, basi nina uhakika Chadema itakufa. Itakufa kwa sababu itakuwa chama ''chawa'' wa CCM, na hata wakipewa wabunge wa bure bado wananchi hawatai-support.
Binafsi nilimpenda sana sana Lissu hadi nilipoona si mtu wa kudhibiti hisia na shari. Msigwa anampotosha vibaya sana Lissu. Lissu anaivaa shari ya Msigwa bila tahadhari. Mkuu wewe ni miongoni mwa wanaJF ninaowaheshimu sana humu jukwaani, naamini una upeo wa kuchambua vitu bila ushabiki, tuweke akiba ya subira tutakuja kukumbushana hapa siku moja.
 
Hakuna aliyetarajia kuwa Mbowe angekosa hekima katika kufikia maamuzi ya ama kugombea au kupumzika, mpaka iliposhuhudiwa leo.

1. Kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, Lisu alistahili kushindani katika nafasi anayogombea, lakini mpinzani huyo hakustahili kuwa MBOWE.

2. Mbowe, kiuhalisia, hata kuwepo kwenye nafasi hiyo kwa miaka 21, tayari ame-over stay. Angekuwa na hekima asingeendelea kuing'ang'ania nafasi hiyo tena.

3. Wanachama na wapenzi wengi wa CHADEMA, wataanza kumwona Mbowe kuwa ni adui mkubwa wa demokrasia, mbinafsi anayeamini kuwa hakuna mtu mwenye uwezo kama wa kwake au kumzidi yeye.

4. Kung'ang'ania kwake madaraka kunapeleka ujumbe muhimu kwa wananchi kwamba Mbowe alipokuwa anasema kuwa uongozi kwenye vyama vya upinzani ni mateso, labda anaongelea watu wengine, lakini kwake binafsi, uongozi huo unamnufaisha na kumfaidisha. Kiuhalisia ni kwamba huwezi kung'ang'ania mateso. Tena akitokea mwingine kuwa tayari kuyabeba hayo mateso, utashukuru sana.

5. Mvurugano na mpasuko alioutengeneza Mbowe ndani ya CHADEMA, unaimaliza CHADEMA, hivyo wanachama wa CHADEMA ambao waliitaka CHADEMA iwe na nguvu zaidi ili kupambana na CCM, watamchukia Mbowe kwa kiwango ambacho hakukitarajia. Mbowe atageuka kuwa adui mkubwa wa wanachama wa CHADEMA, naye atakuwa rafiki mkubwa wa CCM, japo kwa siri, kwa maana ameweza kusaidia kufanikisha malengo ya CCM ya kuua upinzani. Lakini asichokijua ni kuwa baada ya kuisaidia CCM kuiua CHADEMA, CCM hawatakuwa na muda naye kwa sababu CHADEMA haitakuwa threat wala kuwa competitor. CCM itaelekeza nguvu zake kwa kiongozi atakayekuwa akiongoza chama cha upinzani chenye nguvu, inaweza kuwa ni CHAUMA au ACT, kama Lisu atahamia kwenye chama kimojawapo. Itakapofikia hatua hiyo, Mbowe atapozwa na cheo cha Parole, kama ilivyokuwa kwa marehemu Mrema.
Hadi sasa quarter of life ya Mbowe kukiongoza chama kwa misingi yake kilivyokuwa is over.

Mpaka sasa jamii kubwa ya wana CHADEMA washasanuka kuwa FAM yupo hapo kwa manufaa yake wala si kwa wananchi.

Ikumbukwe hata maandamano aliyokua anaitisha lengo na madhumuni ilikua ni kujinadi yeye na malipo yake kashapata ndio maana LISU amesanuka.
 
Kiukweli Kiongozi Bams,HOJA zako huwa nazielewa sana..endelea kuelimisha maelfu ya Watanzania waliopo kwenye platform hii

Nirudi kwa Mh Mbowe...umechelewa kusoma ALAMA za nyakati na pia hukujua NGUVU na MIKAKATI ya ndugu Lissu..mwenzio amewekeza kwenye grassroot pia hoja zake zinaeleweka kirahisi..kiufupi hajawahi KUYUMBA
 
Hahaha nyie watu gani mnaopigia kelele haki na demokrasia, huko ccm na serikali yake, ikifika kwenu hamuitaki tena.
 
2 Billions za mwezi Nov Double Agent kazipeleka wapi ?
Mwenzie kaenda kuupumzisha moyo.
 
Kwa CHADEMA Hii wakuu ni heri CCM itutawale Milele, CCM chondechonde msituache watanzania wenyewe!
 
Kiukweli Kiongozi Bams,HOJA zako huwa nazielewa sana..endelea kuelimisha maelfu ya Watanzania waliopo kwenye platform hii

Nirudi kwa Mh Mbowe...umechelewa kusoma ALAMA za nyakati na pia hukujua NGUVU na MIKAKATI ya ndugu Lissu..mwenzio amewekeza kwenye grassroot pia hoja zake zinaeleweka kirahisi..kiufupi hajawahi KUYUMBA
Mtemi Mbojo, hata kama Lisu amewekeza kwenye grassroot, sina uhakika kama hao viongozi wa kwenye grassroot ni wapiga kura kwenye kumchagua mwenyekiti. Kama wanashiriki kwenye uchaguzi, na Lisu akashinda, hiyo ndiyo itakuwa pona pekee ya CHADEMA.
 
Mtemi Mbojo, hata kama Lisu amewekeza kwenye grassroot, sina uhakika kama hao viongozi wa kwenye grassroot ni wapiga kura kwenye kumchagua mwenyekiti. Kama wanashiriki kwenye uchaguzi, na Lisu akashinda, hiyo ndiyo itakuwa pona pekee ya CHADEMA.
Nakubaliana na wewe kiongozi, hakika ni MTEGO, ni hao wajumbe 1000+ wa mkutano mkuu waende na Mbowe wakiue chama or
 
Back
Top Bottom