Yaani kwa jinsi ilivyo hakuna cha kuhamasishana wala nini lejea yaliotokea kule kwenye kanda yaliotokea mpaka msigwa akahamia ccm ndicho kinakweda kutokea kwenye uchaguzi wa taifaHamasisheni mkapige kura ili mkikomboe chama chenu kupitia Lissu acheni kulia lia...hamuwezi kulazimisha watu wasigombee mkaita ndo demokrasia.... huyo kidume wenu Lissu mwambieni akapambane kwenye boksi la kura!!
Maccm yanahaha sana kumsaidia kibaraka wao Mbowe.Huyo mshenzi Lisu atapata kura kiduchu.
Hafai kabisa...dah balaa
Aende zake Ubelgiji akajifie huko
Awamu hii kayatimba, wote tumezijua rangi zake halisiZZK alipotaka kumchalenge Mbowe tulimuona ZZK mpumbavu msaliti na Mbowe tukamuimbia mwamba tuvushe.
EL alipokatwa CCM akaja CDM tukamsaliti Dr Slaa nakumuona Mbowe ana akili sana na Dr Slaa tukamuona mpumbavu, Mzee wa watu njaa ikampiga ikabidi ageuke jiwe anusuru njaa yake, huku tukimtukana na kumuita msaliti.
Huko nyuma Kila aliyemhoji Mbowe, au kuhoji mambo ya Mbowe tulimshambulia na kumuona mjinga, juzi mchungaji Msigwa pia tukamuona mpumbavu.
Sasa Leo tutaanzaje kuwaaminisha watu juu ya huu unafiki na ukondoo wetu zaidi ya wote kuonekana matapeli na wale tuliowatusi wanaweza kuwa na akili kuliko sisi wote kwa kusoma alama za nyakati mapema sana.
Wakati la sakata la ZZK, alishaonya juu ya CDM kuwa option B ya EL akikatwa CCM tena ilikuwa zaidi ya miaka mitatu nyuma ya tukio la EL kukatwa lakini tulimpuuza ZZK na kumuita majina yoote likiwemo la usaliti.
Nani ni MSALITI SASA, ZZK, DR SLAA, Mch MSIGWA, MBOWE, LISSU AU WAFUASI WA CDM walioshabikia sarakasi za Mbowe?
Bahati Mbaya Mbowe task yake ni nyingine na mabosi wake ni wengine na KPI zake zinapimwa kwingine kabisa na mrithi wake hawezi kuwa Lissu, Mbowe ni genius aliyeweza kurubuni umati wa watu Kwa manufaa ya mabosi zake.
Mbowe anadhihirisha alivyo mchovu,si mvumilivu na hapendi Demokrasia ndio amekaa kwenye uenyekiti katika mazingira ya usanii sanii tu hana kitu na sasa amedhihirisha wazi kuwa hana kitu ni mpuuzi mmoja tu.Hakuna aliyetarajia kuwa Mbowe angekosa hekima katika kufikia maamuzi ya ama kugombea au kupumzika, mpaka iliposhuhudiwa leo.
1. Kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, Lisu alistahili kushindani katika nafasi anayogombea, lakini mpinzani huyo hakustahili kuwa MBOWE.
2. Mbowe, kiuhalisia, hata kuwepo kwenye nafasi hiyo kwa miaka 21, tayari ame-over stay. Angekuwa na hekima asingeendelea kuing'ang'ania nafasi hiyo tena.
3. Wanachama na wapenzi wengi wa CHADEMA, wataanza kumwona Mbowe kuwa ni adui mkubwa wa demokrasia, mbinafsi anayeamini kuwa hakuna mtu mwenye uwezo kama wa kwake au kumzidi yeye.
4. Kung'ang'ania kwake madaraka kunapeleka ujumbe muhimu kwa wananchi kwamba Mbowe alipokuwa anasema kuwa uongozi kwenye vyama vya upinzani ni mateso, labda anaongelea watu wengine, lakini kwake binafsi, uongozi huo unamnufaisha na kumfaidisha. Kiuhalisia ni kwamba huwezi kung'ang'ania mateso. Tena akitokea mwingine kuwa tayari kuyabeba hayo mateso, utashukuru sana.
5. Mvurugano na mpasuko alioutengeneza Mbowe ndani ya CHADEMA, unaimaliza CHADEMA, hivyo wanachama wa CHADEMA ambao waliitaka CHADEMA iwe na nguvu zaidi ili kupambana na CCM, watamchukia Mbowe kwa kiwango ambacho hakukitarajia. Mbowe atageuka kuwa adui mkubwa wa wanachama wa CHADEMA, naye atakuwa rafiki mkubwa wa CCM, japo kwa siri, kwa maana ameweza kusaidia kufanikisha malengo ya CCM ya kuua upinzani. Lakini asichokijua ni kuwa baada ya kuisaidia CCM kuiua CHADEMA, CCM hawatakuwa na muda naye kwa sababu CHADEMA haitakuwa threat wala kuwa competitor. CCM itaelekeza nguvu zake kwa kiongozi atakayekuwa akiongoza chama cha upinzani chenye nguvu, inaweza kuwa ni CHAUMA au ACT, kama Lisu atahamia kwenye chama kimojawapo. Itakapofikia hatua hiyo, Mbowe atapozwa na cheo cha Parole, kama ilivyokuwa kwa marehemu Mrema.