Wataliban wamewawaaibisha Wamarekani

Wataliban wamewawaaibisha Wamarekani

Marekani na washirika wake pamoja na kutumia takribani dola bilioni 89 ($89 billions) kwa kuvifundisha na kuvipa silaha vikosi vya jeshi la Afghanistan kwa takribani miaka 20 hivi, iliwachukua mwezi mmoja tuu kwa Taliban kuvi fyekelea mbali na kuvisambaratisha vikosi vya jeshi la Afghanistan baada ya ‘washirika wao’ kutangaza kuviondoa vikosi vyao nchini Afghanistan.

‘‘Allahu Akbar’ wapiganaji wetu wamefanikiwa kuichukua ikulu huku serikali dhalimu ikianguka, kibaraka mkuu ( raisi Ashraf Ghani ) na vikosi vyake wamekimbia na sasa vita imekwisha.!

’ haya maneno ya msemaji wa Wa -Taleban Suhail Shaheen na kuwaasa wakazi wa Kabul hawana haja ya kuwa na wasiwasi na kwamba mali na maisha yao ni salama. "Sisi ni watumishi wa watu na wa nchi hii,"

Taliban imetangaza ushindi nchini Afghanistan baada ya kuteka mji mkuu Kabul, na kutamatisha karibu miaka 20 uwepo wa Marekani na washirika wake nchini humo

Kutokea Kandahar ( kusini mwa nchi) adi Mazar-i-Sharif ( kaskazini), Herat ( Magharibi) mpaka Jalalabad ( mashariki) huku Kabul ukiwa mji mkuu wa mwisho nchini Afghanistan kudhibitiwa na Taliban, baada ya wapiganaji wake kuikamata miji zaidi ya miji kumi kwa muda wa siku kumi tuu. Aliye kuwa raisi, Ashraf Ghani, alitimua mbio na kukimbilia Tashkent katika nchi jirani ya Uzbekistan

Kikubwa zaidi kwa takriban masaa 36 tangu wa Taleban wauteke mji wa Kabul, hakuna raia au mwananjeshi yeyote aliye uwawa au kuchinjwa tofauti kabisa na ilivyo kuwa ikielezwa apo kabla na Marekani na washirika wake kuwa watu wengi watauwaa na kuchinjwa pindi Wa Taleban watakapo ingia Kabul....

Kongole kwa Wa Taleban kwa kuweza kuidhibiti tena nchi walionyang'anywa na wavamizi takribani miaka 20 iliyo pita,
Jeshi la serikali wanajeshi hawakuwa na nua ya kupigana kabisa,na pakistani rafiki mkubwa wa matalebani aliingiza wajashi 30,000 kupambana na askari waliopoteza ari ya kupigana

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Vita ya Libya ilianzishwa kwa lobbying ya Wafaransa unapaswa kuelewa hilo.Read

Hata ingekua ni NATO, na hapo ndio ilikua point yangu, hawa jamaa hawaendi sehem isipokua kuna maslahi binafsi.
 
Hata ingekua ni NATO, na hapo ndio ilikua point yangu, hawa jamaa hawaendi sehem isipokua kuna maslahi binafsi.
Hakuna vita isiyokuwa na maslahi duniani-hata Tanzania kuivamia Uganda kulikuwa na maslahi ndani yake 🤣 🤣
 
aiseeee watalebani ni wanaume wa shoka! si mchezo . watu wanashinda milimani marekani mwenyewe kasanda
 
kuna la kujifunza apo, na hasa kuto kukata tamaaa maishani!
 
Hakuna vita isiyokuwa na maslahi duniani-hata Tanzania kuivamia Uganda kulikuwa na maslahi ndani yake 🤣 🤣
Halafu wabongo wengi hawajui tofauti kati ya Al-qaeda na Taliban. Haya ni makundi mawili tofauti kabisa.
 
Kwa nini Taleban wameweza kurudi madarakani baada ya Marekani kuondoa vikosi vyao? Kwa nini Taleban hawakuthubutu kurudi katika miaka yote 20 wakati Marekani ameweka vikosi vyake Afghanstan?
Mmarekani alikuwa anajua mambo yatakavyokuwa baada ya kuondoka. Ni mambo yaliyopangwa na hata waziri mkuu wa Uingereza amesisitiza jambo la muhimu ni Taliban kutoruhusu vikundi vya kigaidi kama Al-qaeda kuweka makao yao huko. NB: kuna watu wengi wandani Al-qaeda ni Taliban.
 
tatizo apo watu walisha 'panikishwa' na waka 'panic' na wengine wanaenda kutafuta 'fursa' ……….
Hayo ni mawazo mgando,kwa hiyo wewe ili umkimbie chui unahitaji kupanikishwa kwanza?
 
wa taleban ni makamanda kweli kweli, ndani ya mwei mmoja tuu wamei kamata nnchi
 
Marekani ni Taifa la kipuuzi sana. Wanapenda kutengeneza matatizo kwenye nchi nyingine, halafu baadae wanakimbia na kuwaacha wenyeji kwenye mataa.
 
Marekani ni Taifa la kipuuzi sana. Wanapenda kutengeneza matatizo kwenye nchi nyingine, halafu baadae wanakimbia na kuwaacha wenyeji kwenye mataa.

Marekani huratibu na kufadhili vikundi hivyo kwa kusudi maalumu.
 
Watalebani wanaabisha wananchi wao wenyewe,sasa hivi wameshaanza kuwaambia waanawake wasirudi makazini tena,halafu kibaya zaidi wameanza kuvamia familia mbalimbali na kilazimisha wapewe mabinti wawe kama wasaidizi wao,hao ni washenzi tu ndio maana wananchi wanawakimbia
 
ungekuwa unazijua vizuri siasa za beberu mkuu ungekaa kimya..

Hivi unafahamu beberu mkuu aliondoka Afghanistan bila kumpa mtu yeyote taarifa hata serikali haikujua kama anaondoka..? Jiulize kwanini?..
Huyu beberu mkuu hata neti unayojifunikia kakupa kama sio wewe bas bibi yako anaitumia
 
hivi hawa wamarekani walikuwa wanatafuta nini Afghanistan, ni kweli kwa miaka yote 20 walikuwa wanapambana na ugaidi ?
 
Marekani na washirika wake pamoja na kutumia takribani dola bilioni 89 ($89 billions) kwa kuvifundisha na kuvipa silaha vikosi vya jeshi la Afghanistan kwa takribani miaka 20 hivi, iliwachukua mwezi mmoja tuu kwa Taliban kuvi fyekelea mbali na kuvisambaratisha vikosi vya jeshi la Afghanistan baada ya ‘washirika wao’ kutangaza kuviondoa vikosi vyao nchini Afghanistan.

‘‘Allahu Akbar’ wapiganaji wetu wamefanikiwa kuichukua ikulu huku serikali dhalimu ikianguka, kibaraka mkuu ( raisi Ashraf Ghani ) na vikosi vyake wamekimbia na sasa vita imekwisha.!

’ haya maneno ya msemaji wa Wa -Taleban Suhail Shaheen na kuwaasa wakazi wa Kabul hawana haja ya kuwa na wasiwasi na kwamba mali na maisha yao ni salama. "Sisi ni watumishi wa watu na wa nchi hii,"

Taliban imetangaza ushindi nchini Afghanistan baada ya kuteka mji mkuu Kabul, na kutamatisha karibu miaka 20 uwepo wa Marekani na washirika wake nchini humo

Kutokea Kandahar ( kusini mwa nchi) adi Mazar-i-Sharif ( kaskazini), Herat ( Magharibi) mpaka Jalalabad ( mashariki) huku Kabul ukiwa mji mkuu wa mwisho nchini Afghanistan kudhibitiwa na Taliban, baada ya wapiganaji wake kuikamata miji zaidi ya miji kumi kwa muda wa siku kumi tuu. Aliye kuwa raisi, Ashraf Ghani, alitimua mbio na kukimbilia Tashkent katika nchi jirani ya Uzbekistan

Kikubwa zaidi kwa takriban masaa 36 tangu wa Taleban wauteke mji wa Kabul, hakuna raia au mwananjeshi yeyote aliye uwawa au kuchinjwa tofauti kabisa na ilivyo kuwa ikielezwa apo kabla na Marekani na washirika wake kuwa watu wengi watauwaa na kuchinjwa pindi Wa Taleban watakapo ingia Kabul....

Kongole kwa Wa Taleban kwa kuweza kuidhibiti tena nchi walionyang'anywa na wavamizi takribani miaka 20 iliyo pita,
Wameua watu watano Airport ya Kabul jana.

Acha uzandiki.
 
SASA HIVI HAWAELEWI ILA SIKU MAGAIDI WAKIANZA KUWAGEUKA CHINA NA URUSI NDIO AKILI ZITAWAKAA WATAJUA GAIDI HANA SHUKRANI
 
Back
Top Bottom