Watangazaji wa Azam Wanapendelea Mabondia wa Jeshi wa kutoka DSM

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hii iko wazi kabisa na inaitia aibu Azam Media , Watangazaji hawapaswi kuwa na upande .

Kwa Mfano , bondia wa JW anayeitwa Emiliano Partric amefagiliwa na watangazaji wa Azam kibwege sana huku akibanwa mbavu na bondia mchanga aitwaye Osama kutoka Mtwara , kwa kifupi ni kwamba huyo dogo Osama hajapigwa ngumi yoyote ya maana , hata kama ni kweli kwamba huyo Emiliano ameshinda , lakini kiukweli Watangazaji wa Azam walitaka kuwaandaa Washabiki kwa matokeo ya Utata .

Hii ni Aibu sana !

Acheni Matokeo yatangazwe na Majaji , Watangazaji wa Azam kudhani sisi wengine hatujui boxing ni mawazo ya Kijinga sana !

Tuheshimiane .
 
Hili la watangazaji kufagili mabondia wa jeshi ni kweli kabisa, lakini kwa hili la kwamba eti hajapiga ngumi za maana naweza nikakupinga......jamaa alijijua hana pumzi ndefu kwa hyo alikuwa anapigana kwa hesabu kubwa sana, alikuwa anahakikisha ngumi 10 anazorusha 6 au 7 zinampa point, japo huyo dogo Osama ni mgumu na mvumilivu sana.....hongera sana kwake Osama japo amechapika kihalali kabisa
 
Osama ni promising fighter. Akipata training vema, ni mtu.
 
hivi kupiga guard ndio kupata point ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…