Watangazaji wengi wa Television na Radio hapa Tanzania wanagangamala sana utafikiri wanakula cement, na wanatumia sauti zisizo zao (artificial)

Emily Lazarus wa Radio One kabobea kwenye kukosea majina. Kila habari lazima akosee jina Mfano kila siku anatamka "Joe Biden" kama inavyoandikwa badala ya "Jo Baiden". Sasa sijui "Peter" atatamka kama inavyoandikwa badala ya kusema "Piter"? Huwa hafanyi utafiti wa namna ya kutamka majina yalioko kwenye habari kabla hajasoma na haangalii habari za nje.
 
Kuna kitu umesema. Ni cha maana sana. Watangazaji karibu wote wa Bongo, iwe TV iwe Radio au haya ma TV online yaliyoibuka kama mchicha... hawatumii sauti zao za asili. Kifupi huwezi kuwatofautisha.
 
Utangazaji ni kurelax siyo unatoa meno machafu mbele ya mic huku shingo ikitoa mishipa kama miguu ya mbung'o.

Mfano yule anayetangaza magazeti kwa mbwembwe huku akiongea kama anafokeana na mpwa wake.
Kitenge anatumia nguvu sana.
Na kuna wale watangazaji wa vipindi vya bongfleva sauti zao wote kutoka radio tofaut hufanana.
 
Ila jamaa ana sauti nzuri sana kwenye habari makosa madogo madogo yanamshusha.

Anaitwa Emilius Lazaro.
 
Ila jamaa ana sauti nzuri sana kwenye habari makosa madogo madogo yanamshusha.

Anaitwa Emilius Lazaro.
Ana sauti nzuri sana ila kutofuatlia taarifa za habari za nje na kujifunza namna ya kutamka majina ya watu na miji kutamfelisha.
 
Ana sauti nzuri sana ila kutofuatlia taarifa za habari za nje na kujifunza namna ya kutamka majina ya watu na miji kutamfelisha.
Alikuwa Mwl wangu nyakati fulani jamaa anajua anajitahidi kiasi chake japo makosa yake ni ya wazi.
 
Kumbe na we ushamshtukia? Mara nyingi anachemsha kwenye majina sema nimekumbuka mfano huu mmoja.
Na mtiririko wa usomaji wa habari kuna muda anaenda spidi isiyo kawaida katika usomaji.

Mtangazaji pekee ninaemhusudu ni Ahmed Ally wa Azam Media jamaa anajua sana kufanya kazi pia anajua kutangaza kwa mtiririko mzuri.
 
Sasa mkuu unataka nitangazee na kiswahili changu kile cha chattle kweli kabsa. 'Hiiiiiii heno nene bhanghosha...'

Sent using myLG leon
 
Lini ulimtembelea Christine Amanpour nyumbani?
 
Unamsema kitenge au samsa sali?

Sent using myLG leon
Huyo huyo Kitenge. Kaona usomaji wa magazeti lazima ufoke na kelele za kujirudiarudia kama anaongea na viziwi.

Zembwela akiwa EA Radio alikuwa anafanya kazi kwa utulivu sana hata David Rwenyagira ila combination yao na Kitenge watakuja kutoka studio taya zimetanuka.
 
Kuna uyu wa redio one Simon Kabendera ni kituko kwa kweli

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…