Watanzania 24 wanashikiliwa na Mamlaka ya Uhamiaji Marekani

Watanzania 24 wanashikiliwa na Mamlaka ya Uhamiaji Marekani

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani umesema Serikali ina taarifa rasmi ya watu 24 wanaoaminika kuwa Watanzania wanaoshikiliwa na Mamlaka ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) kwa kuishi nchini humo kinyume cha sheria.

1738919481512.png
“ICE imetuarifu kwamba, watu wanne kati ya hao wameshakamilisha taratibu zote za kimahakama za kuondoshwa nchini Marekani, hivyo watarejeshwa Tanzania muda wowote kuanzia sasa. Watu 20 waliobaki wapo kwenye hatua mbalimbali za kesi zao za uhamiaji huko Marekani,” umeeleza ubalozi huo.

Ubalozi huo umesema hayo katika majibu ya maswali yaliyoulizwa na Mwananchi hivi karibuni kuhusu Watanzania waishio Marekani kinyume cha sheria.

Pia soma Hadi kufikia Novemba 24, 2024, Idadi ya watu waliopaswa kuondoka Marekani ni 1,445,549, wamo watanzania 301

Mwananchi
 
Wakichelewa tu Guantanamo inawahusu au kwenye lile Gereza hatari la El Salvador ambapo Rais wa huko amejitolea Marekani iwapeleke wahamiaji awafunge huko
 
Trump anaamini kuwafukuza wageni & wazamiaji kutapunguza tatizo la ajira kwa wananchi wake, kumbe kiuhalisia wanaofukuzwa walikua wanalipwa maokoto ya chini ya kiwango cha kawaida na kutumikishwa like hell

Anyway hii baada ya mda inaweza kuwa na faida au shot

Vijana wa hovyo andaeni passport zenu mapema anytime marekani ataanza kuwaomba awape ajira
 
Ila watanzania habari mbaya tunazipenda, tupunguze chuki 😹😹
 
Trump anaamini kuwafukuza wageni & wazamiaji kutapunguza tatizo la ajira kwa wananchi wake, kumbe kiuhalisia wanaofukuzwa walikua wanalipwa maokoto ya chini ya kiwango cha kawaida na kutumikishwa like hell

Anyway hii baada ya mda inaweza kuwa na faida au shot

Vijana wa hovyo andaeni passport zenu mapema anytime marekani ataanza kuwaomba awape ajira
Usitetee ujinga acha watoke nchi za watu
 
Back
Top Bottom