Watanzania acheni unafiki, ina maana kifo cha Ivan kimewauma kuliko Dogo Mfaume?

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Watanzania kwa unafiki tu hatujambo, sishangai ndio maana hatuendelei.

Leo nimeshangaa sana baada ya kuingia kwenye mitandao ya kijamii nakuta watu wengi wakilia na kuonyesha kuumia sana na kifo cha Ivan, kwanza niseme tu mimi nilikua simjui huyo ndugu, nikataka kujua ni mtu wa wapi nikaambiwa ni mganda alikua mume wa mke wa Daimondi.

Nikauliza kama ni msanii labda wa muziki au maigizo nikaambiwa hapana ni social celebrity tu, anyway sina shida na hilo lakini kilichonishangaza ni kukuta watu kuonekana wameumia sana na kifo cha Ivan kuliko mtanzania mwenzao Dogo mfaume ambae amezikwa juzi na sikuona msanii yoyote ametupia picha ya dogo mfaume au basi kutoa pole.

Utashangaa kifo cha Ivan kimewaumiza sana watanzania kuliko mtanzania mwenzao aliefariki juzi tu hapa, na utashangaa kujua kua watanzania wameumia sana na kifo cha Ivan kuliko hata waganda.

Unafiki jambo baya sana.
 
Msiba wa tajiri unahudhuriwa na mpaka hata ambao hawakuwahi kumuona au kumjua siku za uhai wake..

Wakishapata bio fulani kafariki, yule mwenye sijui Hotel gani, sijui mwenye biashara gani alikuwaga anatembea na Vogue, VX V8 basi kila mtu atajipeleka msibani kwenda kuona ufahari na ibada na mahubiri marefuuuu.. Maskini akifa mambo yanaenda fasta fasta tu ufukiwe mambo yaishe..

Too sad aisee..
 
Huu ni upenzi wa kimitandao, Dogo Mfaume ni kutoka moyoni.
 
Hatupangiwi wa kumlilia

We endelea kumlilia huyo mfaume wako aliyekufa kwa matumizi ya ngada sisi tuache tumlilie Ivan
 
Dogo mfaume alikuwa nani? Tunajua Ivan alikuwa mume wa Zari now mke mzazi mwenzake Diamond, alikuwa anasaidia vijana wengi kuwainua kimaisha., alikuwa mtu anependa sana mitandao ya kijamii kujitangaza, saa Mfaume R.I.P wangapi walikuwa na habari zake?! Usije kushangaa siku Messi anafari pole nyingi kuliko akifariki mchezaji wa Toto, au mabao maana hata majina wengi hatuwajui, acha kulalamika kwa kila jambo.
 
Unajua maana ya neno unafiki?
 
Dogo Mfaume alikuwa na nani?
Thamani ya mtu ni vile alivyo navyo, ndiyo maana hata wewe hukuleta uzi wa masikitiko kwa huyo dogo, mwenye nacho ataongezewa. Huu ni ukweli mchungu, huna kitu huna chako, huna rafiki wa kweli wala nini!!
 
Hahahaaaa.... Jamaa kala bata ni hakuna.. Wacha akapumzike..
 
Pesa INA nguvu sana mkuu!
Hapo usitafute mchawi jombaaaa!
Hiyo yote imetokana Na nguvu ya shekeri
Umenena vyema, soma[emoji116] [emoji116] [emoji116]
Dogo Mfaume alikuwa na nani?
Thamani ya mtu ni vile alivyo navyo, ndiyo maana hata wewe hukuleta uzi wa masikitiko kwa huyo dogo, mwenye nacho ataongezewa. Huu ni ukweli mchungu, huna kitu huna chako, huna rafiki wa kweli wala nini!!
 
Bora umewaambia ukweli maan duu
 

Mi simjui huyo Dogo mfaume, ila namfaham Ivan, kosa langu lipo wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…