Watanzania hatumtendei haki Vanessa Mdee

'''Naomba unirogee''' song la kiswaz kabisa
song la kiswazi lililojaa pozi za kibeyonce......muziki unataka timing.cheki snura hit moja tu la chura sasa hivi anazunguka nchi nzima kupiga show japo ni za buku tano tano kiingilio but si haba teh teh teh
 
sasa navy kenzo hiyo kamatia chini chorus peke yake ndo ya kiswahili ila verse zote zina lugha ngeni tu nafikiri ni melody kiukweli mziki hauna lugha pia kwa V money ni suala la wakati tu maana hata kina nahreel wana nyimbo nyingi hko nyuma
 
mziki
 
Mtoa mada tambua kitu kimoja, ma promoters hawaangalii ukubwa wa msanii wanaangalia mvuto na uwezo wakujaza watu, msanii anaweza kua mkubwa ila asiwe na mvuto wakujaza watu viwanjani, kua msanii2 haitoshi kuna mambo yaziada unatakiwa kua nayo ili uvute usikivu wa watu kwako, ndio maana diamond ataendelea kua juu
 
Ule wimbo wake wa come over baby, biti nzuri sauti nzuri video nzuri lakini tatizo lugha na uvaaji. Akipunguza uzungu nadhani atakua zaidi ya alipo sasa.
 
wabongo kwa unafiki..mbona kuna wanamuziki wanapiga nyimbo za kiswazi kabisa hawana uzungu wowote na wanakula ugali maharage uswahilini kwa mama ntilie lakini hawavumi? SOMETIMES KUVUMA NI BAHATI TU YA MTU NA MASKENDO YA HOVYO HOVYO
 
Aka kademu siku hizi kamejichubua na kanapaka marangi rangi usoni kamekuwa Kama kaclown ka birthday za watoto.
 
Lugha sio tatizo nilikuwa gaborone live band walipiga nyimbo za kiswahi sina makosa watu walicheza sana na kuimba
relative wa rafiki yng alishangaa naujua huo wimbo nikamwambia ni wa Tz akasema naupenda ingawa sijui maana yake. Vanessa lugha sio tatizo ni wewe hujui soko la ndani linataka nini pia live kuimba huwezi kucheza tu beyonce anaimba live so kaza buti
 
Naunga mkono wanaosema UZUNGU UMEZIDI, Ingawa una umuhimu wake Kimataifa ..!!

Yeye ndo hatutendei haki mashabiki wa nyumban, na sio kwenye music tu, hata kwenye mahojiano ya kawaida..!!

Aweke UZUNGU kimataifa na aweke USWAHILI nyumban, ajue kuchanyanga na kutenganisha majukwaa na mashabiki, ni muhim sana kwa Wabongo ..!!
 
Kuna watu walikuwa wanamfananisha Vanessa na Jide wakati hata kuandika tu mpaka amemsikilizie Barnaba.

Project yake ya Niroge imefeli mapema wakati Jide ana sold out concert.
 
mziki hauna lugha jamaa
Wamesahau kuwa wamecheza sana miziki ya kikongo, reggae na wanaendelea kusikiliza miziki ya àkina Rihanna na wanaija ingawa lugha sio kiswahili na wanaipenda.
 
Hivi kwaito na beat za naija anazotumia Diamond na wenzake asili yake ni Tz!? Ungesema mchiriku au singeli ningeelewa. Wote wanaiga tu.
 
Watu wanasema huyu ni Ciara wanna be
Usikute ndio kinachamgharimu
 
uzungu umemzidia, kazi zake amelenga zaid watu wa nje kuliko soko la ndani!!
abadilike tu la sivyo itakua hivihivi tu miaka yote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…