Watanzania, hususani wa Dar, tuache ulimbukeni wa kuagiza watu mizigo isiyo na tija watu wanaposafiri

Watanzania, hususani wa Dar, tuache ulimbukeni wa kuagiza watu mizigo isiyo na tija watu wanaposafiri

SIPIYU30

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2012
Posts
1,751
Reaction score
2,437
Wakati mwingine tunafanya mambo tukidhani tunasolve matatizo, kumbe tunajiongezea Utamaduni huu umezoeleka miongoni mwetu kama sehemu ya maisha, lakini mimi nauita ushamba. Ikitokea mtu anatoka mikoani kuja mjini hususan Dar, au hata huko mikoani kwenyewe, mtu unatoka mkoa huu unaenda mwingine, utasikia mtu anaagiza "usisahau kunichukulia nyanya, parachichi, maembe, n.k.

Bei ya parachichi hapa Dar ni kati ya sh. 500 hadi 1000. Huko mikoani inauzwa 400 hadi 800. Tofauti ya bei ni sh. 200 tuu kwa tunda moja. Sasa nijitwishe nyanya ndoo, parachichi, sijui na mengineyo. nakubebea wewe mtu wa Dar. Hivi mnajua usumbufu tunaopata kwenye mabasi kubebeshana na hiyo mizigo? Ukifika stend wala huji kupokea nibebeshane nao, nilipe watu wanibebee mpaka kwenye bajaj au daladala. Humo kwenye daladala mara uambiwe ulipie mzigo. Hata kama nina kigari changu, unajua implications za kuongeza uzito kwa kulundika mizigo kwenye hivi vigari vyetu corolla?

Kwa mahesabu ya kiuchumi, hakuna tofauti yoyote ya gharama uliyookoa. Sasa, afadhali kama mtu anakutumia hela ya kuvinunua. Bado atataka umchukulie kwa hela yako.... jamani jamani watu wa Dar... acheni hizo basi. Mbona nyie mkija kijijini hata kubeba nguo mbili tatu ambazo zimekuvuka ukapaki kwenye begi la ziada ukaja nalo kijijini ambako wenzio wataziona mpya huwezi? Unalalamika mizigo mingi...

mimi mizigo isiyo na ulazima sihangaiki nayo, hata ukinipa bure nipeleke kwetu, kama haina tija kiuchumi mtaniona ,mbaya tuu poa. Kuna siku nikiwa mkoa x, nilisafiri hadi mkoa z ambako ndio kijijini kwetu. Umbali kati ya hiyo mikoa ni km 650. Ajabu, siku naaga kurudi mkoa x, nawasha gari, nikaona shemeji anakuja na furushi kubwa nikaogopa... Kanijazia debe mbili za viazi vitamu. Sasa ili nisimkatishe tamaa nikapokea mzigo.... Nilipowasha gari tuu, nikafikiria fasta either nikifika mjini kama km 20 tu mbele niuze. Baadaye nikawaza napita kwa broo mwingine kama 50km ahead. na kule kuna ukame vyakula kama hivyo havipatikani sana wanahemea huku, nikaona bora nikaudamp huko kwa bro tena watoto watashukuru sana. Haiwezekani nitembee na debe 2 za viazi kilometa 600 wakati huku niliko bei ni ile ile, kama kuna tofauti haizidi sh 2000 tuu.Huyu shem wangu nilimsamehe tu bure, kwa sababu ya village culture, hana exposure na magari, wala safari ndefu. Nilimsamehe kwa ignorance yake, lakini nyie wa mjini, siwezi kusema ni ujinga, bali ni ulimbukeni na unyonyaji.

Hiki kisa changu nimeweka tu kama mkolezo, lakini watu wa Dar mnatusumbua jamani, acheni kutuagiza hovyo hovyo, hailipi..... acheni unyonyaji
 
Ndio maana mimi nlishaamua nikienda kijijin napanda ndege na anaeagiza namwambia kusafirisha mizigo kwa ndege ni gharama, alaf lazma ifike mahala tuache kuvalue gharama kwakutumia kigezo cha fedha tu, watu wajue hata muda, usumbufu ni gharama
 
Mkuu nakuunga mkono hapo kwenye kuagiziwa kwa kweli inakera sometimes .. Lakini ni utamaduni kwa mikoa au niseme makabila mengi hapa Tz unapoenda kutembelea either kijijini au popote pale haipendezi kwenda mikono mitupu, na pia unapoondoka ugenini na wao pia hawakuachi urudi mikono mitupu. Ni aina fulani ya ukarimu.

Ila haya mambo ya mtu kukwambia naomba niletee nyanya, vitunguu etc of course unaweza kukataa kwa kutoa sababu zako.
 
Sitasahau siku mnyalukolo mmoja aliponipigia Simu na kuagiza Supu ya pweza bila aibu. Tena akaelekeza kabisa iweke kwenye thermos itafika haijaharibika.. Haa watu wa mikoani bwana...
 
Hata sibebi mzigo asee[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Niliwahi kutumwa miche ya sabuni nipeleke kijijini kwa wazazi wa mshkaji mmoja. Nilichofanya niliiacha geto kwangu nikaenda mpaka bush nikanunua kwenye kiosk nikawapelekea.

Niliporudi wazazi wa mshkaji wakanituma debe la maharage, nikayaacha home kwetu nikaja mpaka dar nikamwitisha mshkaji kufika geto kwangu akamaindi kuona miche ya sabuni aliyonituma imelala geto, nikampeleka sokoni nikanunua debe la maharage nikamtwisha na kumwambia ni zawadi ya wazazi wake baada ya kuwapa miche ya sabuni uliyowatumia. AKAEREWA

Sijui na nyinyi MMENIEREWA? Sitaki ujinga kabisa
 
Mkuu husisahau kuniletea makabichi ukifika uyole
 
Wa mikoani kwa vizinga sasa khaaa... watu watakuwa wanatembea na ATM card za exim sasa huko mikoani hamna...
 
Inategemea ....inawezakana kikijin kwenu kuna njaa ..na wewe mtoa mada unaonekana una njaa sana ...sisi kijijin kwetu ukika kuondoka unapewa kuku kama 10 ...sasa hapo unawaachaje si bora uwauze ...ili... au wakuukangie ....then mtu kukupa zawadi ...ni Kama ameamua kupay back ...kwasababu unapokwenda kumtembelea kijijin.... anaona umemthamin...kwaiyo ni kama na yeye anapoamua kukupa kijizawadi ...nikama anaamua kulipa Fadhila....ila kiukwel wewe mtoa mada inaonekana ...kijijin kwenu kuna Njaa sana.
 
Hivi dar ni wilaya ee[emoji23] au ni nchi nyingine?


Uwe unakataa kubeba mizigo wakikuagiza
 
Ndio maana mimi nlishaamua nikienda kijijin napanda ndege na anaeagiza namwambia kusafirisha mizigo kwa ndege ni gharama, alaf lazma ifike mahala tuache kuvalue gharama kwakutumia kigezo cha fedha tu, watu wajue hata muda, usumbufu ni gharama

Kijiji gan kina uwanja wa ndege?chato au

Swissme
 
Wakati mwingine tunafanya mambo tukidhani tunasolve matatizo, kumbe tunajiongezea Utamaduni huu umezoeleka miongoni mwetu kama sehemu ya maisha, lakini mimi nauita ushamba. Ikitokea mtu anatoka mikoani kuja mjini hususan Dar, au hata huko mikoani kwenyewe, mtu unatoka mkoa huu unaenda mwingine, utasikia mtu anaagiza "usisahau kunichukulia nyanya, parachichi, maembe, n.k.

Bei ya parachichi hapa Dar ni kati ya sh. 500 hadi 1000. Huko mikoani inauzwa 400 hadi 800. Tofauti ya bei ni sh. 200 tuu kwa tunda moja. Sasa nijitwishe nyanya ndoo, parachichi, sijui na mengineyo. nakubebea wewe mtu wa Dar. Hivi mnajua usumbufu tunaopata kwenye mabasi kubebeshana na hiyo mizigo? Ukifika stend wala huji kupokea nibebeshane nao, nilipe watu wanibebee mpaka kwenye bajaj au daladala. Humo kwenye daladala mara uambiwe ulipie mzigo. Hata kama nina kigari changu, unajua implications za kuongeza uzito kwa kulundika mizigo kwenye hivi vigari vyetu corolla?

Kwa mahesabu ya kiuchumi, hakuna tofauti yoyote ya gharama uliyookoa. Sasa, afadhali kama mtu anakutumia hela ya kuvinunua. Bado atataka umchukulie kwa hela yako.... jamani jamani watu wa Dar... acheni hizo basi. Mbona nyie mkija kijijini hata kubeba nguo mbili tatu ambazo zimekuvuka ukapaki kwenye begi la ziada ukaja nalo kijijini ambako wenzio wataziona mpya huwezi? Unalalamika mizigo mingi...

mimi mizigo isiyo na ulazima sihangaiki nayo, hata ukinipa bure nipeleke kwetu, kama haina tija kiuchumi mtaniona ,mbaya tuu poa. Kuna siku nikiwa mkoa x, nilisafiri hadi mkoa z ambako ndio kijijini kwetu. Umbali kati ya hiyo mikoa ni km 650. Ajabu, siku naaga kurudi mkoa x, nawasha gari, nikaona shemeji anakuja na furushi kubwa nikaogopa... Kanijazia debe mbili za viazi vitamu. Sasa ili nisimkatishe tamaa nikapokea mzigo.... Nilipowasha gari tuu, nikafikiria fasta either nikifika mjini kama km 20 tu mbele niuze. Baadaye nikawaza napita kwa broo mwingine kama 50km ahead. na kule kuna ukame vyakula kama hivyo havipatikani sana wanahemea huku, nikaona bora nikaudamp huko kwa bro tena watoto watashukuru sana. Haiwezekani nitembee na debe 2 za viazi kilometa 600 wakati huku niliko bei ni ile ile, kama kuna tofauti haizidi sh 2000 tuu.Huyu shem wangu nilimsamehe tu bure, kwa sababu ya village culture, hana exposure na magari, wala safari ndefu. Nilimsamehe kwa ignorance yake, lakini nyie wa mjini, siwezi kusema ni ujinga, bali ni ulimbukeni na unyonyaji.

Hiki kisa changu nimeweka tu kama mkolezo, lakini watu wa Dar mnatusumbua jamani, acheni kutuagiza hovyo hovyo, hailipi..... acheni unyonyaji
Mkuu inaonekana wewe ni mpole sana au aina Fulani ya MTU mstaarabu sana .Nawaza tu kwa jinsi nilivyo serious MTU ana anza anzaje kuniambia upuuzi kama huo?
 
Hao wanaokuagiza uwaletee ni Sawa hawafanyi vizuri na una haki ya kunung'unika lakini nikwambie tu mtu anayekupa mzigo upeleke kwako anakuwa kakudhamini sana nashaa unachukia dhamani mtu anayokuonyesha na huwa hawakupi wewe wanasema wapelekee watoto na familia wanajua mjini vipo lakini wanakupa kama shukrani ya kuwatembelea wakati wewe unashishindwa kubeba kwenye gari wasio na magari wakipewa wanabeba kichwani wakiwa na furaha tele
 
Back
Top Bottom