Watanzania hutumia miaka 10 hadi 15 kujenga nyumba

Watanzania hutumia miaka 10 hadi 15 kujenga nyumba

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Licha ya kuwepo kwa mwamko wa wananchi kujenga nyumba kupitia fedha zao za mfukoni, hali inaonyesha kuwa huwachukua wastani wa miaka kumi hadi miaka 15 kumaliza kujenga nyumba hizo.

Hayo yameelezwa leo Ijumaa Agosti 9, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah.

“Mpaka sasa asilimia 99 ya Watanzania wanajenga nyumba kupitia fedha za mfukoni mwao ambazo nyingi ni zile za kudunduliza na hivyo kuchukua muda mrefu kuzimaliza,’’ amesema.

images (16).jpeg

Watanzania wengi wanaishi kwenye nyumba zinazoendelea kujengwa​

Ni kutokana na hilo amesema wengi wao huishi katika nyumba ambazo bado hazijamalizika na pale wanapopata fedha, humalizia chumba kimoja kimoja wakiwa ndani.

Pia Abdallah amesema takwimu pia zinaonyesha mpaka sasa kuna uhaba wa nyumba milioni 3.8 huku uhitaji wa nyumba kila mwaka ukiwa ni 3000 na kati ya nyumba hizo zipo za kupanga au za kununua.

“Ukiangalia kwa kazi tunayoifanya tunatakiwa kupambana na uhitaji wa watu wa nyumba hizo lakini wakati huohuo kuangalia ongezeko la watu na kuitumia kama fursa katika biashara ya nyumba.

“Takwimu zinaonyesha kuwa hadi kufika mwaka 2050, asilimia 44 ya Watanzania watakuwa wanaishi mjini na hali hiyo imeanza kujionyesha namna Dar es Salaam kwa sasa ilivyojaa na wengi huishi mkoani Pwani na kuja kufanya kazi Dar es Salaam.

“Vilevile kuanza kwa mradi wa treni ya umeme tutegemee watu wengi wataishi Morogoro na kuja kazini Dar es Salaam,” amesema Abdallah.
 
Licha ya kuwepo kwa mwamko wa wananchi kujenga nyumba kupitia fedha zao za mfukoni, hali inaonyesha kuwa huwachukua wastani wa miaka kumi hadi miaka 15 kumaliza kujenga nyumba hizo.

Hayo yameelezwa leo Ijumaa Agosti 9, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah.

“Mpaka sasa asilimia 99 ya Watanzania wanajenga nyumba kupitia fedha za mfukoni mwao ambazo nyingi ni zile za kudunduliza na hivyo kuchukua muda mrefu kuzimaliza,’’ amesema.

View attachment 3065896
Watanzania wengi wanaishi kwenye nyumba zinazoendelea kujengwa​

Ni kutokana na hilo amesema wengi wao huishi katika nyumba ambazo bado hazijamalizika na pale wanapopata fedha, humalizia chumba kimoja kimoja wakiwa ndani.

Pia Abdallah amesema takwimu pia zinaonyesha mpaka sasa kuna uhaba wa nyumba milioni 3.8 huku uhitaji wa nyumba kila mwaka ukiwa ni 3000 na kati ya nyumba hizo zipo za kupanga au za kununua.

“Ukiangalia kwa kazi tunayoifanya tunatakiwa kupambana na uhitaji wa watu wa nyumba hizo lakini wakati huohuo kuangalia ongezeko la watu na kuitumia kama fursa katika biashara ya nyumba.

“Takwimu zinaonyesha kuwa hadi kufika mwaka 2050, asilimia 44 ya Watanzania watakuwa wanaishi mjini na hali hiyo imeanza kujionyesha namna Dar es Salaam kwa sasa ilivyojaa na wengi huishi mkoani Pwani na kuja kufanya kazi Dar es Salaam.

“Vilevile kuanza kwa mradi wa treni ya umeme tutegemee watu wengi wataishi Morogoro na kuja kazini Dar es Salaam,” amesema Abdallah.
Mchawi wao anajulikana
 
True, jenga nyumba size utakayoweza kuimaliza vizuri ipendeze. Unakuta four bedroom house, kila chumba ni self contained, sitting room ni 40sqm, jiko kama uwanja wa mpira.. kipato chenyewe hakiruhusu. Lazima utajenga hadi unazeeka.
Yaan utachunda🤒
 
Licha ya kuwepo kwa mwamko wa wananchi kujenga nyumba kupitia fedha zao za mfukoni, hali inaonyesha kuwa huwachukua wastani wa miaka kumi hadi miaka 15 kumaliza kujenga nyumba hizo.

Hayo yameelezwa leo Ijumaa Agosti 9, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah.

“Mpaka sasa asilimia 99 ya Watanzania wanajenga nyumba kupitia fedha za mfukoni mwao ambazo nyingi ni zile za kudunduliza na hivyo kuchukua muda mrefu kuzimaliza,’’ amesema.

View attachment 3065896
Watanzania wengi wanaishi kwenye nyumba zinazoendelea kujengwa​

Ni kutokana na hilo amesema wengi wao huishi katika nyumba ambazo bado hazijamalizika na pale wanapopata fedha, humalizia chumba kimoja kimoja wakiwa ndani.

Pia Abdallah amesema takwimu pia zinaonyesha mpaka sasa kuna uhaba wa nyumba milioni 3.8 huku uhitaji wa nyumba kila mwaka ukiwa ni 3000 na kati ya nyumba hizo zipo za kupanga au za kununua.

“Ukiangalia kwa kazi tunayoifanya tunatakiwa kupambana na uhitaji wa watu wa nyumba hizo lakini wakati huohuo kuangalia ongezeko la watu na kuitumia kama fursa katika biashara ya nyumba.

“Takwimu zinaonyesha kuwa hadi kufika mwaka 2050, asilimia 44 ya Watanzania watakuwa wanaishi mjini na hali hiyo imeanza kujionyesha namna Dar es Salaam kwa sasa ilivyojaa na wengi huishi mkoani Pwani na kuja kufanya kazi Dar es Salaam.

“Vilevile kuanza kwa mradi wa treni ya umeme tutegemee watu wengi wataishi Morogoro na kuja kazini Dar es Salaam,” amesema Abdallah.
Tafiti nyingine ni kama zinafanywa na walevi, au basi tu...
 
Sasa wao kama shirika la nyumba la taifa wanafanyaje kutusaidia wa Tanzania tunamiliki nyumba za ndoto zetu kwa wakati muafaka.

Nazikubali nyumba zao ila location zao na viwanja vinakua vidogo. Sisi wafugaji na wakulima tunashindwa kutimiza ndoto zetu
 
Hayo ndo niliyakataa....

Unajenga nyumba MDA mrefu Sana,

unakuja kuhamia bati tyr lishapauka,

fashion uliyojenga tayari ishapitwa na wakati.

Unajikuta unaishi kwenye makumbusho (historical site).
😂😂😂😂😂
 
True, jenga nyumba size utakayoweza kuimaliza vizuri ipendeze. Unakuta four bedroom house, kila chumba ni self contained, sitting room ni 40sqm, jiko kama uwanja wa mpira.. kipato chenyewe hakiruhusu. Lazima utajenga hadi unazeeka.
Jumbaa kubwaaaa la nin na ndio unajipanga Upo sahihi
 
Serikali ikopeshe watumishi wake hela za kujenga nyumba. Tena iwe free of Interest.

Mbona wabunge wana kopeshwq magari ya milion 200
 
Hao wanao jenga nyumba miaka 10 hawaibi hela
Wanaojenga nyumba ya thamani ya bln 1 ,mln 700 kwa miezi miwili hela wanatoa wapi alafu wengi wao watumishi wa umma

Ova
 
Serikali ikopeshe watumishi wake hela za kujenga nyumba. Tena iwe free of Interest.

Mbona wabunge wana kopeshwq magari ya milion 200
Zamani kulikuwepo na bank ya nyumba THB nakumbuka ilikuwa opposite na sananu la askari
Kilichokikuta bank ile wanajuwa wenyewe

Ova
 
Back
Top Bottom