Watanzania ilitokeaje mkaishia kubadilishiwa kibao na Barrick kwenye madini, hadi mkaangukia pua?

..siku ripoti zinawasilishwa ikulu kulikuwa mpaka na wasanii wa kuimba.

..hivi umeona wapi ripoti ya uchunguzi, ya kitaalamu, uwasilishaji wake unatanguliwa na nyimbo za wasanii?

Unakomalia kwa $191b. Wewe huelewi vita na mabeberu hufanywa kwa mikakati gani. Uliza wakenya 'Mau mau' walidai ngapi kwa beberu waliowafunga jela katika harakati za Uhuru na hatimaye walilipwa ngapi.

Fahamu Barric na Accacia ni limited liability companies..Hauwezi wadai zaidi ya Assets zilizopo kwa balance sheet na hawafikishi hata hiyo $191b.

Magu alijua hilo, Na alidai akijua hilo. Na matunda yake ni 50:50 shareholding, 50:50 profit share.

Tafuta mkataba kama huo afrika nzima unioneshe.

Tuseme magu level yake ya negotiations ipo juu kinyama. Hauwezi elewa kwa kupitiapitia tu juu juu, utumbo na tamaa za $191b
 
Uchambuzi mzuri
 
Kwa upande mwingine ndo maana serikali ilivipiga marufuku vyombo vya nje kurusha maudhui bila kibali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…