Amani Msumari
JF-Expert Member
- Aug 21, 2016
- 1,830
- 972
Wapendwa watanzania wenzangu,
Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kikiomba michango kutoka kwa watanzania katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokikabili chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Watanzania tuna utaratibu wa kuchangiana kwenye mambo mbalimbali hususani misiba na harusi. Hata CHADEMA wanaomba michango kutokana na utaratibu uleule wa kuchangiana, hivyo sio mbaya.
Hatahivyo, nina maswali ya kuhoji Kuhusu Michango hiyo:
Je, ruzuku inayopokelewa chamani, inafanya kazi gani?
Je, yale makato ya shilingi milioni moja kwa kila mbunge, yanatumikaje?
Chama hakina utaratibu wa kupata michango kutoka kwa wanachama wao badala ya kulifanya kuwa jambo la kitaifa?
Kuna uwazi gani katika mapato na matumizi ya michango hiyo?
Je, chama hakikujua kuwa kuna uchaguzi unakuja na kuwa una gharama?
Je, kuwaomba watanzania michango ilihali wamekuwa wakisemwa kuwa ni mafukara sana na kuwa wamepigika si ni unyonyaji kama ni kweli?
Je, mbona hatuoni nguvu kubwa ikitumika kuomba michango kwa ajili ya harambee za kujenga vyumba vya madarasa, zahanati na mambo mengine ya kusaidia maendeleo ya watu wao?
#Kuulizasiujinga
Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kikiomba michango kutoka kwa watanzania katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokikabili chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Watanzania tuna utaratibu wa kuchangiana kwenye mambo mbalimbali hususani misiba na harusi. Hata CHADEMA wanaomba michango kutokana na utaratibu uleule wa kuchangiana, hivyo sio mbaya.
Hatahivyo, nina maswali ya kuhoji Kuhusu Michango hiyo:
Je, ruzuku inayopokelewa chamani, inafanya kazi gani?
Je, yale makato ya shilingi milioni moja kwa kila mbunge, yanatumikaje?
Chama hakina utaratibu wa kupata michango kutoka kwa wanachama wao badala ya kulifanya kuwa jambo la kitaifa?
Kuna uwazi gani katika mapato na matumizi ya michango hiyo?
Je, chama hakikujua kuwa kuna uchaguzi unakuja na kuwa una gharama?
Je, kuwaomba watanzania michango ilihali wamekuwa wakisemwa kuwa ni mafukara sana na kuwa wamepigika si ni unyonyaji kama ni kweli?
Je, mbona hatuoni nguvu kubwa ikitumika kuomba michango kwa ajili ya harambee za kujenga vyumba vya madarasa, zahanati na mambo mengine ya kusaidia maendeleo ya watu wao?
#Kuulizasiujinga