Uchaguzi 2020 Watanzania lazima tuhoji kuhusu michango hii inayochangishwa na CHADEMA

Uchaguzi 2020 Watanzania lazima tuhoji kuhusu michango hii inayochangishwa na CHADEMA

Amani Msumari

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2016
Posts
1,830
Reaction score
972
Wapendwa watanzania wenzangu,

Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kikiomba michango kutoka kwa watanzania katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokikabili chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Watanzania tuna utaratibu wa kuchangiana kwenye mambo mbalimbali hususani misiba na harusi. Hata CHADEMA wanaomba michango kutokana na utaratibu uleule wa kuchangiana, hivyo sio mbaya.

Hatahivyo, nina maswali ya kuhoji Kuhusu Michango hiyo:

Je, ruzuku inayopokelewa chamani, inafanya kazi gani?

Je, yale makato ya shilingi milioni moja kwa kila mbunge, yanatumikaje?

Chama hakina utaratibu wa kupata michango kutoka kwa wanachama wao badala ya kulifanya kuwa jambo la kitaifa?

Kuna uwazi gani katika mapato na matumizi ya michango hiyo?

Je, chama hakikujua kuwa kuna uchaguzi unakuja na kuwa una gharama?

Je, kuwaomba watanzania michango ilihali wamekuwa wakisemwa kuwa ni mafukara sana na kuwa wamepigika si ni unyonyaji kama ni kweli?

Je, mbona hatuoni nguvu kubwa ikitumika kuomba michango kwa ajili ya harambee za kujenga vyumba vya madarasa, zahanati na mambo mengine ya kusaidia maendeleo ya watu wao?

#Kuulizasiujinga
 
Hayakuhusu, hujalazimishwa kuchangia....Hivi kwanza unajua gharama za kuendesha kampeni za urais kwa Tanzania nzima wewe kapuku......Uliza kwanza kwanini CCM wantumia Mali na pesa za walipa kodi kufanyia kampeni mgombea wao...Kapuku wewe
 
Mchango ni hiari ndugu na hakuna alolazimishwa, cha ajabu wachangiaji wako happy ila wasochangia ndo wana-vijiba vya roho....

Tatizo lako ni hiyo Username uitumiayo, si lazima uwe against opposition kisa tu watumia jina lalo halisi. Wakeup !!
 
CHADEMA Ni chama kizuri lakini hakina fedha za kutosha kufanya kampeni nchi nzima . Na ccm Ni chama kilichobaki madarakani kwaiyo mambo ya fedha za kampeni Ni kukwaruza vocha na kaingiza kwenye simu tu .

NB Lissu anahangaika tu na kampeni zake hawezi kuchukua uraisi ,labda nchi ya ahadi
 
Pia tuhoji pesa zinazochotwa HAZINA kwa ajili ya kampeni za CCM

gari zaidi ya 60 mnatoa wapi hela za mafuta na posho za waliomo kwenye hayo magari??
 
Unako elekea utaishia tu kuvalishwa kanga na kuchezeshwa Baikoko! Haiwezekani mwanaume uwe na hulka za umbea na kuwashwa washwa kiasi hiki!
 
Lengo la hiyo michango ni kuwafuta machozi watumishi wa umma waliotelekezwa na Meko kwa miaka mitano bila nyongeza ya mishahara wala kupandishwa vyeo.
 
Mbona CCM mnachangisha fedha ila hujaesema hapa?Au hujui kama mnafanya hilo?Mnatembeza bakuli kwenye taasisi za serikali na wao wanawachangia kwa kulazimika!
Hukuona siku ya ufunguzi bashiru akitaja mamilioni yaliyochangwa?
Unajua gharama za uchaguzi ni kubwa kiasi gani?
Hebu hangaikeni na CCM yenu huko mtuachie CDM yetu pendwa!
 
Achana nasisi!
... TUNAIPENDA WENYEWE CHADEMA YETU!

[SUP]NB: Mali tulizoichangia CCM, wakati wa chama kimoja, CCM Kirumba ... etc, ZITAIFISHWE![/SUP]
😅
👊 ✌✌✌💥
 
Ccm hamchangishi kwani
Wapendwa watanzania wenzangu,

Katika siku za hivi karibuni tumeshuhudia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kikiomba michango kutoka kwa watanzania katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokikabili chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Watanzania tuna utaratibu wa kuchangiana kwenye mambo mbalimbali hususani misiba na harusi. Hata CHADEMA wanaomba michango kutokana na utaratibu uleule wa kuchangiana, hivyo sio mbaya.

Hatahivyo, nina maswali ya kuhoji Kuhusu Michango hiyo:

Je, ruzuku inayopokelewa chamani, inafanya kazi gani?

Je, yale makato ya shilingi milioni moja kwa kila mbunge, yanatumikaje?

Chama hakina utaratibu wa kupata michango kutoka kwa wanachama wao badala ya kulifanya kuwa jambo la kitaifa?

Kuna uwazi gani katika mapato na matumizi ya michango hiyo?

Je, chama hakikujua kuwa kuna uchaguzi unakuja na kuwa una gharama?

Je, kuwaomba watanzania michango ilihali wamekuwa wakisemwa kuwa ni mafukara sana na kuwa wamepigika si ni unyonyaji kama ni kweli?

Je, mbona hatuoni nguvu kubwa ikitumika kuomba michango kwa ajili ya harambee za kujenga vyumba vya madarasa, zahanati na mambo mengine ya kusaidia maendeleo ya watu wao?

#Kuulizasiujinga

Amani Msumari
Tanga
 
Hata kupanda mbegu au Deci watu mwanzoni hawakujua madhara yake.
Katika pilikapilika za uchaguzi wapo wafia chama wamejitoa kwa hali na mali.
Lakini wapo vibaka wanachukulia nafasi hizo kama ni fursa ya kujitajirisha.
Sio kubeza tu,weka makisio,mapato,matumizi wazi.Ili kujenga uadililifu kabla hamjachukuwa dola.
 
Ruzuku ni sh. Ngapi wanapokea na kulipa watumishi na kuendesha chama ni sh. Ngapi kwa mwaka?
Ccm wamewahi kueleza hadharan matumiz yao? Je unataka kusema chadema haina vikao vyao? Je CAG huwa anakagua nini kule?
KAULIZE ZILE ZA BUKOBA ZILIISHIA WAPI
 
Back
Top Bottom