Watanzania matatizo yenu hayatamalizwa na Hayati Magufuli. Hatujadili tena mstakabili wa nchi yetu!

Watanzania matatizo yenu hayatamalizwa na Hayati Magufuli. Hatujadili tena mstakabili wa nchi yetu!

Mwisho wake ni nini?
Katika nchi ya watu wanaojifunza na kujiongeza, natumaini kadiri watu wanavyoweza kuchambua mambo kwa kina zaidi, ndivyo elimu itakavyoweza kupatikana, watu wajifunze kwa nuance.

1. Mazuri ya Magufuli ni yapi?
2. Mabaya ya Magufuli ni yapi?
3. Mambo gani tunaweza kufanya ili tusirudie mabaya aliyotuletea Magufuli?
4. Mambo gani tunaweza kufanya ili tujiongeze katika mazuri aliyotuletea Magufuli?

Bila kujua historia yetu, tumetoka wapi, kwa nini tumetoka hapo, na sasa tunakwenda mbele ya hapo au tunarudi nyuma, hatuwezi kupanga mipango vizuri.

Na maisha ya rais ni sehemu kubwa ya kuchambua historia yetu.

Kwa nini kumuongelea Magufuli liwe jambo la ajabu na linalopingwa?

Huyu ni mtu alikuwa rais wa watu zaidi ya milioni 60 kwa multiple presidential terms.

Magufuli anatakiwa kuandikiwa vitabu vya kuchambua maisha yake yote, tangu kifamilia, alivyosoma, alivyofanya kazi, alivyoingia katika siasa z abunge, alivyopata uwaziri, mpaka urais.

Kapanda vipi? Mfumo wetu umeruhusu vipi mtu kama huyu kupanda?
 
Katika nchi ya watu wanaojifunza na kujiongeza, natumaini kadiri watu wanavyoweza kuchambua mambo kwa kina zaidi, ndivyo elimu itakavyoweza kupatikana, watu wajifunze kwa nuance.

1. Mazuri ya Magufuli ni yapi.
2. Mabaya ya Magufuli ni yapi?
3. Mambo gani tunaweza kufanya ili tusirudie mabaya aliyotuletea Magufuli?
4. Mambo gani tunaweza kufanya ili tujiongeze katika mazuri aliyotuletea Magufuli?

Bila kujua historia yetu, tumetoka wapi, kwa nini tumetoka hapo, na sasa tunakwenda mbele ya hapo au tunarudi nyuma, hatuwezi kupanga mipango vizuri.

Na maisha ya rais ni sehemu kubwa ya kuchambua historia yetu.

Kwa nini kumuongelea Magufuli liwe jambo la ajabu na linalopingwa?

Huyu ni mtu alikuwa rais wa watu zaidi ya milioni 60 kwa multiple presidential terms.

Umeongea pointi mkuu!
 
Kesho ni siku ya maombolezo.

Happy Magufuli day everyone.


Nitaiadhimisha siku hii kwa kumuombea misa ya shukrani kwa maisha ya mtumishi wa Mungu JPM.

Karibuni St.Joseph Catherdal tushiriki pamoja kumshukuru Mungu.

Mungu ni wetu sote.
 
Kesho ni siku ya maombolezo.

Happy Magufuli day everyone.


Nitaiadhimisha siku hii kwa kumuombea misa ya shukrani kwa maisha ya mtumishi wa Mungu JPM.

Karibuni St.Joseph Catherdal tushiriki pamoja kumshukuru Mungu.

Mungu ni wetu sote.
Amen
 
Hata viongozi walioongoza nchi vibaya wanazungumziwa, ili mabaya waliyoyafanya yajulikane, yakataliwe, yasirudiwe.

Ndiyo maana kila mwaka kuna vitabu vipya vinaandikwa, vya Hitler, vya Idi Amin.

Watu wajifunze.

Chuki yako dhidi ya Magufuli isikufanye ukoseshe watu nafasi ya kujifunza kutokana na maisha yake.

Kama humpendi Magufuli kwa sababu ya mabaya aliyoyafanya, chukua mazungumzo yoyote kuhusu Magufuli kama nafasi ya kumulika mabaya yake.

Usikataze watu kumuongelea.

That is censorship.

Ukikataza watu kumuongelea Magufuli na wewe utakuwa unaendeleza u Magufuli.

Utakuwa mfuasi wake ambaye hukumpenda kwa sababu hukuwa wewe kwenye kiti tu, lakini ulitamani kuwa kama yeye.

Let people talk maan, after all, kama hupendi mazungumzo hayo si unayaruka tu, kwani lazima uchangie kila mazungumzo?
Kwahy bado hamjamaliza kuzungumza mabaya yake au hua mnarudia-rudia.?
 
Kwahy bado hamjamaliza kuzungumza mabaya yake au hua mnarudia-rudia.?
Mkuu,

Hapa sasa nasoma kitabu kipya cha maisha ya Idi Amin. Kimeandikwa na Mark Leopold na kuchapishwa mwaka 2021. Kinaitwa "Idi Amin: The Story of Africa's Icon of Evil".

Ndiyo kwanza nimemaliza kusoma vitabu vitatu vya "Development as Rebellion: A Biography of Julius Nyerere"

by Issa G. Shivji, Ng'wanza Kamata, and Saida Yahya-Othman.

Hatujamaliza kuwaongelea Idi Amin na Nyerere, unataka tuwe tumemaliza kumuongelea Magufuli mara hii?

Tatizo si kwamba watu wanamuongelea sana Magufuli.

Tatizo watu hawajamuongelea vya kutosha.

Kwa mfano, tangu afariki hakuna hata kitabu kimoja kilichoandikwa kuhusu maisha yake.

Ni jamii za watu wasio na elimu tu ambazo zinaishi bila kuzungumzia viongozi wao, watu walioelimika ni lazima wawazungumzie viongozi wao.

Huyu mtu kaongoza zaidi ya watu milioni sitini, kwa nini asiongelewe?
 
Kuna point moja ya muhimu sana kuielewa.

Kichwa cha thread ni kama kinawasuta Watanzania, kwamba wanamuongelea sana JPM ili awatatulie matatizo yao, wakati JPM kashakufa, hawezi kuwasaidia.

Mtu akishafariki ndiyo kafariki, hawezi kusaidia moja kwa moja.

Msiba na shughuli za kilio, uchambuzi wa maisha ya marehemu etc ni kwa ajili ya watu waliobaki, wajiongeze vipi, wafarijiane vipi, wajifunze nini kutoka maisha ya marehemu.

Si kwamba watu wanamuomba Magufuli awasaidie.
 
Ile 17 March ilikuwa siku ya ukombozi kwa taifa letu. Ukombozi ulitoka Juu. Atukuzwe Aliye Juu!
Wachaga watarudi kilimanjaro kwa speed ya radi.

Bei ya kiwanja pale old moshi itakua 1b

Mchaga anauzaga ardhi?

Wachaga wanaenda kuwa mabilionea duniani

North kilimanjaro itakuwa upande wa rombo tarakea na kamwanga.ile eneo yotr hata hivyo naskia ni ya marehem malkia.ni sehemu maini kinoma

Hawajawahi kuhama kule

Daah!

Sasa nashindwa namna ya kuelezea jinsi isivyo kawaida kwa aliyekuwa Raisi wa nchi yetu Tanzania hayati John Pombe Magufuli!

Huyu alikuwa ni kiongozi wa aina gani?

Ni miaka miwili sasa hatuna naye, lakini bado hajatoka mioyoni na midomoni mwetu, tena kila uchwao jina lake linakuwa linavutia zaidi kuwa maarufu zaidi mitandaoni na hata kwenye vijiwe vyetu kwa mijadala iwe kwa mabaya ama kwa mazuri, utadhani yupo hai bado!

Naona ni kama tumekwama na hatufanyi tena mijadala kuhusu ustawi wa nchi yetu, badala yake ni jina tunabishana kama wendawazimu kuhusu jina lake! Je, zile chanjo hazijaleta shida?

Tuna matatizo mengi kiasi cha kuzidi hata wakati wa yeye akiwa Raisi, lakini ni kama hatuoni shida hizo! kuna anguko la kifedha duniani na migogoro ya kifedha itayosababisha mgogoro mkubwa kwa nchi zenye madeni na kuanguka kwa uchumi Nani atusaidie?

Tuna matatizo ya chakula, mvua kutokunyesha kwa wakati, umeme kukatikatika na kama si kukosekana kabisa, tuna wafanya biashara wengi wameanguka kibiashara shida ikiwa ni TRA

Tunamadeni kama nchi na mengine yameiva na hatuna uwezo wa kuyalipa mpaka tukakope tena ndo tuyalipe!

Huduma mbovu kwenye sector za kiserikali, tunawatoto wako shule miaka saba lakini hawajui hata kuandika majina yao na wengine wako secondary lakini hawajui chochote

Tunaupungufu wa walimu, madaktari, manesi n.k

Kama nchi tutakabiliana vipi na njaa inayotokana na ukosefu wa mvua kwa mwaka huu, mifugo yetu itaishije kwenye ukame ujao, watu wetu vipi,

Badala ya kuongelea mambo ya mhimu, wasomi wetu ndio wanaongoza mijadala isiyo na tija

Sifahamu, labda ndio sehemu ya wao kufichia udhaifu wao?

Ni lini tutaacha mijadara ya kipuuzi na kuanza kudili na mambo mhimu ya maendeleo kwa nchi yetu?

Si wapinzani wala chama tawala! Wote tunakutanishwa hapa kumwongelea mtu asiyekuwa nasi!

Nchi za watu weusi iko siri iliyojificha ndani yetu ambapo kuijua kwake, ni hadi wazungu wahame kwenye hii sayari!

Tunapaswa kuendeleza misingi mizuri aliyotuwekea JPM kama tunataka kujikwamua kutoka hapa.

Tuendeleze uchapakazi, upingaji wa rushwa kwa vitendo, kuongeza nidhamu na uwajibikaji, kujenga miundombinu bora.

Tuachane na safari zisizokuwa na tija, mikopo, na kubembelezana.

Kwa kifupi tunapaswa kuwa na uongozi imara kama wa JPM kama tunataka kujikwamua kutoka kwenye mkwamo huu tulionao kama taifa.

Hatutaendelea kwa ku-copy na ku-paste kwa wazungu. Changamoto zao hazilingani na zetu, uwezo wao haulingani na wetu, na zaidi; mazingira yao hayafanani na yetu.

Magufuli ameharibu nchi hii tutanahitaji Ten yrs of maintenance chini ya Rais muislamu Kama Mama samiah

Nchi imeharibiwa na Magufuli kila kitu kaharibu
Ajira kaua
Wawekezaji kaua
Biashara kaua
Kilimo kaua

Sasa what the next be humble we need at-least ten years of Economic reviving.
 
Jina la Magufuli ni faraja kwa wanyonge. Leo ajira za wanyonge zinaitwa laana.

Kwao ufisadi, wizi na ubadhirifu wa mali za umma kwa sasa ndio imekuwa kazi ya heshima sababu wamepewa sehemu ya hilo jasho la wanyonge pasipo gharama yoyote.

Tutaendelea kumuimba Magu hadi mwisho wa nyakati.
 
Mwanasiasa akitaka kick anakuja na shutuma dhidi ya Magu pamoja na kuwa tuna rais mwingine na ni miaka takribani miwili sasa hayupo nasi. Huo ndio ukubwa wake hata baada ya kifo kumchukua, legend in life and afterlife too
 
Tunapaswa kuendeleza misingi mizuri aliyotuwekea JPM kama tunataka kujikwamua kutoka hapa.

Tuendeleze uchapakazi, upingaji wa rushwa kwa vitendo, kuongeza nidhamu na uwajibikaji, kujenga miundombinu bora.

Tuachane na safari zisizokuwa na tija, mikopo, na kubembelezana.

Kwa kifupi tunapaswa kuwa na uongozi imara kama wa JPM kama tunataka kujikwamua kutoka kwenye mkwamo huu tulionao kama taifa.

Hatutaendelea kwa ku-copy na ku-paste kwa wazungu. Changamoto zao hazilingani na zetu, uwezo wao haulingani na wetu, na zaidi; mazingira yao hayafanani na yetu.
Nadhani umekosea. Tunapaswa kuiga uongozi Bora wa smaia siyo jpm
 
Licha ya kero zoote hizi zilizozaliwa ndani ya miaka hii miwili yake?
Hizo no external forces tu kama kupanda kwa mafuta kunakosa abishwa na vita. Nafaka hziji tena kutoka Ukraine. Mvua hazinyeshi nk hivyo Samia has nothing to do with exogenous varaiables.
 
Hizo no external forces tu kama kupanda kwa mafuta kunakosa abishwa na vita. Nafaka hziji tena kutoka Ukraine. Mvua hazinyeshi nk hivyo Samia has nothing to do with exogenous varaiables.
Vipi kuhusu nafaka na vyakula kwa ujumla

Kuhusu umeme vipi mkuu
 
Vipi kuhusu nafaka na vyakula kwa ujumla

Kuhusu umeme vipi mkuu
Lazima vipande bei kwa sababu magari ya kusafirisha kutoka mikoani wanapolima wanatumia magari ambapo bei ya mafuta IPO juu sana. We ombe vita iishe na bei itashuka simultaneously.
 
Lazima vipande bei kwa sababu magari ya kusafirisha kutoka mikoani wanapolima wanatumia magari ambapo bei ya mafuta IPO juu sana. We ombe vita iishe na bei itashuka simultaneously.
Shida ya umeme na huduma bora kwenye vitengo vipi, nazo zinatoka ulaya?
 
Mkuu nchi kujengwa upya is not about single day hapa ni Africa tunaishi kwa Mnyonyoro Sasa Magufuli kakata mnyonyoro wa uchumi vijana wasomi wenye Akili kawageuza wamekuwa wamachinga na wengine bodaboda

Nguvu Kazi ya watu smart upstairs wameishia kuwa bodaboda na Mama ntilie

Huku akiwaita wanyonge so tunabidi kutumia miaka kumi kujenga nchi upya huyu Magufuli hawezi kukumbukwa Hana Jambo la maana alilowafanyia Watanzania yaani eti msomi wa masters anakuwa muuza matunda ya kutembeza Upumbavu mtupu
Daaaah....ulichoandika hapa aibu naona mimi....Tanzania my country
 
Shida ya umeme na huduma bora kwenye vitengo vipi, nazo zinatoka ulaya?
Umeme unqtumia vipuli kutoka nje. Matrasfomer yanatokq nje. Vifaa vya kufulia umeme wa maji vinatoka nje nk. Tunarudi kwenye swala ya usafirishaji wa vifaa hivyo qmbao kwa Sasa ni ghali sana. Mqarobaini wa huduma Bora ni effect ya katiba mbovu tuliyonayo. Labda rais aamue kuwa dictator kama jpm
 
Back
Top Bottom