Watanzania msipotoshwe na hoja za kiukaguzi (Audit queries) maana sio hitimisho kuwa ni ufisadi, zikipatiwa majibu ukweli hujulikana

Watanzania msipotoshwe na hoja za kiukaguzi (Audit queries) maana sio hitimisho kuwa ni ufisadi, zikipatiwa majibu ukweli hujulikana

CAG akisema ninashauri Mamlaka husika zifuatilie kujua kwa nini fedha husika haikutumika mahala hapa au zifuatilie kujua ni kwa nini vielelzo havikuwasilishwa, hapo ndio tunasema kuna hoja za ukaguzi zinazohitaji majibu. ila ripoti ya mwaka huu ni tofauti mkuu, ipo conclusive tayari, mjiandae tu kwenda nyavu.
Umemsikia Spika amesema acheni kupotosha ripoti ya CAG. Ripoti imepelekwa kwenye Kamati ya Bunge kupitiwa kama taratibu za Bunge zinavyosema na Wizara na Taasisi za Serikali zitapata muda wa kuwakirisha ushahidi wao kabla ya kujadiriwa Bungeni na kutolewa uamuzi na ushauri kwa serikali kuhusiana na audit queries ambazo wahusika watashindwa kutoa majibu yanayojitoshereza.
 
Huu ni utaratibu wa kawaida katika kufanya ukaguzi wa matumizi, au taratibu za ujenzi. Kwamba mkaguzi ataibua hoja ya kuwa na wasiwasi juu ya anachokagua pale panapotokea kuwa hakuna vielelezo vya kile anachohoji ili kuthibitisha. Hivyo baada ya kuibua hoja hizo majibu ya uhakika huwa yanahitajika.

Mfano mkaguzi anakagua juu ya manunuzi ya sare za jeshi la polisi, lazima aulizie risiti za manunuzi, usafiri na ikiwezekana aone hizo sare. Asipoziona hapo ndipo huibua hoja ambazo huhitaji majibu.

Kwa hiyo kama CAG ameibua Audit queries sio conclusion kuwa tayari kuna ufisadi. Maana lazima PAC au LAAC watafute majibu ya hizi hoja ili tujue ukweli wake.

Hivyo wanasiasa wapenda sifa kama Zitto wasitumie nafasi hii kupotosha umma kuwa tayari kuna ufisadi.

Mmesahau ishu ya tril 1.5 ambayo ilikuja kupata majibu? Mbona Assad hadi hii leo na hasira zake za kufukuzwa uCAG hajaikumbushia kama kweli zilipigwa.

Tusubiri majibu ya PAC ka LAAC.
Exactly mi nashangaa wanavyoshabikia. Halafu hata kama kuna ubadhilifu maafisa wahusika si wapo. Yaani huu mpango wa Hovyo kabnisa wa kumchafua Hayati Magufuli hawataweza hata kidogo. Sisis wanyomge tuko wengi Team masfisadi wako wachache. Hawawezi kutushinda hata kidogho.
 
Kwahiyo wale wa hati chafu nao tuseme wameonewa flani hivi?

naposema 1.5T zilikuja kupata majibu, UNAWEZA UKATUWEKEA HAPA HAYO MAJIBU? Maana binafsi sikuwahi kuyasikia majibu halisi, ila akina Polepole kujaribu kutueleza mara Zanzibar, mara sijui nini!

HAYO MAJIBU KWANINI HUWA HAWAMPI CAG wakati wanaulizwa? Kwanini ripoti ikishatoka na mnahangaika kumjibu CAG?

Kwani hao wanaoulizwa hayo makitu, huwa hawapewi nafasi ya kueleza au kutoa uthibitisho wa wanayoyasema? Hivi waulizwaji si wanajua kuwa kuna time frame ya wao kutoa majibu na ukivuka wakati huo maelezo yako yanakuwa hayana maana?

NI SAWA NA HUKUMU ILYOTOLEWA MAHAKAMA I INA MUDA WA KUKATIWA RUFAA, MUDA UKIPITA YALIYOAMULIWA YANABAKI KUWA NI MAAMUZI SAHIHI.

HUWEZI SUBIRIWA FOREVER
CAG hufanya exit meeting baada ya ukaguzi ambapo hoja hujibiwa kishwa Management letter hutolewa ili majibu yatolewe kwa maandishi. Kiuhalisia Auditors huwa hawafuti hoja zote vinginevyo ingeonekana hawana kazi waliyofanya. Baada ya report yao kutolewa public,Management hutoa majibu na kisha hufuta baadhi ya hoja kwenye kaguzi zinazofuata kwa kigezo kuwa zimetekelezwa
 
Ninavyojua mimi, audit queries huwa wanapewa hao walifanyiwa ukaguzi, ili wazijibie kabla ya final report.
 
Back
Top Bottom