Watanzania na kichaa cha mpira

The golden

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2018
Posts
1,382
Reaction score
2,582
Kuna hali fulani hivi ya ushabiki naendelea kuiona si ya kawaida. Nadhani imesababishwa na kutazama mpira wa Ulaya.

Watu wamejitolea kwa jasho na damu kupigania mpira kuliko hata maisha yao wenyewe. Kama binadamu jitahidi sana kuhimili mihemko ya mambo ya dunia hii.

Dunia ina mambo mengi sana yenye kuleta hisia kali kama hutajifunza kuyakabili unaweza kuishi maisha ya stress kila siku au kupoteza maisha.

Watanzania wanateswa na haya
1. Umasikini
2. Mpira
3. Mapenzi

Mengine unaweza kuongeza....
 
Tulishawashauri CCM, wakitaka watawale kwa muda mrefu bila kushtukiwa na wananchi, basi wawekeze katika mpira.

Yaani wajenge viwanja vya kisasa kila mkoa, wapunguze bei ya ving'amuzi vinavyorusha mpira, viingilio viwe bei chini.

CCM wakifanya hivyo, watakuwa wamewazubaisha wananchi wengi kwa kiasi kikubwa sana hapa Tanzania! Halafu CCM wenyewe waendelee kupiga hela!
 
Watanzania ni viumbe hai wa ajabu sana duniani, hawana umeme na maji pia vyakula vinapanda bei kila leo ila wao wapo bize na ushabiki wa mipira, ndio maana maisha yanazidi kuwa magumu tu. Wanasahau mambo ya msingi wanajadili mambo mepesi sana.
 
Watanzania ni viumbe hai wa ajabu sana duniani, hawana umeme na maji pia vyakula vinapanda bei kila leo ila wao wapo bize na ushabiki wa mipira, ndio maana maisha yanazidi kuwa magumu tu. Wanasahau mambo ya msingi wanajadili mambo mepesi sana.
Yaani......
 
Ccm wanafurahia sana wakiona hiyo hali!

Nchi nyingine sehemu kama Dar ndio ilipaswa kuwa kitovu cha mabadiliko ila sisi Dar ndio kitovu cha upumbavu, ujinga na uzwazwa unaofanana na huo!?

Maji tu na umeme vilitosha kimuondoa mtu pale ikulu achia mbali mfumuko wa bei,,!

Yani muda wote simba yanga, simba yanga.

Jitu liko busy linatoa mapovu juu ya yanga na simba huku likiwa halijaoga wiki nzima sababu ya uhaba wa maji.

Watu wako kama wamejaza mavi vichwani mwao
 
Acha ushamba..mpira nao ni sehemu ya maisha
 
Watu wamejitolea kwa jasho na damu kupigania mpira kuliko hata maisha yao wenyewe. Kama binadamu jitahidi sana kuhimili mihemko ya mambo ya dunia hii.
Maisha waliyoyachagua ndio hayo. Au wewe ulitaka wafanye kitu gani ndio useme wanapigania maisha? Wamechagua hivyo, nawe uchague vile, jambo la msingi isivunjwe sheria ya mamlaka. Maisha ni furaha, kama mtu ameona furaha yake ataipata kupitia mpira, muziki au mapenzi, acha apiganie hilo, na kama wewe umeona furaha yako ni kutafuta hela, shikilia hapo hapo usiangalie wala kulazimisha mwingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…