Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?

Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?

Katiba MPYA itapatikana siku wananchi wenyewee watakapoitaka. Mchakato wakati a umeathiliwa na migongo ya matakwa ya vyama vya siasa ndio MAANA halina mvuto wowotee. Vyama siasa vikazanie katiba za vyama vyao na siokatiba ya wananchi ambao wengine sio wanavyama vya siasa. Katiba ya wananchi itafutwe na wananchi wenyewee wasio na mgongo wa chama chochote Cha kisiasa, ili tupate katiba itakayosimamia vyama vyote vyasiasa Kwa maslahi mapana ya Taifa.

Wananchi wameshaitaka sana hadi maoni yao yalishakusanywa, tena kisheria. Watawala wa CCM wenye kiburi viburi vya madaraka ndio wameendelea kuizuia katiba hiyo kwa vitisho, hila na ghiliba. Na ww ni mmoja wa hao wafanya ghiliba ili katiba isipatikane. Machafuko tu ndio yataleta katiba mpya.
 
Wananchi wameshaitaka sana hadi maoni yao yalishakusanywa, tena kisheria. Watawala wa CCM wenye kiburi viburi vya madaraka ndio wameendelea kuizuia katiba hiyo kwa vitisho, hila na ghiliba. Na ww ni mmoja wa hao wafanya ghiliba ili katiba isipatikane. Machafuko tu ndio yataleta katiba mpya.
Wananchi gani hao, kama sio wale waliopitia mlango wa vyama vya siasa ambao wamechangia pakubwa kunajisi zoezi zuri la upatikanaji wa katiba? Vya vya siasa kaeni pembeni mchakato uwehuru usiokuwa na chembe ya kiherehere za chama Cha siasa chochote, zoezi liludiwe kama like la kipindi Cha akina walioba na wenzake. Kwa kuwa jambo hili limekua la kisiasa, wananchi Sasa wanaliona kama katiba IMEKUWA ni ya chama Fulani na Kwa matakwa Yao.
 
Kaka Pascal Mayalla una akili sana nadhani kwa vile tunakuona kwa maandishi au kwa jinsi ya nje huenda ndio sababu wakati fulani tunakudhihaki. Lakini nafsi yangu inaniambia viatu vyako ni vikubwa sana, vita vyako sio vya kawaida. Tusamehe sana mkuu wangu, vile ambavyo tunakujudge vibaya kwa sababu ya yale tunayoyaona kwa nje. Mungu akulinde kaka mkubwa
Mkuu Dp800 asante sana kunitia moyo, faraja yangu ni Matayo 5
5 Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.
6 Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.
7 Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.
8 Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.
9 Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.
10 Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.
Zaburi 32 : 7-8,10
Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, Utanizungusha nyimbo za wokovu. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama. Naye mtu mwovu ana mapigo mengi, Bali amtumainiye BWANA fadhili zitamzunguka.
Amen.
P
 
Wananchi gani hao, kama sio wale waliopitia mlango wa vyama vya siasa ambao wamechangia pakubwa kunajisi zoezi zuri la upatikanaji wa katiba? Vya vya siasa kaeni pembeni mchakato uwehuru usiokuwa na chembe ya kiherehere za chama Cha siasa chochote, zoezi liludiwe kama like la kipindi Cha akina walioba na wenzake. Kwa kuwa jambo hili limekua la kisiasa, wananchi Sasa wanaliona kama katiba IMEKUWA ni ya chama Fulani na Kwa matakwa Yao.

Kila mtu anataka katiba ifuate maoni yaliyokusanywa na tume ya jaji Warioba. Vyama vya siasa ni watanzania na wana wajibu wa kufuatilia jambo lolote watakalo, ili mradi hawavunji sheria. Usitegemee eti hivyo vyama vya siasa vitakaa kimya bila kuweka msukumo wa kupatikana kwa katiba mpya, kwa kusubiri wananchi waongelee. Kwa hii nchi yetu kila jambo lina watu wanaliwekea msukumo, kisha makundi mengine na wananchi kwa ujumla wanafuata.

Mimi ni mwananchi na ninaona sahihi vyama vya siasa kuweka msukumo kwenye upatikanaji wa katiba mpya. Sasa hao wananchi unaosema wameona ni zoezi la wanasiasa umekusanya wapi hayo maoni? Acha kuwa bendera fuata upepo, ukisikia viongozi wa ccm wanaongelea jambo fulani, na ww unalirukia ili kufanya upotoshaji wa kijinga.
 
Wanabodi,

Leo 30/12/2022 tunapoanza safari ya kuuaga mwaka 2022 hapo kesho na keshokutwa kuukaribisha mwaka mpya wa 2023 hivyo naomba nianze makala yangu hii ya "Kwa Maslahi ya Taifa" kwa kusema "kwaheri 2022, na Karibu 2023, kwa kuwatakia heri ya mwaka mpya 2023 in advance, kwa rai moja tuu, "Mwaka 2023, Tubadilike, Tufanye Kitu!"

Nimegundua sisi Watanzania, kwa jina letu maarufu la Wabongo ni watu wa maneno maneno mengi, kulalamika na na kulialia, lakini tukija kwenye matendo, Vitendo zero, sifuri, 0 nil!. Kwenye hili la Katiba, ni maneno maneno tuu, na kulia lia, ukiangalia matendo, ni hakuna kitu zaidi ya kelele!, makala ya leo ni ya swali, Jee na mwaka huu wa 2023, tuendeleze kulia lia kwa maneno maneno matupu au tubadilike tufanye vitendo, tufanye kitu, to do something, au tuendelee na maneno maneno na kulia lia tuu?.

Wengi huuanza mwaka mpya kwa kuweka malengo ya mwaka, “new year’s resolutions” kwamba mwaka huu nitafanya nini, ila katika kupanga hayo malengo, sii wengi hufanya mapitio ya mwaka ulioisha, walipanga kufanya nini, wametekeleza nini, wamefanikiwa nini na wamwkwama nini, ili baadhi yay ale malengo ya mwaka uliopita, ambayo hayakufanikiwa, yabebebwe katika mwaka unaofuata, au kama hayabebebi yafutwe, na sio kila mwaka unakuja na malengo mapya, mwisho wa mwaka hufanyi tathmini wala mapitio ya mwaka ulioisha, kisha unakuja na mengine mapya!, mwisho wa siku, unakuwa huwezi kupima mafanikio yako!.

Katiba ya nchi ndio Biblia ndio Msahafu wa uendeshaji wa nchi yetu. Kama ilivyo Ikulu ni mahali patakatifu, katiba ni kitabu kitakatifu kwa nchi yetu kama vilivyo vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu kwa Wakrusto na Quran Tukufu kwa Waislamu. Hii ndio sheria mama ya uendeshaji wa nchi yetu.

Tofauti pekee kati ya Biblia, Msahafu na Katiba, ni Msahafu haubadiliki, katiba inaweza kubadilishwa, ila mabadiliko yoyote ya katiba, lazima yawe ni mabadiliko halali ya haki.

Katiba ndio sheria kuu kuliko zote za nchi, viongozi wetu wakiisha chaguliwa, tunawaapisha kwa mujibu wa katiba, wanaapa kuilinda na kuitetea katiba ya JMT, na ikitokea hata rais wa JMT akikiuka katiba, anaondolewa madarakani!.

Sheria yoyote ikitungwa, ikiwa ni kinyume cha katiba, sheria hiyo inahesabika ni batili “null and void”, ikitungwa sheria ambayo ni batili, kwa kwenda kinyume cha katiba ya JMT, kisha ubatili huo, ukaja kuchomekewa ndani ya katiba yetu!, huku sasa tukuiteje?, maana kunakuwa sio kuibatilisha katiba, bali ni kuinajisi katiba!.

Mwaka 2022 tuliipigia kelele najisi fulani ndani ya katiba yetu kwa kulialia na kuisema sema, hivyo tumefika hadi mwisho wa mwaka 2022 bila jambo lolote la maana kufanyika kuiondoa najisi hii, sasa tumeingia mwaka mpya wa 2023, je na mwaka huu 2023, tuendelee tuu kupiga kelele kwa kulialia na kusema sema tuu, bila kufanya tendo lolote, au mwaka huu 2023, tubadilike, badala ya kulia lia na kusema sema, twende hatua moja zaidi mbele kwa kutenda kitu? ( msiwe na wasiwasi kuhusu kutenda huku, sio kwa mikutano ya hadhara au kufanya maandamano, ni kutenda kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni).
Maneno Maneno Yangu Kuhusu Najisi Kwenye Katiba Yetu ya 1977
  1. Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli
  2. Asante Mungu kwa Rais Samia: Ni Msema Kweli na Mtenda Kweli, Ni Msema Haki na Mtenda Haki. Je, Ataruhusu Ubatili Huu Kuendelea Ndani ya Katiba Yetu?
  3. Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
  4. Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
  5. Haki Huinua Taifa! Rais Samia kwa Kauli na Matendo ameonesha ni mtu wa Haki. Akitekeleza hili kama alivyosema, atabarikiwa, Tanzania itabarikiwa
  6. Samia Mpango wa Mungu kwa Tanzania: Kwa Hili, Atabarikiwa!, Taifa Litabarikiwa!. Asante Mungu kwa Samia, Mungu Mbariki Samia, Mungu Ibariki Tanzania
  7. Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law! Kuendelea Kuitumia ni Ujinga? Kuwabebesha Masikini Gharama za Uchaguzi ni Dhambi!
  8. Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
  9. Mgombea Kudhaminiwa na Chama ni Ubatili Uliochomekwa Kiubatili na Bunge Letu Ndani ya Katiba Yetu!. Tuache Ubatili Huu Uendelee Ndani ya Katiba Yetu?
  10. Hukumu ya Mgombea Binafsi Juni 17, 2010
  11. "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza
  12. Trends, Visions: Watanzania msitatizwe na kauli zake kuhusu Katiba, baada ya Nyerere, ni Magufuli ndiye ataacha legacy kubwa ikiwemo Katiba Mpya!. kwa vile Rais Samia ameisha jitanabaisha yeye ni kama Magufuli, hivyo anapaswa kulitimiza na hili!.
Sisi Watanzania tuna fani mbalimbali, kuna wenzetu kazi yao ni kufikiri na kupanga mikakati, hawa wanaitwa think tanks, kuna wenzetu ni viongozi, kazi yao ni kutuongoza, kuna wenzetu ni watendakazi, kazi yao ni kutenda kazi kwa kutumia nguvu zao, kuna wengine tukiwemo sisi waandishi wa habari na vyombo vya habari, wa kiasili, yaani “traditional media” kazi zetu kuu ni tatu, kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha, hatuna kutenda!. Na tumegawanyika makundi mawili, waandishi wa habari watangazaji na vyombo vya utangazaji (broadcast media) ambao kazi yao ni kutangaza na kuongea tuu, hakuna kutenda lolote!, na waandishi wa habari wa magazeti (print media) ambao kazi yao ni kuandika tuu hakuna kutenda lolote!.

Lakini ujio wa mapinduzi ya kidigitali kwenye dunia yetu na ujio wa mitandao ya kijamii, haya makundi mawili ya vyombo vya habari, yaani broadcast media na print media, yameunganishwa na mtandao wa jamii, hivyo kule kwenye mtandao, hakuna print peke yake wala broadcast peke yake. Vyombo vya utangazaji vina kurasa zake za mitandao ya kijamii navyo sasa vinaandika, mtu unaweza kusoma, vyombo vya print, kama magazeti, navyo kwenye kurasa zake, vinatangaza, na kuweka magazeti mtandao, hivyo siku hizi, kupata habari, kuangalia TV au kusoma gazeti, sio lazima ukae nyumbani uwashe TV uangalie habari, ukijisajili tuu na mtandao fulani, wanaita ku subscribe, unaletewa tuu habari, kila inapotokea, hivyo mtu hana tena haja kusubiria taarifa ya habari saa mbili usiku, kila tukio linapotokea linatangazwa live, hivyo kufikia ule muda wa habari, kila kilichotokea, watu wanakijua, magazeti ya kesho yake, sisi tunayasoma leo, maana kwenye kurasa zao za mitandao, kila habari, inachapishwa pale pale inapotokea.

Ujio huu wa mitandao ya jamii, umemfanya sasa kila mtu kuwa ni mwandishi wa habari, kila mtu sasa ni mtangazaji, hali inayopelekea hata sisi ambao ni watangazaji wa kweli wa kusomea hii kazi, kujikuta hatufui dafu mbele ya watangazaji vijana wa kisasa kwenye mitandao ya jamii, hivyo ukiwauliza vijana wa kisasa, unamjua Pasco Mayalla?, atakuuliza, Pascal Mayalla ndio nani?, utamwambia ni mtangazaji maarufu wa kipindi cha Kiti Moto, atakuuliza kiti moto ndio nini?, naomba link yake ni kitazame nikivutiwa, nita subscribe, unajikuta huna cha kumwambia!, hivyo sisi waandishi wakongwe wa ki analojia, ili tuendelee kuwepo ni lazima tubadilike na kwenda kidigitali vinginevyo tunafutika jumla!, hivyo mwaka 2023, Pasco Mayalla nae anakuja kidigitali zaidi!.

Hivyo kwa vile mimi kazi yangu ni kuandika tuu na kutangaza, nikikaa chini na kuutafakari mwaka 2022, nimeandika mangapi na kutangaza mangapi, kuhusu katiba na yapi yamefanyiwa kazi, nimejikuta kwa mwaka huu 2023, ili kuisaidia jamii, na kulisaidia taifa, nisiishie kuandika tuu, na kutangaza tuu, ninapaswa nifanye kitu cha ziada kwa kwenda mbele zaidi kidigitali zaidi na kufanya jambo la kuandika tuu na kutangaza tuu, I must do something more!. Hii something more ni nini?, naomba kwa sasa nisiseme, but watch me!.

Ndipo yale maneno ya rais kijana wa Marekani, John F. Kennedy aliyowaeleza Wamarekani, “usijiulize Marekani imekufanyia nini, jiulize umeifanyia nini Marekani?”. Hivyo tunapoukaribisha mwaka mpya, wa 2023, kama kila mmoja wetu atajitafakari kwa kujiuliza “jee ameifanyia nini Tanzania” akijikuta hajaifanyia kitu chochote cha maana huko nyuma, basi mwaka huu wa 2023, abadilike kwa kupanga malengo yenye mipango mkakati kwa kujiuliza, “jee ataifanyia nini Tanzania?”, Inawezekana kama kila mtu atatimiza wajibu wake kikamilifu,

Mwaka huu wa 2023, tupunguze maneno, kuongea sana, tupunguze maandishi kuandika sana, hayo maneno tunayoongea sana, badaya ya kuishia kuongea tuu, na kuandika tuu, tufanye na vitendo, tutende,!. Hivyo jambo langu kuu la kwanza kwa mwaka huu 2023 ni Katiba!. Japo kuna mambo mengi muhimu ya kuyashughulikia, lakini kwangu mimi kwa mwaka huu, naona muhimu kuliko yote ni la Katiba!, kwenye hili la Katiba, sasa tufanye kitu, tusiishie kuongea tuu na kuandika tuu, tufanye kitu cha ziada!, jee tufanye nini?, ungana nami wiki ijayo, nikiianzisha safari ya Katiba!, “it can be done, play your part” .
Kwa heri 2022, karibu 2023
Happy New Year!, Heri ya Mwaka Mpya!.
Paskali.
Umenena sana lakini kikwazo kikubwa cha Tanzania na waBongo wenyewe. Wanaotuongoza ni waongo na wanafuki sio DC sio mkuu wa Mkoa, sio mbunge na hata Waziri! Wanazuga kila kukicha ili kulinda maslahi yao, Hawa ndio CCM walaji Wakuu!
Akitokea mwenye kusema ukweli anaambiwa hafai na amesaliti chama.
Hivi chama ni wao au ni waTanzania!
KATIBA mpya halikwepeki ni jambo endelevu japo Kuna madilu wanaona ni sakata.
Kwaheri 22 na karibu 23.
 
Wanabodi,

Leo 30/12/2022 tunapoanza safari ya kuuaga mwaka 2022 hapo kesho na keshokutwa kuukaribisha mwaka mpya wa 2023 hivyo naomba nianze makala yangu hii ya "Kwa Maslahi ya Taifa" kwa kusema "kwaheri 2022, na Karibu 2023, kwa kuwatakia heri ya mwaka mpya 2023 in advance, kwa rai moja tuu, "Mwaka 2023, Tubadilike, Tufanye Kitu!"

Nimegundua sisi Watanzania, kwa jina letu maarufu la Wabongo ni watu wa maneno maneno mengi, kulalamika na na kulialia, lakini tukija kwenye matendo, Vitendo zero, sifuri, 0 nil!. Kwenye hili la Katiba, ni maneno maneno tuu, na kulia lia, ukiangalia matendo, ni hakuna kitu zaidi ya kelele!, makala ya leo ni ya swali, Jee na mwaka huu wa 2023, tuendeleze kulia lia kwa maneno maneno matupu au tubadilike tufanye vitendo, tufanye kitu, to do something, au tuendelee na maneno maneno na kulia lia tuu?.

Wengi huuanza mwaka mpya kwa kuweka malengo ya mwaka, “new year’s resolutions” kwamba mwaka huu nitafanya nini, ila katika kupanga hayo malengo, sii wengi hufanya mapitio ya mwaka ulioisha, walipanga kufanya nini, wametekeleza nini, wamefanikiwa nini na wamwkwama nini, ili baadhi yay ale malengo ya mwaka uliopita, ambayo hayakufanikiwa, yabebebwe katika mwaka unaofuata, au kama hayabebebi yafutwe, na sio kila mwaka unakuja na malengo mapya, mwisho wa mwaka hufanyi tathmini wala mapitio ya mwaka ulioisha, kisha unakuja na mengine mapya!, mwisho wa siku, unakuwa huwezi kupima mafanikio yako!.

Katiba ya nchi ndio Biblia ndio Msahafu wa uendeshaji wa nchi yetu. Kama ilivyo Ikulu ni mahali patakatifu, katiba ni kitabu kitakatifu kwa nchi yetu kama vilivyo vitabu vitakatifu vya Biblia Takatifu kwa Wakrusto na Quran Tukufu kwa Waislamu. Hii ndio sheria mama ya uendeshaji wa nchi yetu.

Tofauti pekee kati ya Biblia, Msahafu na Katiba, ni Msahafu haubadiliki, katiba inaweza kubadilishwa, ila mabadiliko yoyote ya katiba, lazima yawe ni mabadiliko halali ya haki.

Katiba ndio sheria kuu kuliko zote za nchi, viongozi wetu wakiisha chaguliwa, tunawaapisha kwa mujibu wa katiba, wanaapa kuilinda na kuitetea katiba ya JMT, na ikitokea hata rais wa JMT akikiuka katiba, anaondolewa madarakani!.

Sheria yoyote ikitungwa, ikiwa ni kinyume cha katiba, sheria hiyo inahesabika ni batili “null and void”, ikitungwa sheria ambayo ni batili, kwa kwenda kinyume cha katiba ya JMT, kisha ubatili huo, ukaja kuchomekewa ndani ya katiba yetu!, huku sasa tukuiteje?, maana kunakuwa sio kuibatilisha katiba, bali ni kuinajisi katiba!.

Mwaka 2022 tuliipigia kelele najisi fulani ndani ya katiba yetu kwa kulialia na kuisema sema, hivyo tumefika hadi mwisho wa mwaka 2022 bila jambo lolote la maana kufanyika kuiondoa najisi hii, sasa tumeingia mwaka mpya wa 2023, je na mwaka huu 2023, tuendelee tuu kupiga kelele kwa kulialia na kusema sema tuu, bila kufanya tendo lolote, au mwaka huu 2023, tubadilike, badala ya kulia lia na kusema sema, twende hatua moja zaidi mbele kwa kutenda kitu? ( msiwe na wasiwasi kuhusu kutenda huku, sio kwa mikutano ya hadhara au kufanya maandamano, ni kutenda kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni).
Maneno Maneno Yangu Kuhusu Najisi Kwenye Katiba Yetu ya 1977
  1. Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli
  2. Asante Mungu kwa Rais Samia: Ni Msema Kweli na Mtenda Kweli, Ni Msema Haki na Mtenda Haki. Je, Ataruhusu Ubatili Huu Kuendelea Ndani ya Katiba Yetu?
  3. Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
  4. Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
  5. Haki Huinua Taifa! Rais Samia kwa Kauli na Matendo ameonesha ni mtu wa Haki. Akitekeleza hili kama alivyosema, atabarikiwa, Tanzania itabarikiwa
  6. Samia Mpango wa Mungu kwa Tanzania: Kwa Hili, Atabarikiwa!, Taifa Litabarikiwa!. Asante Mungu kwa Samia, Mungu Mbariki Samia, Mungu Ibariki Tanzania
  7. Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law! Kuendelea Kuitumia ni Ujinga? Kuwabebesha Masikini Gharama za Uchaguzi ni Dhambi!
  8. Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
  9. Mgombea Kudhaminiwa na Chama ni Ubatili Uliochomekwa Kiubatili na Bunge Letu Ndani ya Katiba Yetu!. Tuache Ubatili Huu Uendelee Ndani ya Katiba Yetu?
  10. Hukumu ya Mgombea Binafsi Juni 17, 2010
  11. "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza
  12. Trends, Visions: Watanzania msitatizwe na kauli zake kuhusu Katiba, baada ya Nyerere, ni Magufuli ndiye ataacha legacy kubwa ikiwemo Katiba Mpya!. kwa vile Rais Samia ameisha jitanabaisha yeye ni kama Magufuli, hivyo anapaswa kulitimiza na hili!.
Sisi Watanzania tuna fani mbalimbali, kuna wenzetu kazi yao ni kufikiri na kupanga mikakati, hawa wanaitwa think tanks, kuna wenzetu ni viongozi, kazi yao ni kutuongoza, kuna wenzetu ni watendakazi, kazi yao ni kutenda kazi kwa kutumia nguvu zao, kuna wengine tukiwemo sisi waandishi wa habari na vyombo vya habari, wa kiasili, yaani “traditional media” kazi zetu kuu ni tatu, kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha, hatuna kutenda!. Na tumegawanyika makundi mawili, waandishi wa habari watangazaji na vyombo vya utangazaji (broadcast media) ambao kazi yao ni kutangaza na kuongea tuu, hakuna kutenda lolote!, na waandishi wa habari wa magazeti (print media) ambao kazi yao ni kuandika tuu hakuna kutenda lolote!.

Lakini ujio wa mapinduzi ya kidigitali kwenye dunia yetu na ujio wa mitandao ya kijamii, haya makundi mawili ya vyombo vya habari, yaani broadcast media na print media, yameunganishwa na mtandao wa jamii, hivyo kule kwenye mtandao, hakuna print peke yake wala broadcast peke yake. Vyombo vya utangazaji vina kurasa zake za mitandao ya kijamii navyo sasa vinaandika, mtu unaweza kusoma, vyombo vya print, kama magazeti, navyo kwenye kurasa zake, vinatangaza, na kuweka magazeti mtandao, hivyo siku hizi, kupata habari, kuangalia TV au kusoma gazeti, sio lazima ukae nyumbani uwashe TV uangalie habari, ukijisajili tuu na mtandao fulani, wanaita ku subscribe, unaletewa tuu habari, kila inapotokea, hivyo mtu hana tena haja kusubiria taarifa ya habari saa mbili usiku, kila tukio linapotokea linatangazwa live, hivyo kufikia ule muda wa habari, kila kilichotokea, watu wanakijua, magazeti ya kesho yake, sisi tunayasoma leo, maana kwenye kurasa zao za mitandao, kila habari, inachapishwa pale pale inapotokea.

Ujio huu wa mitandao ya jamii, umemfanya sasa kila mtu kuwa ni mwandishi wa habari, kila mtu sasa ni mtangazaji, hali inayopelekea hata sisi ambao ni watangazaji wa kweli wa kusomea hii kazi, kujikuta hatufui dafu mbele ya watangazaji vijana wa kisasa kwenye mitandao ya jamii, hivyo ukiwauliza vijana wa kisasa, unamjua Pasco Mayalla?, atakuuliza, Pascal Mayalla ndio nani?, utamwambia ni mtangazaji maarufu wa kipindi cha Kiti Moto, atakuuliza kiti moto ndio nini?, naomba link yake ni kitazame nikivutiwa, nita subscribe, unajikuta huna cha kumwambia!, hivyo sisi waandishi wakongwe wa ki analojia, ili tuendelee kuwepo ni lazima tubadilike na kwenda kidigitali vinginevyo tunafutika jumla!, hivyo mwaka 2023, Pasco Mayalla nae anakuja kidigitali zaidi!.

Hivyo kwa vile mimi kazi yangu ni kuandika tuu na kutangaza, nikikaa chini na kuutafakari mwaka 2022, nimeandika mangapi na kutangaza mangapi, kuhusu katiba na yapi yamefanyiwa kazi, nimejikuta kwa mwaka huu 2023, ili kuisaidia jamii, na kulisaidia taifa, nisiishie kuandika tuu, na kutangaza tuu, ninapaswa nifanye kitu cha ziada kwa kwenda mbele zaidi kidigitali zaidi na kufanya jambo la kuandika tuu na kutangaza tuu, I must do something more!. Hii something more ni nini?, naomba kwa sasa nisiseme, but watch me!.

Ndipo yale maneno ya rais kijana wa Marekani, John F. Kennedy aliyowaeleza Wamarekani, “usijiulize Marekani imekufanyia nini, jiulize umeifanyia nini Marekani?”. Hivyo tunapoukaribisha mwaka mpya, wa 2023, kama kila mmoja wetu atajitafakari kwa kujiuliza “jee ameifanyia nini Tanzania” akijikuta hajaifanyia kitu chochote cha maana huko nyuma, basi mwaka huu wa 2023, abadilike kwa kupanga malengo yenye mipango mkakati kwa kujiuliza, “jee ataifanyia nini Tanzania?”, Inawezekana kama kila mtu atatimiza wajibu wake kikamilifu,

Mwaka huu wa 2023, tupunguze maneno, kuongea sana, tupunguze maandishi kuandika sana, hayo maneno tunayoongea sana, badaya ya kuishia kuongea tuu, na kuandika tuu, tufanye na vitendo, tutende,!. Hivyo jambo langu kuu la kwanza kwa mwaka huu 2023 ni Katiba!. Japo kuna mambo mengi muhimu ya kuyashughulikia, lakini kwangu mimi kwa mwaka huu, naona muhimu kuliko yote ni la Katiba!, kwenye hili la Katiba, sasa tufanye kitu, tusiishie kuongea tuu na kuandika tuu, tufanye kitu cha ziada!, jee tufanye nini?, ungana nami wiki ijayo, nikiianzisha safari ya Katiba!, “it can be done, play your part” .
Kwa heri 2022, karibu 2023
Happy New Year!, Heri ya Mwaka Mpya!.
Paskali.


P,

Mimi kwa mawazo yangu waandishi wa habari inabidi wawe wazalendo. Tusiko kuwa makini katiba itabaki kuonekana ni kwa manufaa ya Chadema badala ya manufaa ya taifa. Hivyo nyie waandishi wa habari mnatakiwa kuongea umuhimu wa katiba mpya bila kuweka siasa na mbele ya vyombo vyote na sio mitandao halafu kwenye tv unabadilika.
 
Kila mtu anataka katiba ifuate maoni yaliyokusanywa na tume ya jaji Warioba. Vyama vya siasa ni watanzania na wana wajibu wa kufuatilia jambo lolote watakalo, ili mradi hawavunji sheria. Usitegemee eti hivyo vyama vya siasa vitakaa kimya bila kuweka msukumo wa kupatikana kwa katiba mpya, kwa kusubiri wananchi waongelee. Kwa hii nchi yetu kila jambo lina watu wanaliwekea msukumo, kisha makundi mengine na wananchi kwa ujumla wanafuata.

Mimi ni mwananchi na ninaona sahihi vyama vya siasa kuweka msukumo kwenye upatikanaji wa katiba mpya. Sasa hao wananchi unaosema wameona ni zoezi la wanasiasa umekusanya wapi hayo maoni? Acha kuwa bendera fuata upepo, ukisikia viongozi wa ccm wanaongelea jambo fulani, na ww unalirukia ili kufanya upotoshaji wa kijinga.
Sema wewe ni chadema Tena mwenye t.shirt ya chama chako na maandishi ya katiba MPYA ni Sasa. Nyinyi daini katiba ya chama chenu. Katiba ya wananchi itatafutwa na wananchi wasio na chama chochote.
 
Haya yote ni sawa lakini vyama tawala Afrika ni vichache vilivyoandika katiba mpya kwa amani au kuruhusu demokrasia ya uchaguzi ya kweli kwenye nchi zao ndio msingi wa mtoa hoja baada ya utafiti na hata CCM wanavojivuta kuandika katiba mpya utaona dalili zilezile za kutaka kuharibu amani ya nchi, wanasingizia wanajenga uchumi lakini kimsingi hawajengi uchumi wowote wa nchi maana Taifa bado maskini na halina uelekeo wa kujikomboa maana tumekua tegemezi toka uhuru hadi leo tunaendelea kutegemea ajabu sana ,
Unaelekea ninapodhan ndo option pekee iliyobaka yaan confrotation. Ajab hukuhitimisha tuanzie wapi!
Mpaka sasa kazi inazid kuwa ngumu kwa sabab ushost wa mkandamizaj, ccm, na wenye dunia uko vizur tunabak kujipambania bila external force.
Mbaya zaid kwa sasa hatuna hata kiongoz mwenye dhati wa kutanguliza mbele. Tuliacha kuwaunga mkono kwa wakat muafaka sasa wameamua nao kususa na kukaa na mtesi wa wananchi katika meza ya maakuli. Bila wanasiasa zoez hili ni gumu.
Mwisho, ni HATUJACHELEWA. Ilimrad tukubali kumwaga damu.
 
Waambie wananchi Ukweli.
Waambie Wananchi kuwa hatuwezi kuandika Katiba mpya bila Ridhaa ya Mkuu wa Jumuiya ya Madola....Na ndio maana nashikilia kidete Tuondoke katika Jumuiya hiyo.

Tuambiane ukweli badala ya kujivua nguo na kutokujieshimu kwa kuitana hatuna Akili, kuwa mambo yetu ni Zero! Inauma iwe kweli au la.

We must, change our mindset.

Kuandika au Kubadilisha Katiba kunahitajika kufanya Maamuzi magumu bila kutetereka. Vishinikizo haviko hapa kwetu vipo nje. Mabakuli yanatusumbua.

Amani-Heri ya Mwaka Mpya Inshallah.
 
Nilishalisema hili lakn kwa kuwa ss ni watanzani hakuna wa kubadilika. Acha tuendelee na tuachokijua ~kulalamika~
 
Sema wewe ni chadema Tena mwenye t.shirt ya chama chako na maandishi ya katiba MPYA ni Sasa. Nyinyi daini katiba ya chama chenu. Katiba ya wananchi itatafutwa na wananchi wasio na chama chochote.

Hao wananchi wataanza lini kuidai hiyo katiba mpya? Ama hao cdm sio wananchi? Kama CDM wameamua kuidai wataendelea kuidai, na hawamzuii mwananchi yoyote kuidai.
 
Duh! Bro kama unajisahaulisha hivi? Hivi kwani wewe umeshalia au kujiliza mara ngapi humu jukwaani? Achilia mbali kulia na kupiga ukunga kuleee kwenye Mnavu na Mchicha.
 
Huu ni uchochezi!. Katiba mpya inaweza kupatikana kwa
1. Dialogue- kwa njia ya mazungumzo na kufikia consensus
2. Inaweza kupatikana kwa njia ya lobbying and advocacy
3. Inaweza kupatikana kwa pressure groups to press on issues
4. Inaweza kupatikana kwa confrontations
P
Uligombea Kawe, ukapigwa chini, ukogombea East Africa, ukapigwa chini, Hapa JF wakakushindanisha kwenye jukwaa la siasa ukapigwa chini. Unajua sababu? Sababu ni kwamba wewe ni pangu pakavu tia mchuzi. Huna msimamo, huaminiki, unaweka tumbo mbele na mishipa ya aibu ilishakatika.
 
Uligombea Kawe, ukapigwa chini,
Ni kweli, niligombea na kitu cha kwanza ni kuleta sababu za kugombea, , niligombea
nilizidiwa sifa na niliogombea nao, nikakubali matokeo na humu JF nikayaleta Uchaguzi 2020 - Wana JF, nipeni Pole. Msinicheke wala msinibeze; nimegombea ubunge Kawe kupitia CCM nimeambulia kura 1. Ama kweli CCM ina wenyewe!
ukogombea East Africa, ukapigwa chini,
Ni kweli, kabla ya kugombea EALA pia militia sababu, Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo nikagombea, nikazidiwa sifa nimeshindwa na kukubali matokeo EALA: Waliopitishwa CCM, ni Kwa Haki!, Tulioachwa ni kwa Haki, Tumezidiwa Vigezo!. Thanks4 for Support, Nimekubali Matokeo Kiroho Safi! Kazi Iendelee!
Hapa JF wakakushindanisha kwenye jukwaa la siasa ukapigwa chini.
Pia ni kweli, nako pia nimezidiwa vigezo nikashindwa!.
Unajua sababu? Sababu ni kwamba wewe ni pangu pakavu tia mchuzi. Huna msimamo, huaminiki, unaweka tumbo mbele na mishipa ya aibu ilishakatika.
Hili pia ni kweli, Luna vitu mtu unapewa kabla hujazaliwa na vingine baada ya kuzaliwa, aibu ni kitu kinachotolewa baada ya kuzaliwa, hivyo nilipozaliwa ilipofika wakati wangu wa kuzaliwa mgao wa aibu, ikatokea bahati mbaya, Sikh hiyo tulikuwa wengi zaidi ya aibu zilizokuwepo hivyo wenzetu waliobahatika wakapata mgao wao, sisi tusio na bahati tukakosa mgao!.

P
 
Tatizo katiba mpya wameachiwa wachache kana kwamba hilo lawahusu wao! NB: next year uwe mstari wa mbele kupigania katiba!!

IMG_4321.jpg
 
Back
Top Bottom