Watanzania ni Wakarimu, Nitarudi Tena ' - Busta Rhymes

Watanzania ni Wakarimu, Nitarudi Tena ' - Busta Rhymes

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363


3606326.jpg

Busta Rhymes akichengua wabongo kwenye Fiesta Tuesday, November 24, 2009 8:00 AM
MSANII mkongwe wa Hip Hop kutoka Marekani, Busta Rhymes amesema kuwa ameridhishwa na ukarimu wa Watanzania hali inayomfanya afikirie kuitangaza Tanzania kwa wasanii wenzake wa nje kuja nchini. MSANII mkongwe wa Hip Hop kutoka Marekani, Busta Rhymes amesema kuwa ameridhishwa na ukarimu wa Watanzania hali inayomfanya afikirie kuitangaza Tanzania kwa wasanii wenzake wa nje kuja nchini.

Busta Rhymes alikuwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mwaliko wa kuwa moja ya wasanii wa kutumbuiza katika tamasha la Fiesta la mwaka huu lililofanyika jumamosi katika viwanja vya Chuo cha Posta.

Mara baada ya kupanda jukwaani na kutakiwa azungumze kidogo, Mwanahip hop huyo maarufu duniani alisema "Sikutegemea kuwa Watanzania wanapenda muziki, ni wakarimu, na hii inanifanya niwakumbuke zaidi na zaidi nikirejea Marekani".

Alisema, atafanya kila analoliweza kuitangaza Tanzania kimuziki, na hata kuwavutia wanamuziki wenzake wakubwa, wakiwemo 50 Cent na Jay Z kuja kwa ajili ya onyesho, ikiwezekana katika onyesho lijalo la Fiesta.

Licha ya msanii huyo kuchelewa kupanda jukwaani, aliweza kutumbuiza zaidi ya saa moja huku akiwa na wasaidizi wake na kuufanya umati uliofika hapo kumshangilia kwa nguvu.

Busta alishangiliwa zaidi pale alipoimba vibao vyake ambavyo vimezoeleka katika masikio ya wapenda muziki kama `Make it Clap` na `Arab money'.

Mbali na nyota huyo kutoka Marekani, onyesho hilo pia lilipambwa na wasanii mbalimbali wa hapa nchini.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3606326&&Cat=8
 
He..this is a NEWS to me!
Watanzania ni Wakarimu, not because he got all his due in full?
 
Sijawahi kusikia mtu kaenda ugenini kisha akasema hapa ni pabaya sana na nyie ni wakatili kabisa sirudi ng'oooo
 
Nenda Somalia au Afghanistan ndio utajua kama upasifie wakarimu au la.

wee mwanangu usimshauri mtu hivyo atafariki bure....

Ila mwisho wa siku kweli bado waTZ ni wakarimu sana...Nchi nyingine hata

kumpa hi mtu barabarani ni isue, hata kuongea na mtu kwenye daladala sio

kawaida yani mnaanza safari mpaka mwisho kama mabubu, hata kitendo

cha kusimama kwenye daladala ili kumpisha mtu mzima anapoingia ni nadra

sana kutokea nchi nyingine, hata kitendo cha watu kuudhuria msiba na

kufil kama sehemu ya yale matatizo

watusaidie waliotembea nchi nyingi.
 
Kwa kweli huwezi kwenda mahali ukasema eti nyie wabaya na sirudi tena hiyo ni fact, ingawa moyoni anajua ukweli! Nadhani dada zetu walimkarimu pia....nakumbuka Etoo, alitamani kutorudi Barcelona!
 
Sijawahi kusikia mtu kaenda ugenini kisha akasema hapa ni pabaya sana na nyie ni wakatili kabisa sirudi ng'oooo
Nimeipenda hii,lakini niliwahi sikia kuwa kuna kipindi ze late Wacko Jacko alikuja bongo na kudai kuwa eti bongo kunastink,ikamlead kutembea na mask mpaka mwisho wa dhiara yake!!
 
Salam.

Watanzania ni wakarimu kwa wageni, mgeni akija unampa vilivyo bora, wenyeji mnabakia kula, au kulala kwenye sehemu zisizo bora, mtamchinja kuku hata kama ndiye aliyebakia kuwa wa mbegu. Pia hatuna tabia ya kuwaeleza wageni wanaotuudhi kuwa wametuudhi. Niliwahi kuwa na urafiki na wanaafrika mashariki wengine, walikuwa wanadhani kuwa Watanzania ni wanafiki kwa kuwa tunavumilia sana kuudhiwa na watu wengine.

Kwa maoni yangu huu ''ukarimu'' umetusababishia kutawaliwa na wakoloni wa zamani na hata wa mamboleo. How can you explain a chinese Konda? ( mgonga debe kwenye daladala) We do not have the guts to say he he he do not do the kind of jobs that can be done by our youth. If you are a foreigner please do the jobs that we are not yet able to do like the technical stuff.
 
Huyu jamaa milele ntamkumbuka na huu wimbo wake hapa chini. Umekaa ki-ajabu sana ila ndiyo ulimfanya ATESE dunia nzima na kuwa anafahamika. Pia ni moja ya watu walioanza kutumia Video Camera with FISH-EYE LENS.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=AiVpSSkwPU4&feature=related[/ame]
 
kwa maoni yangu huu ''ukarimu'' umetusababishia kutawaliwa na wakoloni wa zamani na hata wa mamboleo. How can you explain a chinese Konda? ( mgonga debe kwenye daladala) We do not have the guts to say he he he do not do the kind of jobs that can be done by our youth. If you are a foreigner please do the jobs that we are not yet able to do like the technical stuff.
Hapo mzee umenena pointi
 
Akienda kenya atasema hivyo hivyo , akienda Uganda atasema hivyo hivyo kote akienda atasema Nchi nzuri , wakarimu na wanawake wao wazuri .
Sehemu yeyote ukiwa mgeni unakarimiwa bwana . Nakumbuka mara ya kwanza nafika USA , kila jirani kwenye neighborhood yetu alikuja kutukaribisha kwa kutuletea matunda na mazagazaga kibao nikasema kumbe wazungu ni wakarimu .Ngoja huyu Busta ange haribikiwa gari mtaani halafu aone wabongo wangemsachi kinamna gani .

Michael Jackson hakusema kua Bongo inanuka, ila alivaa ile surgical mask ambayo ilifanya watu wadhani kua anaona harufu mbaya .

Kiukweli ni kwamba Kulikua kunanuka shombo ya samaki kutoka ferry maana ilikua maeneo ya Kilimanjaro hotel , Kama una bisha hakunukio nenda Kempinsky level 8 toka kwa nje pale halafu sikilizia hiyo shombo.

Halafu hawa clouds mbona sijaona nani kashinda gari? au ilikua longo longongo?
 
Kwa kweli huwezi kwenda mahali ukasema eti nyie wabaya na sirudi tena hiyo ni fact, ingawa moyoni anajua ukweli! Nadhani dada zetu walimkarimu pia....nakumbuka Etoo, alitamani kutorudi Barcelona!

kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi olalalalalala
Ila ni ahah haha haha haha aha aha aha ah
Aisee wapunguze
 
Sijawahi kusikia mtu kaenda ugenini kisha akasema hapa ni pabaya sana na nyie ni wakatili kabisa sirudi ng'oooo
Wengine husema kwa matendo, kama yule aliyeshika pua yake mara baada ya kutua JK N international airport
 
Hana lolote ameshakuwa played out anafurahia mshiko aliolipwa.
 
Akienda kenya atasema hivyo hivyo , akienda Uganda atasema hivyo hivyo kote akienda atasema Nchi nzuri , wakarimu na wanawake wao wazuri .
Sehemu yeyote ukiwa mgeni unakarimiwa bwana . Nakumbuka mara ya kwanza nafika USA , kila jirani kwenye neighborhood yetu alikuja kutukaribisha kwa kutuletea matunda na mazagazaga kibao nikasema kumbe wazungu ni wakarimu .Ngoja huyu Busta ange haribikiwa gari mtaani halafu aone wabongo wangemsachi kinamna gani .

Michael Jackson hakusema kua Bongo inanuka, ila alivaa ile surgical mask ambayo ilifanya watu wadhani kua anaona harufu mbaya .

Kiukweli ni kwamba Kulikua kunanuka shombo ya samaki kutoka ferry maana ilikua maeneo ya Kilimanjaro hotel , Kama una bisha hakunukio nenda Kempinsky level 8 toka kwa nje pale halafu sikilizia hiyo shombo.

Halafu hawa clouds mbona sijaona nani kashinda gari? au ilikua longo longongo?

Mkuu hayo mapokezi ya shangwe na vigeregere ni Marekani hii hii au South America? State gani hiyo na wengine waende japo kutembea!
 
huyu kaonjeshwa milupo ya CORNER BAR anatoa ukarimu kwa watanzania wote tungempeleka GARDEN BISTOL Si angeomba na uraia kabisa..ngozi za bongo noma
 
Labda woooooote mliopinga hapo juu mlitaka labda mchizi asemeje? Sisi kwa kukosoa hata angesema chochote tungelalamika tu, nafikiri duniani sisi ndio tunaongoza kwa kulalamika.
 
Back
Top Bottom