Watanzania ni watu wa kuchekesha sana - wakati wa bajeti hizi nchi tunaziita washiriki wetu wa maendeleo, wakitukosoa na kushauri tunawaita mabeberu!

Watanzania ni watu wa kuchekesha sana - wakati wa bajeti hizi nchi tunaziita washiriki wetu wa maendeleo, wakitukosoa na kushauri tunawaita mabeberu!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Lazima kuna kitu hakiko sawa akilini mwa viongozi wetu na mashabiki wengi wa siasa wasio na uwezo mkubwa wa kufikiri kwa makini. Leo nasoma bajeti ya serikali, nakutana na maneno kwamba bajeti yetu pia itategemea msaada kutoka kwa washiriki wetu wa maendeleo (development partners).

Sasa mimi nimeona huku ni kuwa wanafiki sana. Ikiwa tunaziona hizi nchi na taasisi za kimataifa kuwa washiriki wetu wa maendeleo, kwamba wanatujali kiasi cha kutoa fedha zao ili kuchangia maendeleo yetu, kwa nini pale ambapo wanatukosoa na kutushauri tunawaita mabeberu? Kama huu sio ulevi na wendawazimu wa kisiasa ni nini basi?

Mtu ambaye anakusaidia katika mambo ya msingi ya maendeleo, ni wazi kuwa kwa kiasi fulani anakuwa na uhalali wa kukushauri au kukukosoa pale ambapo anaona unakosea. Kuna usemi kwamba usiume mkono unaokulisha (dont bite the hand that feeds you), kwa nini viongozi wetu wanakuwa wepesi sana wa kusahau hili wanapokuwa kwenye majukwaa ya kisiasa na kutaka kujiongezea umaarufu kwa kuropoka maneno "mabeberu"?

Hatusemi kwamba tunapaswa kuuza uhuru wetu kwa nchi tajiri au taasisi za kimataifa ambazo ni "washiriki wetu wa maendeleo". Bali twapaswa kuwa waungwana kiasi kwamba hata pale tunapokosolewa au kushauriwa na hatupendi, basi tujue jinsi ya kujibu kistaarabu. La sivyo sisi na viongozi wetu tunajionyesha kuwa wanafiki tu! Ningependa kuona hili linazingatiwa kwanza na Rais Magufuli na wengine watafuata.
 
Tusijisahalishe hizo ni tabia za Watanzania walio wengi, tunapenda kujisifia ata ujinga kukosolewa kwetu mwiko, tabia ya Viongozi wetu ni uthibitisho.
 
Yes, wakitusaidia ni nchi rafiki, nchi wahisani, nchi wafadhili, ni development partners, ila wakitukosoa sasa ndio wanakuwa mabeberu.
P
 
Wakoloni ni wakoloni tu, misaada yao ni ya kinafiki tu.
 
Yes, wakitusaidia ni nchi rafiki, nchi wahisani, nchi wafadhili, ni development partners, ila wakitukosoa sasa ndio wanakuwa mabeberu
P
Kweli Mkuu Pascal. Tatizo ni kwamba viongozi wa Tanzania wana serious deficiency ya diplomatic maturity. Wanakuwa kama viranja wa shule za msingi.

Only in Tanzania tuna mabeberu ambao pia ni wahisani, wafadhiri, washiriki wa maendeleo, nchi rafiki!
 
Wakoloni ni wakoloni tu, misaada yao ni ya kinafiki tu.
Kama mmegundua hilo kwa nini mnawaomba misaada? Kwani wao ndio wanaomba kutupa misaada? Unaona misaada ni ya kinafiki bado unaenda kuwapigia magoti, sasa nani mnafiki kati yenu?

Fikiria kwamba hadi kwenye bajeti tunaweka sehemu ya misaada! Ni kwamba tunakiri wazi tutaomba misaada kwa kuwa sisi ni ombaomba. Kama tuna uwezo wa kuita watu mabeberu basi ifikie mahali tupange bajeti bila kuwa na sehemu inayotegemea bajeti. Habo tu ndio tutaweza kutamba tutafanya maendeleo kwa pesa zetu za ndani.
 
Back
Top Bottom