Watanzania tuiombee Tume ya Uchaguzi ituvushe salama

Watanzania tuiombee Tume ya Uchaguzi ituvushe salama

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kama yupo anaetutakia amani na nchi yetu kwenye kipindi hiki basi atusaidie kuifanya Tume ya uchaguzi isiyumbishwe na wanasiasa wote.

Afande Sirro ni msomi sana na muelewa, Maaskofu na Masheikh ni waelewa sana, wananchi ni wapenda amani na ni waelewa sana. Makundi yote haya washirikiane kupambana na mtu yeyote yule anaeiamuru au kuishawishi Tume isiweze kufanya kazi yake ya kitaaluma, maana Tanzania ni kubwa kuliko mtu au chama cha siasa.

Mheshiwa Afande Sirro, watu wa dini na wananchi simameni nyuma ya Tanzania sio nyuma ya mtu, chama au maslahi. Tuwaache watanzania waamue nani wawe viongozi wao, tuwaache wanasiasa wakaukiwe makoo yao kwa kuwashawishi wapiga kura kwa usawa. Historia itakuja kutuhukumu vizuri au vibaya kwa matendo yetu, amani ikitoweka kwa kupigana au vikwazo tutajilaumu sana sisi wenyewe na vizazi vyetu vitatulaumu pia. Historia lazima itakuja kuandikwa kuhusu nani kasababisha nini kwasababu gani.

Viongozi wa tume hampendi historia ije iandikwe vizuri kuhusu nyinyi? Msitishwe tendendeni haki hata kama haki itawagarimu, hakuna anaeingia peponi akiwa hai.
 
Akili na busara vitumike, hayo mambo hayaitaji maombi, ni utelekezaji, mnasumbua sana Mungu kufanya maombi ya vitu obvious, wapo watu wenye genuine uhitaji wa divine intervention
 
Akili na busara vitumike, hayo mambo hayaitaji maombi, ni utelekezaji, mnasumbua sana Mungu kufanya maombi ya vitu obvious, wapo watu wenye genuine uhitaji wa divine intervention
Siku watanzania wengi watakapogundua kuwa maombi, kusema na kuandika hakutoshi kubadili hali ilivyo tutakuja kuona hatua ingine zaidi.
 
Akili na busara vitumike, hayo mambo hayaitaji maombi, ni utelekezaji, mnasumbua sana Mungu kufanya maombi ya vitu obvious, wapo watu wenye genuine uhitaji wa divine intervention
Siku watanzania wengi watakapogundua kuwa maombi, kusema na kuandika hakutoshi kubadili hali ilivyo tutakuja kuona hatua ingine zaidi.
Vyeo vya kuteuliwa vinachanga sana, mpaka watu wanasahau taaluma zao.
 
Mkuu ni kweli kabisa, mambo mengine ni kumsumbua Mungu, hili la kuizibiti Tume lipo ndani ya uwezo wetu. Mungu tumpe nafasi asikilize wagonjwa na watu walio na matatizo serious.
Akili na busara vitumike, hayo mambo hayaitaji maombi, ni utelekezaji, mnasumbua sana Mungu kufanya maombi ya vitu obvious, wapo watu wenye genuine uhitaji wa divine intervention
 
Tumuombe magufuli akubali uchaguzi huru na kupokea matokeo yoyote.

Dunia nzima haimtaki Magufuli
 
Back
Top Bottom