Watanzania tukatae serikali Moja, Mbili au Tatu. Tupiganie REFERENDUM.


Hilo ndio CCM hawalitaki maana ukiuwa muungano na yenyewe inakufa....hail TANGANYIKA you all!

 

Wandugu mchana mwema; Mfano mwingine TALAKA... Mke akingangania talaka na kumburuza Mumewe kwa wahusika, itabidi mume atoe talaka na asiulize we mama watoto wangu utaenda wapi na kuiishi na nani? talaka ikitolewa tu hapo hayamhusu mume tena. huyo ex-mke atajua lake na maisha yake (kumradhi/hashakum awe kahaba au jambazi au gaidi au Barmedi nk,) Kwa hiyo haijalishi awe kama Somaliya au Iraki au Afghanistan !! Sasa hapo ndo tatizo letu Vile Mume atabeba tija na matokeo yote ya mustakabali ( yaani kutunza watoto na kulipia madeni yote) Wakuu Jambo hili ni la kujikamua na kulitafakari kiutu uzima. siyo kufuata mahanjamu na presha la viongozi njaa na wasiyo na misimamo. tukubali
kupoteza machache ili tuokoe shehena kubwa la jahazi. LONG LIVE TANZANIA.
 

Mkuu turudishe na ile kauli mbiu yetu ya "UHURU! KAZI YA TANU"
 
Mkuu naheshimu hisia zako na maoni yako fika, Lakini nachokijua mie kuwa " Zama (zamani) hairudi nyuma "
Sidhani kama TIME inajirejesha awali nyuma.
kama upo uhai Tupo tutona.
 

Ndiyo yale yale ya tume ya Nyalali kuuliza wananchi kama wanataka kuendelea na mfumo wa chama kimoja au la wakati wanafahamu kabisa wananchi wengi hawana mwamko wa kisiasa na aina za mifumo mbalimbali utawala ikichukuliwa CCM ilikuwa imeshika hatamu za uongozi. Tume ya Nyalali ilifahamu jibu hata kabla ya kwenda kuwahoji wananchi.

Leo wananchi wana mwamko wa kisiasa, wanasiasa wetu kwa kujua hivyo, waliamua kuwekwa kufuli kwenye swala la muungano ndani ya hadidu za rejea kitu ambacho kimewanyima wananchi uhuru wao katika maamuzi ya mstakabali wa nchi yao.
 
Serikali ziwe mbili. Ya Tanganyika, na ya Zanzibar... Bora tuanze upya...
Kukata mzizi wa fitina, watupe hii kura ya referendum tujue moja na kila mmoja arudi majumbani kwake akijua wananchi wengi wanataka nini.

Hii ndiyo maana ya demokrasia yenye mipaka iliyowazi.
 
Mkuu naheshimu hisia zako na maoni yako fika, Lakini nachokijua mie kuwa " Zama (zamani) hairudi nyuma "
Sidhani kama TIME inajirejesha awali nyuma.
kama upo uhai Tupo tutona.

Kaka hata RUSSIA ilimezwa na USSR kwa miaka 80 (1917-1991) bila ridhaa ya wananchi wake na hatimaye ikarudi na bado ipo na USSR is gone.......forever hopefully


 
Ewe mola tunakuomba
Uibariki nchi yetu
Tanganyika na jirani zetu
Eee Mola

Salum Abdallah Yazid and Cuban Marimba Band- 1961
 
umegusia ukweli japo ni kidogo mkuu, dudu muungano tukiling'ang'ania madhala yake yanaweza kuwa mabaya siku za usoni! tunaweza zalisha vikundi vya upigania uhuru, tuwe tayari kushuhudia mabomu yakilipuliwa, kwa kutumia charisma! madhala ya kutotaka kuongelea muungano yanaweza kuwa mabaya na makubwa!

kwa upande wa CCM wanawakalilisha vijana wao kuwa muungano uliopo unafaa, pasi kuangalia viashiria tulivyoanza kuvishuhudia! vijana wanacopy ideal za zamaani saana! nimemsikia kijana mmoja kwenye tv akichemka!

suala wanalotetea wale wanaopenda mfumo wa sasa uendelee ati ni ghalama za uendeshaji wa serikali itakuwa kubwa, they dont state upande gani utazidiwa na ghalama! kwa upande wa tanganyika kwa mtazamo wangu ghalama zitapungua tuu! hebu fikiria watanganyika tumekopa mpaka mawaziri kwa wenzetu! kwa ghalama zetu, achiambali mlalahoi wa bara kumlipia umeme wenzetu! tena wengine wenye uwezo! hebu tuangalie kwakina hoja zetu!
 
Kitu cha kushangaza ni kuona kuwa vyama vyetu vya siasa pamoja na asasi zimerukia hii bandwagon ya serikali tatu kana kwamba huu ndiyo muarobaini wa matatizo ya muungano wakati kiini cha tatizo na mazingira ya kisiasa kwa sasa hayawezi kutatuliwa na kuwepo kwa serikali tatu achilia mbali gharama za kuziendesha.

Wanasiasa wetu wameamua kuwa non-committal kwa kujificha kwenye hadidu za rejea zilizoainisha misingi muhimu ya kuzingatia kana kwamba hayo yalikuwa ni makubaliano na wananchi wengi.
 

Hapo ndugu yangu si kweli umelinganisha vitu ambavyo kwa namna yoyote hailingani kabisa. Unaweza kuwa na point lakini mifano ikakupoteza hivyo hata poiny yako ikawa ni pointless. Jaribu kutafuta mifano mingine lakini siyo huo. Baba na mama ni wazazi Muungano si mzazi. Baba au mama au wote wakifariki mtoto anaitwa yatima mbona Russia haiitwi yatima baada ya muungano kufa na maisha yanasonga mbele? "Si kila unachofikiri ukiseme bali kila unachosema ufirkiri"
 
Mm nahisi watanganyika wanaona aibu kuirejesha tanganyika yao,mbona kule zanzibar wanajinasibu kwa zanzibar yao sio zanzibar pekee yenye kujinasibu bali pia kenya,italiy,rwanda wanajinasibu kwa utaifa wao,tanzania ni jina la mpito tu lakini asili yenu ni watanganyika tu,mkataa kwao mtumwa.
 
Hoja imepita, wanokubali sema ndiyooooooooooooooooo, wanokataa sema siyoooooooooooooooooooooo
 

Naiona Tanzania Kusini na Tanzania Kaskazini zinakuja kwa mbaaaaaali!
 

Tatizo liko hapo kwenye namna ya kuuvunja. tukiwaambia znz kuwa katika deni la taifa tulilonalo mfano tirioni 300 nyie mtatakiwa kulipa tirioni 50 hiyo pekee inatosha kuanzisha vurugu kati ya tanganyika na znz kama ilivyo kwa hizo nchi za sudan na sudan kusini, hao wanajeshi tutakao gawana ni wengi sana tangu vijana walioko sasa mpaka wazee wa miaka 80 au 70 bado wako kwenye muungano kwa vyovyote znz haitaweza kuwalipa kama walivyolipwa kwenye muungano nini kitatokea?kumbuka znz hakuna chochote cha kuingiza pesa zaidi ya utalii,bandari na vikarafuu ambapo. waznz wanaakili za kiarabu wanacholilia kikubwa tu ni kujiunga oic na kuwa moja ya nchi huru za kiislam hiyo ndio hoja yao kuu sasa watu hawa ni wakuangalia sana, nigeria walilia hivyo hivyo kujitenga walipojitenga bado wanalazimisha viongozi wote wa serikali wawe waislam, yaani ni watu wakulalamika tu na vurugu bila vita hawana raha, sasa watu hawa wanacholilia kujitenga nini kama ni gesi tanganyika in a gesi ya kusambaza africa mashariki na kati kwa muda mrefu kama ni uranium ipo nyingi tanganyika. hawa watu wanataka kutuletea matatizo tu, wengine wana viramani feki wanasema 10km za dar ni ardhi yao na ndivyo wanavyoamini
 
Tatizo hiyo referendum haimo kwenye hadidu rejea za rasimu iliyotangazwa.

Kingine kinachonitatiza ni juu ya uelewa wa wananchi juu ya maana halisi ya serikali,muundo wake na namna yake ya uajibikaji. Pengine sawa serikali tatu,je nini taswira kimataifa?

Binafsi ningefikiri labda tungepiga hatua nyingine ya nchi mbili hizi kuungana moja kwa moja kupata nchi moja kubwa yenye nguvu ya ushawishi wa kiuchumi.Na hii ingekuwa vema hata kwa majirani zetu wajifunze ili ile azma ya kuelekea EAC na AU iweze kufanikiwa.
Kiukweli serikali tatu italeta mgongano si tu wa kimaslahi bali hata ule wa kihitifaki katika siasa za afrika na dunia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…