Watanzania tulikubali suala la tozo mpya za miamala halafu leo tunaanza kulalamika!

Watanzania tulikubali suala la tozo mpya za miamala halafu leo tunaanza kulalamika!

Aise! Wabunge wa sasa wa CCM walipewa uwakilishi na wananchi gani wakati walipewa Ubunge na Mwendazake kwa kutumia Tume ya Uchaguzi ya CCM na Vyombo vya ulinzi na usalama wa Taifa?
 
Hao wabunge hawakuchaguliwa na wananchi, bali walichaguliwa na hiyo hiyo serikali, ndio maana wanalinda maslahi ya serikali. Usitake kutuletea story za kutuvuruga boss.
Ni kweli, lakini bado wanatuwakilisha. Na hata mbunge akichaguliwa, huwakilisha waliomchagua na wasio mchagua.
 
Aise! Wabunge wa sasa wa CCM walipewa uwakilishi na wananchi gani wakati walipewa Ubunge na Mwendazake kwa kutumia Tume ya Uchaguzi ya CCM na Vyombo vya ulinzi na usalama wa Taifa?
Kama tuliweza kukubali serikali kutuchagulia wawakilishi wa kuisimamia, basi hili la tozo ni dogo sana. Tutulie tu.
 
... huo ndio ukweli wenyewe. Let's learn in a hard way kwa ujinga wetu!

Nendeni kwenye mikutano ya kisiasa/kampeni mkasikilize na kuchuja sera na ilani - hatuna nafasi sisi!

Someni sera za vyama na ilani zao mpate mwanga wa jinsi zitakavyosaidia au kuumiza maisha yenu watanzania - hayatuhusu sisi!

Fuatilieni vyombo vya habari mjue yanayojiri nchini na Bungeni kwa manufaa ya maisha yetu na vizazi vyetu - mambo ya wanasiasa hayo!

Sikilizeni hotuba za viongozi wa kisiasa na kuzichambua kwa umakini - fiesta iko mtaani leo!

Kutakuwa na mikutano ya kisiasa kuhusu Katiba Mpya - hayatuhusu, tumpigie kura Diamond ashinde!

Jamani saa mbili usiku wekeni taarifa ya habari kuna jambo zito la kitaifa - kaangalie chumbani kwako na mkeo sisi tunaangalia mchezo!

Siasa ndio kila kitu ndiyo inayoamua maisha yetu ila ndicho kitu kinachopuuzwa zaidi na watanzania! Unapopuuza siasa unapuuza maisha yako hivyo tusilalamike wala kumsingizia mtu; ni matokeo ya upumbavu wetu wenyewe!
Kamanda kwanza nikupe salute. Umenena vyema. Kati ya comment jamii forum ww unatakiwa upewe tuzo. Niliandikaga ujumbe kama huu kuna baadhi ya watanzania waliishia kuponda kuwa mbona inaniuma sana na wengine wakitoa vi like tu bila ku comment.wawili tu waka support
 
Wabunge ni wawakilishi wetu. Tumewapeleka wakaisimamie serikali kwa niaba yetu. Kama wawakilishi wetu wamekubali maana yake tunaowakilishwa tumekubali.

Kama hawa wawakilishi wameenda kukubali kitu ambacho hatujawatuma, tuwalalamikie wao na kuwawajibisha na si serikali. Zaidi ya hapo tutulie.
Wewe una mbunge uliyempeleka bungeni? Ninachojua, hao unaowaita ni wabunge, hawawawakilishi wananchi, waliteuliwa na marehemu, kuanzia kwenye kura za maoni ndani ya CCM.
 
Utawawajibisha wabunge vip wakati katiba haitoi hiyo nafasi.Kwa katiba hii ata tuwe na wabunge vihiyo kiasi gani hatuna chakuwafanya hadi miaka mitano ipite.Ndo maana wenye haja wanaona huitaji wa katiba mpya itakayoweza kuweka utaratibu wa wananchi kumwajibisha mwakilishi wao pale wanapoona hakidhi vigezo anapokua tayari ni mbunge.Kwa bunge hili la sasa tutegemee maumivi yakutosha maana kamwe huwezi kupata jambo jipya la kuinufaisha nchi.
 
Back
Top Bottom