Watanzania tumefikia hatua ya kuwa Wanyama, roho mbaya kiasi cha kufikia kurecord tu Mtanzania mwenzetu anauwawa na Wapita njia?

Watanzania tumefikia hatua ya kuwa Wanyama, roho mbaya kiasi cha kufikia kurecord tu Mtanzania mwenzetu anauwawa na Wapita njia?

rest in peace kamanda .......kiukweli hata mimi kusikia niliumia sana hata responce ya watu tu baada kifo inatia mashaka hata kuliongelea watu hawaliongelei kukemea watu hawakemei ......kiujumla na hizi changamoto zinazotokea katika jamii udhalilishaji wa watoto na watu wazima style hiii sidhani kama tutaweza tokomeza kwa ukimya huu tanzania tumepoa sana ujinga na uchoyo ukatupata katika ubora wetu....umoja kama taifa umepotea kama mtu anaweza fanyiwa hivi katika ardhi mama yake na watu hawasemi hata kukemea mungu atusaidie sana tumepotea kama taifa
 
Mkitoka hapo hoo huu mwenge uchawi.

Siku ya mashujaa ifutwe.

Sio kuwalaumu sana kwa sababu hayo propaganda yake sio ndogo.

Ukisikia hiyo ‘armistice day’ huko kwa wenzetu propaganda yake ya nationalism sio ndogo.

Na namna serikali zao zinavyotumia hela nyingi nyingi kwenye nationalism propaganda na mbinu zenyewe sasa jamaa ni hatari.

Ni hivi msijiongopee na hili halina mzaha hata kidogo; usalama wa taifa ni mchezo wa watu wenye akili tu (hakuna cimpromise hapo kwa wazungu).

Na nationalism propaganda inataka kutumia akili kubwa sana ni amongst the priority za national security.

Wanaelewa basi hao watu.

Ukiona raia wako anauliwa na wageni na ndugu zake wanaangalia tena nchini kwenye nchi yake.

Siasa za Tanzania ni kukubali kwa sisi wengine let fate take its place.
 
Walimtazama akigombana kwa ajili ya njia, akashuka kwenye bus kugombana na madereva wa malori. wakammwagia kvant kwenye macho akakosa control akaanguka wakamshindilia vyuma kichwani.

Watanzania tumekuwa waoga hivi?

Alijitetea mwenyewe, akafa, Pole dereva, Mungu mpokee kijana wako

Hiyo nchi ya Rwanda sijui Burundi na madereva wale NAWALAANI KWA JINA LA BWANA.
Umekunywa mbege asubuhi hii saa 11 kasoro?
 
Wabongo roho mbaya+makatili tu point yake ndiyo hiyooo

Ova
actually,
inaweza kua kweli kwasabb hali kama hiyo huonekana sana kwa dereva daladala dhidi ya wa bodadoda, au dereva wa Lori dhidi ya wa dalala, sasa sembuse huyo wa busi dhidi ya malori?

kiujumla madereva hawapendani labda wawe wa aina moja ya magari but tofauti na hapo ni kuvimbiana, chuki na kukorimeana kila moja akijiona ana haki zaidi ya mwingine..

Abiria wanahusikaje hapo dereva ikiwa kwa utashi, maamuzi na ujuaji wake kutanua tena wrong site or side na kujuchubua gari au kakwanyua site mirrors za magari ya wengine wakiwa right side and site,

kwa hiyo aachwe tu, na watu walivyo vurugwa na maisha, anaogopwa au anapendwa sana?🐒
 
SIku moja ukijikuta kwenye situation kama hiyo utanielewa , unajua kutokuamini kinachotokea na kuifanya akili ikubaliane na hali kwa haraka ni rahisi? Hebu wazia unanusurika kupasua kichwa au kufa kabisa alafu muda huo huo uone kundi zima linakucheka unafikiri hautapata wenge?
Watu hawataki kuwa mashahidi mixer washukiwa
 
Polisi Hadi Sasa Bado tu hawajawakamata.Hii Nchi hii!
 
Umoja kama taifa umepotea kama taifa,

Hili ni kubwa sanaaa miongoni mwetu.Nimeanzisha biashara sehemu, baada ya siku kadhaa juzi tarehe 4 wamevunja wanechukua TV na radio,naona kuna watu wamefurahia.Tafsiri yake ni ngumu kuielewa
 
Alibaba maisha zaidi ya Watanzania 60, je ni kweli tulichoweza kumsaidia Mtanzania mwenzetu akiuwawa na Watu ambao sio Watanzania ni kurecord video?

Unauma saaana, inatafakarisha saaana, Hivi hiki kitengo hiki kinafanyika Kenya au Rwanda ingekuwaje? Anyway itoshe kusema Wanaume wote mlio kuwepo kwenye lile basi wote mtafutiwe jina mipya.

Pumzika kwa Amani kaka, rafiki, umeangushwa na watu ambao walipaswa kukupigia kwa namna ukivyojitolea kuwapigania.

PIA SOMA
- Dereva wa basi la Mtei Express auawa na madereva wa malori kutoka Rwanda

Huenda alimsema vibaya kiongozi hasa spika.
Spika alishatoa amri ya kunyooka na mtu yeyote anayemsema vibaya kiongozi. Sasa hatujui kama alimsema vibaya kiongozi yupi au ni ubaya ubwela tu.

Nchi ina Watu waliojengwa kiubinafsi sana . Watu wanamuangalia mtu anauawa hadharani bila kuchukua hatua yoyote . Nadhani hata wakina mama wangeweza wakashuka wakamzuia yule Muuaji asiye achalia mbali wanaume .

Uzalendo umeuawa na waliouza rasilimali zetu kwa kuwathamini wageni.

Lakini pia Watu wanaopotea huku wengine wakikaa kimya tena wakiwa ni watawala wanaopaswa kutulinda nalo ni jambo la hatari sana. Watu wakiambiwa waandamane wapinge mauaji na kutekwa kwa Watu wasio na hatia wanasema hayo ni mambo ya Chadema hayaruhusu.

Kwa sasa roho ya ubinafsi ni kubwa sana na imejengwa na wale tuliowapa madaraka ya kujenga umoja,utu, upendo ,amani na mshikamano. Kila mtu yupo bize kuangalia mambo yake . Hata Alphonce Mawazo aliuawa hadharani bila Watu kusaidia.

Uligusa kamba ya mtu anayoitumia kula kwa urefu wake basi ujue atanyooka na wewe.

2025 tuifute CCM na unyama wake utaondoka na Tanzania,Tanganyika na Zanzibar zitakua nchi bora sana zenye kuwalinda na kuwaheshimu Watu wake.


Watanganyika hatuna pa kukimbilia endapo tukiendelea kuacha hawa madalali waendelee kuuza nchi yetu kwa wageni.

Watanganyika tukiwa wakimbizi hata Zanzibar hawawezi kutopokea.
Watanganyika Nchi yetu ni kwa ajili yetu na watoto wetu na wajukuu zetu. Tusidanganywe Kuwa wageni wanatusaidia la hasha . Tukiwaacha waovu nchi waibinafsishe kwa wachina na wazungu na waarabu na hata nchi nyingine yeyote basi tumekwisha.
Maisha yetu watanganyika ni ya kubishana ,kukemeana ,kuambiana kwa maneno lakini wenzetu hawana utamaduni huo hata hapo Zanzibar kwa majirani zetu zaidi hawana uvumilivu na watanganyika na mila zao na dini zao za asili au zilizo tofauti na ya kwao.

Tujifunze kuwapigania wengine wanapoonewa itatusaidia kwani uonevu na mauaji vileramalaki sana Tanganyika kwa sasa.
 
Kawaida sana. Kama watu wanapigwa risasi mchana kweupe, wanatekwa, wananyimwa haki zao mahakamani na "tunakenua mimeno tu" hilo haliwezi kuwa jambo la kushangaza. Expect the worse...
 
Back
Top Bottom