Watanzania tumejifunza nini kupigwa Risasi na kujeruhiwa kwa Donald Trump?

Watanzania tumejifunza nini kupigwa Risasi na kujeruhiwa kwa Donald Trump?

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Sote naamini tunaendelea kufuatilia taarifa ambayo imeisimamisha Dunia nzima na kuitikisa pamoja na kuteka vyombo vyote vya habari na mitandao ya kijamii ulimwenguni kwote kunakotokana na kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa Donald Trump Rais mstaafu wa Marekani na mgombea Urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican alipokuwa akihutubia jukwaani huko Pennsylvania.

Taarifa za kupigwa kwa Donald Trump zimewashitua sana wamarekani na kuwaunganisha wanasiasa wote wakubwa Nchini humo wale wa Democratic na Republican,katika kulaani tukio hilo na kusema kuwa Marekani siyo mahali pa siasa za vurugu .Rais Bideni pia amelaani sana tukio hilo la kupigwa risasi kwa Mpinzani wake huyo Mkuu.

Trump.jpg

Tukio hilo limewakumbusha mbali sana hasa kwa kuzingatia kuwa wamarekani wamewahi kupoteza Marais wao baada ya kupigwa Risasi.na kwa mara ya Mwisho ni kwa John F Kennedy aliyepigwa risasi miaka ya 60 ambaye alifariki Dunia.

Sasa nataka kuwaulizeni Watanzania mmejifunza nini kupitia tukio hilo? Mimi nimejifunza kuwa matukio ya aina hiyo yanaweza kutokea mahali popote pale na nchi yoyote ile bila kujali ni nchi maskini au nchi tajiri, linaweza kutokea hata kama nchi ina teknolojia ya kiwango cha juu au intelijensia ya kiwango cha kimataifa.

Embu fikiria Marekani yenye kila aina ya teknolojia ya kisasa, zana za kisasa, miundombinu bora, ujuzi na maarifa ya kila kitu lakini walishindwa kung'amua tukio hilo na kulizima kabla ya risasi kumpata mgombea Urais jukwaani.

Nimejifunza pia uharaka wa vyombo vyake vya ulinzi katika kumuokoa mtu kutoka eneo la tukio na kumkabili adui, maana adui aliuawa palepale lakini ukiangalia namna walinzi walivyokimbia haraka kwenda kumzingira Trump pale jukwaani huku wengine wakiendelea kulizunguka jukwaa zidi ya adui, namna walivyokuwa wakimtoa jukwaani na kumkimbiza haraka kwenye gari na walivyojipanga kimapambano lile eneo.

Umahiri wa kumtungua adui bila kupiga risasi hovyo hovyo ambazo pengine zingeleta madhara kwa wengine, lakini pia umakini wa kutumia Risasi na silaha zao maana walinzi wale walijibu mapigo kwa kumuelekea adui na siyo kupiga risasi zisizo na maana au kuleta taharuki zaidi.

Lakini pia namna watu waliokuwa mkutanoni walivyokaa chini kwa uharaka sana kujihami, hapa ni somo zuri sana maana kama wangeamua kukimbia huku na huku pengine kungetokea maafa au vifo vingi kutokana na kukanyagana .lakini wamarekani wale nimeona wote walilala chini kwa haraka sana huku vyombo vyao vikimkabili adui kwa uhodari mkubwa sana.

Lakini pia watanzania hususani wanasiasa tuwe wasikivu sana pale vyombo vya ulinzi hususani Jeshi la polisi linapowanyima kibali chama kufanya mkutano sehemu fulani kwa sababu ya taarifa za kiintelijensia kwa sababu za kiusalama.

Kwa sababu nimekuwa nikiona baadhi ya vyama hususani CHADEMA wakinyimwa kibali kwa sababu ya intelijensia au taarifa kuonyesha viashiria vya uvunjifu wa amani au hali kutokuwa shwari au kutokea kwa uvunjifu wa amani. CHADEMA huanza kuleta kukejeli au kutoa lugha za dharau au ujuaji.

Mwisho tuache kuitupia lawama Serikali kwa kila jambo kuwa imehusika. Hii ni kwa kuwa unakuta mtu kapotea au kakutwa na majereha halafu watu kwa mihemuko wanaanza kuropoka kuwa Serikali imehusika, jambo ambalo unakuta hawana ushahidi wala uthibitisho wa aina yoyote ile ambao unaweza kutolewa mahakamani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa,Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.

Pia, soma=> Marekani: Donald Trump ajeruhiwa kwa risasi akihutubia mkutano wa hadhara
 
Mwisho tuache kuitupia lawama serikali kwa kila jambo kuwa imehusika.hii ni kwakuwa unakuta mtu kapotea au kakutwa na majereha halafu watu kwa mihemuko wanaanza kuropoka kuwa serikali imehusika.jambo ambalo unakuta hawana ushahidi wala uthibitisho wa aina yoyote ile ambao unaweza kutolewa mahakamani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mitano tena
 
Ndugu zangu Watanzania,View attachment 3041884View attachment 3041885

Sote naamini tunaendelea kufuatilia taarifa ambayo imeisimamisha Dunia nzima na kuitikisa pamoja na kuteka vyombo vyote vya habari na mitandao ya kijamii ulimwenguni kwote kunakotokana na kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa Donald Trump Rais mstaafu wa Marekani na mgombea Urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican alipokuwa akihutubia jukwaani huko Pennsylvania.

Taarifa za kupigwa kwa Donald Trump zimewashitua sana wamarekani na kuwaunganisha wanasiasa wote wakubwa Nchini humo wale wa Democratic na Republican,katika kulaani tukio hilo na kusema kuwa Marekani siyo mahali pa siasa za vurugu .Rais Bideni pia amelaani sana tukio hilo la kupigwa risasi kwa Mpinzani wake huyo Mkuu.

Tukio hilo limewakumbusha mbali sana hasa kwa kuzingatia kuwa wamarekani wamewahi kupoteza Marais wao baada ya kupigwa Risasi.na kwa mara ya Mwisho na kwa John F Kennedy aliyepigwa risasi miaka ya 60.

Sasa nataka kuwaulizeni Watanzania mmejifunza nini kupitia tukiona hilo? Mimi nimejifunza kuwa matukio ya aina hiyo yanaweza kutokea mahali popote pale na nchi yoyote ile bila kujali ni nchi maskini au nchi tajiri ,linaweza kutokea hata kama nchi ina teknolojia ya kiwango cha juu au intelijensia ya kiwango cha kimataifa.

Embu fikiria Marekani yenye kila aina ya teknolojia ya kisasa,zana za kisasa, miundombinu bora,ujuzi na maarifa ya kila kitu lakini walishindwa kung'amua tukio hilo na kulizima kabla ya risasi kumpata mgombea Urais jukwaani.

Nimejifunza pia uharaka wa vyombo vyake vya ulinzi katika kumuokoa mtu kutoka eneo la tukio na kumkabili adui,maana adui aliuwawa palepale.lakini ukiangalia namna walinzi walivyokimbia haraka kwenda kumzingira Trump pale jukwaani huku wengine wakiendelea kulizinguka jukwaa zidi ya adui ,namna walivyokuwa wakimtoa jukwaani na kumkimbiza haraka kwenye gari.

Umahiri wa kumtungua adui bila kupiga risasi hovyo hovyo ambazo pengine zingeleta madhara kwa wengine,lakini pia umakini wa kutumia Risasi na slaha zao.maana walinzi wale walijibu mapigo kwa kumuelekea adui na siyo kupiga risasi zisizo na maana au kuleta taharuki zaidi.

Lakini pia namna watu waliokuwa mkutanoni walivyokaa chini kwa uharaka sana kujihami.hapa ni somo zuri sana maana kama wangeamua kukimbia huku na huku pengine kungetokea maafa au vifo vingi kutokana na kukanyagana .lakini wamarekani wale nimeona wote walilala chini kwa haraka sana huku vyombo vyao vikimkabili adui kwa uhodari mkubwa sana.

Lakini pia watanzania hususani wanasiasa tuwe wasikivu sana pale vyombo vya ulinzi hususani jeshi la polisi linapowanyima kibali chama kufanya mkutano sehemu fulani ,kwa sababu ya taarifa za kiintelijensia kwa sababu za kiusalama.

kwa sababu nimekuwa nikiona baadhi ya vyama hususani CHADEMA wakinyimwa kibali kwa sababu ya intelijensia au taarifa kuonyesha viashiria vya uvunjifu wa amani au hali kutokuwa shwari au kutokea kwa uvunjifu wa amani . CHADEMA huanza kuleta kukejeli au kutoa lugha za dharau au ujuaji.

Mwisho tuache kuitupia lawama serikali kwa kila jambo kuwa imehusika.hii ni kwakuwa unakuta mtu kapotea au kakutwa na majereha halafu watu kwa mihemuko wanaanza kuropoka kuwa serikali imehusika.jambo ambalo unakuta hawana ushahidi wala uthibitisho wa aina yoyote ile ambao unaweza kutolewa mahakamani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mbona sijaelewa lengo unataka kusema au unataka ku'justify' nini?
 
Ndugu zangu Watanzania,View attachment 3041884View attachment 3041885

Sote naamini tunaendelea kufuatilia taarifa ambayo imeisimamisha Dunia nzima na kuitikisa pamoja na kuteka vyombo vyote vya habari na mitandao ya kijamii ulimwenguni kwote kunakotokana na kupigwa risasi na kujeruhiwa kwa Donald Trump Rais mstaafu wa Marekani na mgombea Urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican alipokuwa akihutubia jukwaani huko Pennsylvania.

Taarifa za kupigwa kwa Donald Trump zimewashitua sana wamarekani na kuwaunganisha wanasiasa wote wakubwa Nchini humo wale wa Democratic na Republican,katika kulaani tukio hilo na kusema kuwa Marekani siyo mahali pa siasa za vurugu .Rais Bideni pia amelaani sana tukio hilo la kupigwa risasi kwa Mpinzani wake huyo Mkuu.

Tukio hilo limewakumbusha mbali sana hasa kwa kuzingatia kuwa wamarekani wamewahi kupoteza Marais wao baada ya kupigwa Risasi.na kwa mara ya Mwisho na kwa John F Kennedy aliyepigwa risasi miaka ya 60.

Sasa nataka kuwaulizeni Watanzania mmejifunza nini kupitia tukiona hilo? Mimi nimejifunza kuwa matukio ya aina hiyo yanaweza kutokea mahali popote pale na nchi yoyote ile bila kujali ni nchi maskini au nchi tajiri ,linaweza kutokea hata kama nchi ina teknolojia ya kiwango cha juu au intelijensia ya kiwango cha kimataifa.

Embu fikiria Marekani yenye kila aina ya teknolojia ya kisasa,zana za kisasa, miundombinu bora,ujuzi na maarifa ya kila kitu lakini walishindwa kung'amua tukio hilo na kulizima kabla ya risasi kumpata mgombea Urais jukwaani.

Nimejifunza pia uharaka wa vyombo vyake vya ulinzi katika kumuokoa mtu kutoka eneo la tukio na kumkabili adui,maana adui aliuwawa palepale.lakini ukiangalia namna walinzi walivyokimbia haraka kwenda kumzingira Trump pale jukwaani huku wengine wakiendelea kulizinguka jukwaa zidi ya adui ,namna walivyokuwa wakimtoa jukwaani na kumkimbiza haraka kwenye gari.

Umahiri wa kumtungua adui bila kupiga risasi hovyo hovyo ambazo pengine zingeleta madhara kwa wengine,lakini pia umakini wa kutumia Risasi na slaha zao.maana walinzi wale walijibu mapigo kwa kumuelekea adui na siyo kupiga risasi zisizo na maana au kuleta taharuki zaidi.

Lakini pia namna watu waliokuwa mkutanoni walivyokaa chini kwa uharaka sana kujihami.hapa ni somo zuri sana maana kama wangeamua kukimbia huku na huku pengine kungetokea maafa au vifo vingi kutokana na kukanyagana .lakini wamarekani wale nimeona wote walilala chini kwa haraka sana huku vyombo vyao vikimkabili adui kwa uhodari mkubwa sana.

Lakini pia watanzania hususani wanasiasa tuwe wasikivu sana pale vyombo vya ulinzi hususani jeshi la polisi linapowanyima kibali chama kufanya mkutano sehemu fulani ,kwa sababu ya taarifa za kiintelijensia kwa sababu za kiusalama.

kwa sababu nimekuwa nikiona baadhi ya vyama hususani CHADEMA wakinyimwa kibali kwa sababu ya intelijensia au taarifa kuonyesha viashiria vya uvunjifu wa amani au hali kutokuwa shwari au kutokea kwa uvunjifu wa amani . CHADEMA huanza kuleta kukejeli au kutoa lugha za dharau au ujuaji.

Mwisho tuache kuitupia lawama serikali kwa kila jambo kuwa imehusika.hii ni kwakuwa unakuta mtu kapotea au kakutwa na majereha halafu watu kwa mihemuko wanaanza kuropoka kuwa serikali imehusika.jambo ambalo unakuta hawana ushahidi wala uthibitisho wa aina yoyote ile ambao unaweza kutolewa mahakamani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Umeharibu uzi ulipomalizia kwa kumtaja na kumpigia chapu mtu yule!
 
1720935716772.png
... Kennedy yeye ilipigangwa risasi vile yeye alichokozanga Papa Doc ndani ya Haiti vile Ruto naye kayakoroganga Haiti mwaka huu!
...
chezea Baron Samedi ulambwe na VOODOO!
😅
 
Wewe ni mpumbavu, intelijensia ipo kwa chadema tu? Kama umekosa cha kuandika bora ungekaa tu kimya chawa wewe

Huyu Mwashambwa kichwani kwake kuna matatizo makubwa. Ndiyo maana hata maandikobyake huwa hayana mpangilio wala mantiki.

Angekuwa na akili japo kiasi kidogo sana, halafu angekosa unafiki, alipofikia kuiongelea Tanzania, angejiuliza:

1) CCM ndiyo hufanya mikutano mingi kuliko vyama vyote, kwa nini haijawahi kutokea hata siku moja mkutano wa CCM ukazuiwa kwa sababu za kiintelijensia?

2) Angetofautisha kati ya uhalifu wa mtu mmoja mmoja au kundi la watu, na ule uhalifu wa kidola. Kwa tukio hili la USA, inaonekana wazi kuwa uhalifu ule ni wa mtu mmoja au kikundi cha watu lakini siyo wa kidola, ndiyo maana dola imehusika kikamilifu kupambana na mhalifu na katika uokoaji wa mhanga wa uovu ule. Shambulio la Lisu, kwa mfano, ulikuwa ni uhalifu wa kidola ndiyo maana dola nzima iliwalinda wahalifu. Dola iliandaa mazingira ya uhalifu kutendeka kwa kuwaondoa walinzi ili uhalifu utendeke, askari wa getini walifungua gate ili gari la wahalifu liingie, dola iliondoa CCTV camera ili waovu wasikamatwe, dola kwa kutumia askati wa barabarani ilisimamisha magari na bodaboda ili gari la wahalifu liondoke baada ya kutekeleza uhalifu. Dola ilizuia kabisa kufanya uchunguzi wa tukio lile hadi leo.
 
Ungeacha wenye kuelewa wajadili hoja na wewe usubiri hoja zenye kuendana na uelewa wako.
Nauliza lengo nini, siulizi maana ya hoja au mjadala. Unapoleta jambo kwenye public domain halina exclusion, linakuwa la wote na kama mleta hoja hajui kwa nini kaleta hoja, anaweza kuondoa hiyo hoja hadi atakapojua lengo lake au atakapoiboresha.
 
Huyu Mwashambwa kichwani kwake kuna matatizo makubwa. Ndiyo maana hata maandikobyake huwa hayana mpangilio wala mantiki.

Angekuwa na akili japo kiasi kidogo sana, halafu angekosa unafiki, alipofikia kuiongelea Tanzania, angejiuliza:

1) CCM ndiyo hufanya mikutano mingi kuliko vyama vyote, kwa nini haijawahi kutokea hata siku moja mkutano wa CCM ukazuiwa kwa sababu za kiintelijensia?

2) Angetofautisha kati ya uhalifu wa mtu mmoja mmoja au kundi la watu, na ule uhalifu wa kidola. Kwa tukio hili la USA, inaonekana wazi kuwa uhalifu ule ni wa mtu mmoja au kikundi cha watu lakini siyo wa kidola, ndiyo maana dola imehusika kikamilifu kupambana na mhalifu na katika uokoaji wa mhanga wa uovu ule. Shambulio la Lisu, kwa mfano, ulikuwa ni uhalifu wa kidola ndiyo maana dola nzima iliwalinda wahalifu. Dola iliandaa mazingira ya uhalifu kutendeka kwa kuwaondoa walinzi ili uhalifu utendeke, askari wa getini walifungua gate ili gari la wahalifu liingie, dola iliondoa CCTV camera ili waovu wasikamatwe, dola kwa kutumia askati wa barabarani ilisimamisha magari na bodaboda ili gari la wahalifu liondoke baada ya kutekeleza uhalifu. Dola ilizuia kabisa kufanya uchunguzi wa tukio lile hadi leo.
Ungeacha wenye akili wajadili hoja hii na wewe usubiri mada zingine nitakazoleta zenye kuendana na upeo wa akili yako.
 
Back
Top Bottom