Watanzania tumekuwa wajinga wa kuwatukuza Viongozi hata pale ambapo hapastahili. Kujipendekeza tu

Watanzania tumekuwa wajinga wa kuwatukuza Viongozi hata pale ambapo hapastahili. Kujipendekeza tu

NewPage

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2021
Posts
1,321
Reaction score
2,106
Humu kuna thread inasema "Rais Samia atoa shilingi bilioni 300 kukamilisha ujenzi majengo ya Serikali Dodoma". Hii ilishamiri zaidi kuanzia awamu ya tano na hii ya sita ninaona kama inaendeleza kwa kasi sana.

Utakuta hata Diwani na Mwenyekeiti wa Serikali za Mtaa anapoongelea fedha zilizotolewa na Serikali au jambo lililofanywa na Serikali wanaliunganisha na kutendwa na Mheshimiwa Rais.

Hii kwangu mimi imekuwa inanisumbua. Badala ya kusema tu kuwa Serikali imefanya hili au imetoa fedha basi fashion imekuwa ni jambo hilo limefanywa na Mhe. Rais au kitu hicho kimewezeshwa na Mhe. Rais.

Watanzania tumekuwaje? Hivi tumeshindwa hata kuelewa kuwa wananchi ndiyo kila kitu na wapo juu hata ya Rais? We are the people to make or unmake the government.

Yaani kadri siku zinavyoenda tunashindwa sana kujitambua! Na Ndugai kuomba msamaha wa namna ile ndiyo katengeneza precedent mbaya kabisa.
 
Huku mitunduruni tunapambana tu kaka.
Poa poa! Vipi Mwigulu anaipangaje Timu yake ya Chama ya kumrudisha kwenye ubunge? Kilimba atarudi kwenye uenyekiti?
 
Huu upumbavu unafanywa na mazwazwa ya CCM Tu usituhusishe Watanzania wote
Mbona sometimes hata watendaji wa Serikali kwa wanayoyatenda wao wanayahusisha na Rais?
 
Tangulia buchani kwa mgogo, mwambie akupe nundu na kidali unavyotaka...tunashukuru wakati pesa ni yako mwenyewe na ni wajibu wa kiongozi kusimamia maendeleo na ndio kazi yao,wanalipwa na kupata stahiki zote kwa kufanya hayo tunayowasifu kinafiki.
 
Akipewa LAWAMA Unafurahi unaruka ruka mpaka unajamba.

Akipewa SIFA unachukia kama KOBOKO.

Sasa tuamue MOJA. Kama atapewa LAWAMA ZOTE basi Apewe na SIFA ZOTE.

Period.
 
Chief amegeuka Bilionea ghafla anamwaga tu mahela kila mahali.

Yaani kodi zetu zimekua zake na anatoa kwa hisani.

Ndio maana hata ikaamuliwa tukope kwa ajili ya vyoo na hakuna aliyepinga.

Ila ajabu anakopa yeye zikifika anafanya anavyojisikia yeye ila tunaolipa ni sisi.
 
Akipewa LAWAMA Unafurahi unaruka ruka mpaka unajamba.

Akipewa SIFA unachukia kama KOBOKO.

Sasa tuamue MOJA. Kama atapewa LAWAMA ZOTE basi Apewe na SIFA ZOTE.

Period.
Ila kurukaruka inawezekana ikatokea lakini kujamba hapana kaka!
 
Humu kuna thread inasema "Rais Samia atoa shilingi bilioni 300 kukamilisha ujenzi majengo ya Serikali Dodoma". Hii ilishamiri zaidi kuanzia awamu ya tano na hii ya sita ninaona kama inaendeleza kwa kasi sana.

Utakuta hata Diwani na Mwenyekeiti wa Serikali za Mtaa anapoongelea fedha zilizotolewa na Serikali au jambo lililofanywa na Serikali wanaliunganisha na kutendwa na Mheshimiwa Rais.

Hii kwangu mimi imekuwa inanisumbua. Badala ya kusema tu kuwa Serikali imefanya hili au imetoa fedha basi fashion imekuwa ni jambo hilo limefanywa na Mhe. Rais au kitu hicho kimewezeshwa na Mhe. Rais.

Watanzania tumekuwaje? Hivi tumeshindwa hata kuelewa kuwa wananchi ndiyo kila kitu na wapo juu hata ya Rais? We are the people to make or unmake the government.

Yaani kadri siku zinavyoenda tunashindwa sana kujitambua! Na Ndugai kuomba msamaha wa namna ile ndiyo katengeneza precedent mbaya kabisa.
Watani zetu wa Kenya wanatushangaa Sana. Uliwahi kusikia wapi wanampongeza Uhuru kwa kutoa pesa za kujenga madarasa au reli ya SGR toka Mombasa? Pesa yote inatolewa na Serikali ambayo hukusanya hiyo fedha kupitia Kodi za Wananchi. Fedha atoe mwingine halafu sifa zote na mapambio wampe yeye!
 
Back
Top Bottom