Watanzania tumepewa uhuru kutokea vijiwe vya kahawa, hatuwezi kuwa sawa na walioupigania kutoka msituni

Watanzania tumepewa uhuru kutokea vijiwe vya kahawa, hatuwezi kuwa sawa na walioupigania kutoka msituni

Mwalimu ni moja ya vichwa adimu mno na mwenye akili sana, alijua kabisa uhuru ungechelewa sana kama tungeingia msituni. Hivi nawe unajiona ni shujaa kweli ambaye ungepambania Uhuru Kama tu unatumia jina bandia hapa JF?

Hamna lolote, uhuru wa Tanzania ulikuwa sio wa kupigania maana tulikuwa chini ya udhamini wa umoja wa mataifa hadi tuwe tayari kujitawala. Na muengereza aliyekabidhiwa kutuongoza hadi tuwe tayari kujitawala hakuipenda sana Tanzania. Usitake kumpa Nyerere sifa za uongo.
 
Upo sahihi ndio maana hata KUDAI HAKI zetu HATUWEZI tunasubiri TUPEWE kama tulivyopewa UHURU
Sir Robby,
Tatizo la watu wengi ni kuwa hawajui historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika.
Damu ya Waafrika ilimwagika kabla ya TANU kuundwa.

Tarehe 1 Februari, 1950, Dockworkers Union ilifanya mgomo mkali sana ambao wafanyakazi wa Bandari ya Dar es Salaam walipambana na askari wa kuzuia fujo waliotumwa na serikali kuvunja mgomo huo na askari 19 waliuliwa.

Historia ya Dockworkers Union inaanza mwaka wa 1947 na inaishia mwaka wa 1950 baada ya mauaji hayo.

Kiongozi wa Dockworkers Union Secretary General alikuwa Abdul Sykes akiwa na umri wa miaka 25 na nafasi hiyo alipewa na Waingereza lakini alijiuzulu kupisha shinikizo la mgomo na aliyechaguliwa kushika nafasi hiyo alikuwa Erka Fiah.

Yeye aliitisha mgomo uliosababisha mauaji na chama kupigwa marufuku.

Harakati hizi za Dockworkers Union na vyama vingine vya wafanyakazi vilitumika sana katika kusukuma agenda ya TAA kudai nchi pale Abdul Sykes alipochukua uongozi wa TAA 1950 kama Secretary General akitokea Dockworkers Union.

Hii historia nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdu Sykes.

Inasikitisha sana kuwa mswada wa historia ya TANU ulioandikwa na Abdul Sykes na Dr. Wllbert Kleruu mwaka wa 1962 haujulikani uko wapi.

Hii nayo ni historia ya pekee iloyojaa mazonge mengi hadi kusababisha Abdul Sykes kujitoa katika mradi ule.

Sasa ikiwa wewe historia unayoijua ya TANU ni hii historia rasmi haya huwezi kuyajua.

1682184868832.jpeg

Erika Fiah​
 
Kwahiyo hata MajiMaji Rebelion walikuwa wanaamini kuwa risasi za Mjerumani zitageuka Kahawa?

Kwanini wasiviite vita vya KahawaKahawa?

My point is Wapigania Uhuru wa Tanganyika sio wote walikuwa watu waoga wa kukaa kwenye vijiwe vya kahawa.
Hizo zilikuwa resistance tu. Wale walikuwa wanapigania koo zao. Sio kupigania uhuru. Vita kama hivyo vilikuwepo kwenye maeneo mengi Afrika inapotokea kingdom fulani inavamiwa kwenye eneo la utawala wake.
 
Sir Robby,
Tatizo la watu wengi ni kuwa hawajui historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika.
Damu ya Waafrika ilimwagika kabla ya TANU kuundwa.

Tarehe 1 Februari, 1950, Dockworkers Union ilifanya mgomo mkali sana ambao wafanyakazi wa Bandari ya Dar es Salaam walipambana na askari wa kuzuia fujo waliotumwa na serikali kuvunja mgomo huo na askari 19 waliuliwa.

Historia ya Dockworkers Union inaanza mwaka wa 1947 na inaishia mwaka wa 1950 baada ya mauaji hayo.

Kiongozi wa Dockworkers Union Secretary General alikuwa Abdul Sykes akiwa na umri wa miaka 25 na nafasi hiyo alipewa na Waingereza lakini alijiuzulu kupisha shinikizo la mgomo na aliyechaguliwa kushika nafasi hiyo alikuwa Erka Fiah.

Yeye aliitisha mgomo uliosababisha mauaji na chama kupigwa marufuku.

Harakati hizi za Dockworkers Union na vyama vingine vya wafanyakazi vilitumika sana katika kusukuma agenda ya TAA kudai nchi pale Abdul Sykes alipochukua uongozi wa TAA 1950 kama Secretary General akitokea Dockworkers Union.

Hii historia nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdu Sykes.

Inasikitisha sana kuwa mswada wa historia ya TANU ulioandikwa na Abdul Sykes na Dr. Wllbert Kleruu mwaka wa 1962 haujulikani uko wapi.

Hii nayo ni historia ya pekee iloyojaa mazonge mengi hadi kusababisha Abdul Sykes kujitoa katika mradi ule.

Sasa ikiwa wewe historia unayoijua ya TANU ni hii historia rasmi haya huwezi kuyajua.

Hii mzee kusema ukweli umetupiga kamba...ingekuwa watu walikufa vasi bendera yetu ingekuwa na rangi nyekundu
 
Hizo zilikuwa resistance tu. Wale walikuwa wanapigania koo zao. Sio kupigania uhuru. Vita kama hivyo vilikuwepo kwenye maeneo mengi Afrika inapotokea kingdom fulani inavamiwa kwenye eneo la utawala wake.
Havijawahi kutokea vita vilivyounganisha Jamii mbali mbali kama vya Majimaji.

Hao ndio walikuwa freedom fighters.
 
Hizo zilikuwa resistance tu. Wale walikuwa wanapigania koo zao. Sio kupigania uhuru. Vita kama hivyo vilikuwepo kwenye maeneo mengi Afrika inapotokea kingdom fulani inavamiwa kwenye eneo la utawala wake.
Nyakati...
"Risistance" ni mapambano.
Unaweza ukatalii vitabu vya historia.

Anza na Maji Maji na Mau Mau.
 
Havijawahi kutokea vita vilivyounganisha Jamii mbali mbali kama vya Majimaji.

Hao ndio walikuwa freedom fighters.
Hizo zilikuwa vita vya kugombania uhuru wa maeneo Yao ya utawala. Hizo stories zimekuwa amplified na kuhusishwa na kupigania uhuru maana walikuwa wanapinga wakoloni waliovamia maeneo yao. Hakukuwepo na unity iloyokuwa na vision ya kuunganisha vita vya kupigania uhuru.

Hadi pale baada ya Vita kuu ya kwanza ya dunia ujerumani ilivyopoteza makoloni yake mengi na hapo baadae mwishoni mwa vita kuu ya pili miaka ya 1945, umoja wa mataifa UN under Chapter XII ilianzisha International Trusteeship System for the supervision of Trust Territories ambayo ilikabidhi Tanganyika 1947 chini ya usimamizi wa UK kama trustee kwa maandalizi ya serikali na mfumo wa kisiasa kuwezesha wenyeji kujitawala.

Hivyo Mwingereza hakuwa na interest Tanganyika maana halikuwa koloni lake lilikuwa la ujerumani ambaye aliwekeza zaidi Tanganyika kuliko kwingereza tofauti na ilivyo Kenya lililokuwa koloni la Mwingereza kwa mfano tu uhuru wao waliupata kwa shida ukilinganisha na Tanganyika. Hivyo UK alikuwa ameshikilia koloni la Tanganyika akisubiri kutimiza takwa la UN na ndio maana uhuru wa Tanganyika ulipatikana smoothly kwa njia ya mazungumzo.
 
Ukiangalia historia ya uhuru wa tanzania utaona imechangia kwa kiasi kikubwa kushape fikra za watanzania wa leo, yaani ukisoma huon struggle kabisa zaid ya watu waliokua wanakutania kwenye bao na vijiwe vya kahawa eti ndo wapigania uhuru hao

Wako wanaosema historia ya Tanzania imechakachuliwa kwa upande mwingine nakubaliana nao ila still hata ukisoma huo upande wa uliochakachuliwa huon struggle kabisa

Madhara ya kupewa uhuru instead ya kuupigania imeleta vizazi vya watu dhaifu na waoga, ukweli ni kwamba watanzania ni waoga na waliojaa na unafki

Ukienda kwa wakenya wale uhuru waliupigania hawakupewa na hii imepelekea kushape kizazi cha kenya kwenye fikra kuliko sis watanzania, mkenya even mtu wa kawaida anajiamin na anajua haki zake na yuko kuzipigania ila mtanzania ni mwoga, mnafki na kila jambo ambalo liko ndani ya uweza wake atakuambia ana mwachia Mungu

Point hapa sio kuisifia sana Kenya hapana still wanamatatizo yao kama rushwa, ukabila, kiwango chao cha maendeleo hakija pishana sana na Tanzania, ila jambo ambalo nauhakika nalo wakenya sio mazoba kama watanzania
Vipi Congo?
Vipi South Africa?
Vipi Msumbiji?
 
Hizo stories zimekuwa amplified na kuhusishwa na kupigania uhuru maana walikuwa wanapinga wakoloni waliovamia maeneo yao. Hakukuwepo na unity iloyokuwa na vision ya kuunganisha vita vya kupigania uhuru.
Imagine kama Mjerumani angeshindwa na kuamua kukabidhi Nchi na kukimbia.

Majimaji freedom fighters wangelikubalika na Watanganyika wengine kama walivyokuwa TANU tu.

TANU lilikuwa ni group dogo tu lakini kwasababu lilikuwa likipigania uhuru kila Mtanganyika alilikubali.

Kwahiyo badala ya Nyerere huenda raisi wa kwanza angelikuwa Abdulrauf Songea Mbano au Mzee Kinjekitile Ngwale.

Majimaji freedom fighters walikuwa na vision na unity kwamba Mzungu aenda Ulaya Mwafrika aoate Uhuru.

Waliunganisha makabila mengi ya Tanganyika ili kumfukuza Mjerumani.
 
Imhotep,

KANISA NA VITA VYA MAJI MAJI

Hassan Ilunga Kapungu
ABDULRAUF SONGEA MBANO
JEMADARI WA VITA VYA MAJI MAJI

130716526_857077991706247_6658267121574270328_n.jpg

Nduna Abdulrauf Songea Mbano​

Nje kidogo ya mji wa Songea kuna kitongoji kinaitwa Mahenge, hapo kuna sehemu ya kumbukumbu ya vita vya Majimaji. Jambo kubwa la mahala hapo ni kaburi kubwa la halaiki ambamo askari zaidi ya sitini na… (sitini na saba) walizikwa kwa pamoja. Na kando ya kaburi hilo la pamoja kuna kaburi la Abdulrauf Songea Mbano ambae yeye alizikwa peke yake.

Kwa mara ya kwanza nilitembelea makumbusho hayo mwishoni mwaka 2007. Baada ya kusaini kitabu cha wageni na kulipa ada ya kituo muhudumu wa kituo hicho alitupa karatasi yenye orodha ya majina ya wale wote walionyongwa na kuzikwa hapo. Ukiitazama orodha hiyo na hasa ukiwa Mwislam jambo moja litakustuwa. Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam. Linaanza jina lake la Kiiislam, kisha kwenye mabano kuna jina la Kikristo na mwishoni linaishia jina la kiasili, mfano Abdulrahman [Dominic] Mputa Gama.

Muhudumu akatueleza kuwa hawa mashujaa wa vita vya Maji Maji kabla ya kunyongwa alikuwako padri ambae aliwabatiza na kuwapa majina ya Kikristo na baadae kunyongwa, wengi walibatizwa kwa hadaa kuwa wakibatizwa wataachiwa huru, wote katika hao walionyongwa walikuwa ni Waislam. Uzuri ni kwamba katika orodha hiyo kulikuwa na jina na sahihi ya yule padri aliyewabatiza, na kwa mkono wake [huyo padri] aliiyaandika hayo majina. Karatasi yenyewe ilihifadhiwa vizuri kwenye fremu ngumu ya kioo. Tuliomba kwa nguvu zote kupatiwa hiyo karatasi ya majina hata kwa kununua lakini haikuwezekana pamoja na kuwaona na kuwaona wakubwa wa kituo hicho. Niliporudi kwa mara ya pili mwezi July 2009 nilipata mstuko.

Karatasi iliyohifadhiwa kwenye fremu ngumu ya kioo, iliyokuwa na majina ya Kiislaam ya mashujaa wa vita vya Maji Maji, haikuwapo,na badala yake imewekwa karatasi nyingine ombayo ndani ya karatasi hiyo majina ya Kiislaam ya mashujaa hao wa vita vya Maji Maji yameondolewa na kuachwa majina ya ubatizo na yale ya kiasili tu, jina la padri, sahihi yake na wadhifa wake katika Kanisa Katoliki pia vimeondolewa na karatasi yenyewe haikuwa kwenye fremu ya kioo na ilikuwa katika fotokopi tu.

Nilimuuliza muhudu kulikoni? Akasema, “Songea pana mzee mmoja maarufu sana katika historia ya TANU na historia ya kuasisiwa Bakwata anaitwa kwa kifupi M. S. Mzee huyu ana binti yake ambaye ameolewa na Mzungu wa Kijerumani. Binti huyu na na mumewe wa Kijerumani walikuja hapa Songea matembezi. Hivyo kwa shinikizo la huyu mzee M.S. karatasi hiyo alipewa huyu Mzungu kwa ahadi kwamba anaipeleka Ujerumani na atairudisha. Hivyo ndivyo karatasi ile asilia ilivyotoweka. Kubwa katika karatasi ile ni ule ushahidi wa majina kuwa wote katika wale walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam, wengi katika hao walihadaiwa kuachwa huru hivyo wakabatzwa ispokuwa wachahe sana waligoma kama shujaa Abdulrauf Songea Mbano. Huyu kwa ushujaa wake wa kupambana na Wajerumani aligoma na akasumbua sana kiasi akanyongwa siku yake na peke yake na ndio sababu akazikwa peke yake.

Ukiingia ndani ya kinyumba cha ghorofa, unaanza kuona picha za mashujaa wa Maji Maji wakiwa wamevaa mavazi ya vita mithili ya mahujaji wanavyovaa Ihraam wakati wa hija. Kinachoongezeka kwao ni vilemba kichwani. Chini ya kila picha kuna jina la aliyekuwa kwenye picha ile. Ukipanda gorofani utaona silaha za kiajadi kama mikuki, pinde, ngao n.k. Kinachosisimua zaidi ni mavazi ya vita. Mavazi ya vita ya askari wa Maji Maji wengi walivaa kanzu za Kiislaam na vilemba. Jambo jingine linalosisimua ni kile ambacho watu wa kituo hicho wameandika ”rosary” hili ni jina la Kikristo, hasa la Kikatoliki, ni zile shanga ambazo huning’inia msalaba lakini unapotazama hicho kilichoitwa “rosary” utaona si “rosary,” bali ni tasbihi hasa ya Kiislaam yenye kupangika hasa shanga zake, 33, 33, 34. Maneno yaliyoandikwa kuelezea “rosary” hizo ambazo ni tasbihi ni:

“Hizi ni rosary ambazo wapiganaji wa majimaji walikuwa wakitumia KUTAMBIKA kabla ya kwenda vitani kwa kuamini kwamba zitawakinga na risasi.”

Ukweli ni kwamba hawa askari wa Maji Maji wengi walikuwa ni Waislaam hivyo hawakuwa WAKITAMBIKA bali walikuwa wakitumia tasbihi hizo kufanya dhikri kwa Allah kabla ya kwenda vitani. Midhali sisi Waislaam hatujawa tayari kuandika historia yetu kama Waislaam wanaotuandikia watapotosha na kupindisha na kutuzulia wanavyotaka. Hapo gorofani kuna jambo jingine la kusisimua. Kuna magudulia na makopo. Wameandika kuwa, haya ndio makopo ambayo askari wa Maji Maji walikuwa wakiyatumia KUNAWA kabla ya kwenda vitani [kushika udhu na sio kunawa] pia kwa kuamini kuwa maji hayo yatawakinga. Muhudumu alitueleza kuwa kumbukumbu nzuri na za kuaminika ziko Jimbo Kuu la Wakatoliki Peramiho.

Tulikwenda jimboni lakini hatufanikiwa kwa sababu za ki-urasimu tu. Tulitakiwa tupate kibali cha Askofu Mkuu. Hatukukipata. Kwa yale tuliyoyaona na kuyashudia yafuatayo:

Vita vya Maji Maji havikuwa ni vita vya kizalendo, kwamba wazalendo walikuwa wakipigania nchi yao. La vilikuwa ni vita vya Waislaam wakipigana na Wakristo wa Kijerumani waliovamia maeneo asilia ya Waislaam kwa lengo la kuuwa Uislam na kusimamisha Kanisa kwani mazingira yote utayoyaona ya mashujaa wa vita vya Maji Maji ni mazingira ya Kiislaam, kingine ni kwamba hukuti mahala yalipo makaburi ya askari wa Kijerumani ila katika miji ya Waislaam kama Kilwa, Bagamoyo n.k. Kwa nini wauliwe maeneo ya Waislaam tu?

Walifuata nini huko?

Kuna upotoshaji mkubwa sana wa historia ya vita vya Maji Maji. Vinaoneshwa kama ni vita vya wazalendo wakipigana na wakoloni wa Kijerumani, wakati ukweli si hivyo. Ukweli ni kwamba vita vya Maji Maji vilikuwa ni vita baina ya Waislaam na Wakrito wa Kijerumani, Waafrika Wakristo wa Songea walijiunga na Wakristo wenzao wa Kijerumani dhidi ya Waafrika wenzao wa Kiislam.

Kanisa limeitafiti hakika hii na wakaijua kisha wameificha kwa maslahi yao.​
 
Imagine kama Mjerumani angeshindwa na kuamua kukabidhi Nchi na kukimbia.

Majimaji freedom fighters wangekubalika na Watanganyika wengine kama walivyokuwa TANU tu.

TANU lilikuwa ni group dogo tu lakini kwasababu lilikuwa likipigania uhuru kila Mtanganyika alilikubali.

Kwahiyo badala ya Nyerere huenda raisi wa kwanza angelikuwa Abdulrauf Songea Mbano au Mzee Kinjekitile Ngwale.

Majimaji freedom fighters walikuwa na vision na unity kwamba Mzungu aenda Ulaya Mwafrika aoate Uhuru.

Waliunganisha makabila mengi ya Tanganyika ili kumfukuza Mjerumani.
Tukirejea historia ni kwamba mjerumani hajawahi kulikimbia koloni la Tanganyika eti kwa sababu ya hizo resistance, wakoloni walikutana na resistance nyingi tena zaidi ya hiyo wakiwa katika harakati za colonisation ila ujerumani ilikuwa defeated wakati akipigana vita vya ww1&2 akapoteza makoloni yake mengi tu ikiwemo Tanganyika. Hadi pale UN trustee walipoliweka chini ya mwingereza kwa uangalizi wa kuwaachia wenyeji kujitawala.
 
Tukirejea historia ni kwamba mjerumani hajawahi kulikimbia koloni la Tanganyika eti kwa sababu ya hizo resistance, wakoloni walikutana na resistance nyingi tena zaidi ya hiyo wakiwa katika harakati za colonisation ila ujerumani ilikuwa defeated wakati akipigana vita vya ww1&2 akapoteza makoloni yake mengi tu ikiwemo Tanganyika. Hadi pale UN trustee walipoliweka chini ya mwingereza kwa uangalizi wa kuwaachia wenyeji kujitawala.

Ungekuwa unanisoma vizuri kabla ya kuninukuu.
 
Ukiangalia historia ya uhuru wa tanzania utaona imechangia kwa kiasi kikubwa kushape fikra za watanzania wa leo, yaani ukisoma huon struggle kabisa zaid ya watu waliokua wanakutania kwenye bao na vijiwe vya kahawa eti ndo wapigania uhuru hao

Wako wanaosema historia ya Tanzania imechakachuliwa kwa upande mwingine nakubaliana nao ila still hata ukisoma huo upande wa uliochakachuliwa huon struggle kabisa

Madhara ya kupewa uhuru instead ya kuupigania imeleta vizazi vya watu dhaifu na waoga, ukweli ni kwamba watanzania ni waoga na waliojaa na unafki

Ukienda kwa wakenya wale uhuru waliupigania hawakupewa na hii imepelekea kushape kizazi cha kenya kwenye fikra kuliko sis watanzania, mkenya even mtu wa kawaida anajiamin na anajua haki zake na yuko kuzipigania ila mtanzania ni mwoga, mnafki na kila jambo ambalo liko ndani ya uweza wake atakuambia ana mwachia Mungu

Point hapa sio kuisifia sana Kenya hapana still wanamatatizo yao kama rushwa, ukabila, kiwango chao cha maendeleo hakija pishana sana na Tanzania, ila jambo ambalo nauhakika nalo wakenya sio mazoba kama watanzania
Nimekusoma. Nimekuelewa, lakini mosi usimhusishe Mungu katika fikra za kibnadamu, pili ukome kutuita mazoba (pamoja na wewe).
Kwa fikra zangu (kwa sababu naamini katika uhuru wa kutoa maoni yako), kosa kubwa kwetu nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, ni kukubali kuitwa maskini wakati sisi, hususan Tanzania ni matajiri.
Kosa la pili ni kutoamini katika brain zetu kwani RASILIMALI Kuu kuliko yote katika nchi yoyote ni BRAIN za Watu wake.
Tusiige. Nawe umekomalia Kenya. Kenya siyo Tanzania
 
Nimekusoma. Nimekuelewa, lakini mosi usimhusishe Mungu katika fikra za kibnadamu, pili ukome kutuita mazoba (pamoja na wewe).
Kwa fikra zangu (kwa sababu naamini katika uhuru wa kutoa maoni yako), kosa kubwa kwetu nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, ni kukubali kuitwa maskini wakati sisi, hususan Tanzania ni matajiri.
Kosa la pili ni kutoamini katika brain zetu kwani RASILIMALI Kuu kuliko yote katika nchi yoyote ni BRAIN za Watu wake.
Tusiige. Nawe umekomalia Kenya. Kenya siyo Tanzania
kosa kubwa kwetu nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania, ni kukubali kuitwa maskini wakati sisi, hususan Tanzania ni matajiri.
Kosa la pili ni kutoamini katika brain zetu kwani RASILIMALI Kuu kuliko yote katika nchi yoyote ni BRAIN za Watu wake.
Tusiige. Nawe umekomalia Kenya. Kenya siyo Tanzania


Hichi ulichosema hapo juu ndo uzoba wenyewe
 
Back
Top Bottom