Watanzania tunapaswa kufanya mambo haya kuanzia sasa ili kukomesha utekaji na uuaji bila kutegemea jeshi la Polisi

Watanzania tunapaswa kufanya mambo haya kuanzia sasa ili kukomesha utekaji na uuaji bila kutegemea jeshi la Polisi

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Juzi hapa niliweka thread ikiishauri serikali, hususa Raisi Samia, kutoa tamko ambalo lingezuia mara moja utekaji na uuaji. Kama kawaida ya hii serikali yetu, naona hawajali kuchukua hatua kama hizi.

Sasa basi, kama Raisi Samia au serikali kwa ujumla hawana nia ya kuchukua hatua thabiti na rahisi kukomesha utekaji na uuaji, acha jukumu hili tulichukue sisi wananchi wenyewe. Maisha yetu ndio yako hatarini tunapaswa kujilinda.

Natoa wito na hima kwa Watanzania wote, popote pale ambapo unaona watu wasio na uniform wanamkamata mtu, tushirikiane kuzuia hilo kwa kila namna. Tuwazuie watu hao kwa kila njia na kuwaambia wasubiri hadi polisi wafike, wakiwa na uniform na magari yanayoeleweka kuwa ni ya polisi. Hadi sasa hili limeshafanyika kwa mafanikio makubwa! Tusiwe kondoo tena wa kuona mwenzetu anaenda kuchinjwa na kusubiri zamu yetu au ya ndugu yetu.

Umati wa watu ukiwazunguka watekaji, pamoja na magari na bodaboda kufunga barabara, watekaji hawawezi kufanikiwa. Tushirikiane Watanzania, hili linawezekana. Hata kama watekaji wana silaha, sio rahisi kwamba wataanze kuufyatulia risasi umati mkubwa wa watu.

Ukiona watekaji wana nia ya kumchukua mtu, piga kelele, na wale wenye magari na boda boda pigeni honi kukusanya umati wa watu. Tutafanikiwa kukomesha tabia hii ya kinyama inayotuondolea ndugu zetu wapendwa.

Na ikitokea kwamba watekaji wanaingia kwenye basi, abiria wote ndani ya basi tusimame katikati ya njia (aisle) na kutoruhusu mtu kupita, na kuamuru dereva wa basi aendeshe basi hadi kituo cha polisi.

Tafadhali saidia kusambaza huu ujumbe kwa watu wote, kwa email na hata magroup ya WhatApp na mengineyo

Angalia pia


View: https://www.youtube.com/watch?v=C_ahzCLMzrw

 
Juzi hapa niliweka thread ikiishauri serikali, hususa Raisi Samia, kutoa tamko ambalo lingezuia mara moja utekaji na uuaji. Kama kawaida ya hii serikali yetu, naona hawajali kuchukua hatua kama hizi.

Sasa basi, kama Raisi Samia au serikali kwa ujumla hawana nia ya kuchukua hatua thabiti na rahisi kukomesha utekaji na uuaji, acha jukumu hili tulichukue sisi wananchi wenyewe. Maisha yetu ndio yako hatarini tunapaswa kujilinda.

Natoa wito na hima kwa Watanzania wote, popote pale ambapo unaona watu wasio na uniform wanamkamata mtu, tushirikiane kuzuia hilo kwa kila namna. Tuwazuie watu hao kwa kila njia na kuwaambia wasubiri hadi polisi wafike, wakiwa na uniform na magari yanayoeleweka kuwa ni ya polisi. Hadi sasa hili limeshafanyika kwa mafanikio makubwa! Tusiwe kondoo tena wa kuona mwenzetu anaenda kuchinjwa na kusubiri zamu yetu au ya ndugu yetu.

Umati wa watu ukiwazunguka watekaji, pamoja na magari na bodaboda kufunga barabara, watekaji hawawezi kufanikiwa. Tushirikiane Watanzania, hili linawezekana. Hata kama watekaji wana silaha, sio rahisi kwamba wataanze kuufyatulia risasi umati mkubwa wa watu.

Ukiona watekaji wana nia ya kumchukua mtu, piga kelele, na wale wenye magari na boda boda pigeni honi kukusanya umati wa watu. Tutafanikiwa kukomesha tabia hii ya kinyama inayotuondolea ndugu zetu wapendwa.

Na ikitokea kwamba watekaji wanaingia kwenye basi, abiria wote ndani ya basi tusimame katikati ya njia (aisle) na kutoruhusu mtu kupita, na kuamuru dereva wa basi aendeshe basi hadi kituo cha polisi.

Tafadhali saidia kusambaza huu ujumbe kwa watu wote, kwa email na hata magroup ya WhatApp na mengineyo

Angalia pia
Sawa,hapo kwenye mafanikio makubwa ilitokea wapi mkuu!
 
Polisi asiyefuata utaratibu ni mhalifu ndani ya sare
 
Kwamba Kupata Uniform na vitambulisho vya kugushi haiwezekani ? Au Polisi wenyewe hawawezi kuwa waharifu (Bad Apples)?; Au majambazi hawawezi kujifanya ni Polisi ?

In short the only solution ni kuacha kamatakamata, hata polisi wenyewe....

 

Context ya hili suala inapotezwa sana, kama sio kupotoshwa makusudi. Sio kwamba wananchi wanataka OSS au RPC aitwe kila polisi wanapofanya arrest, bali wanataka polisi wakifanya arrest basi kuwe katika utambulisho ulio wazi, ili watu waelewe wanaokamata watu sio "wasiojulikana" wanaoteka na kuua. Nimeona hata Raisi Samia katika hotuba yake amelifanya hili suala liwe completely out of context, na huenda ni kwa makusudi. Hawa watu wasijifanye hawaelewi hili somo. Wakiendela kujifanya hawaelewi kuna siku OSS au RPC ataitwa kuchukua maiti za hao wanaokuja kufanya arrest bila kuwa na utambulisho rasmi kama uniform.

Siku ndugu yangu akitekwa nawaambia nitakuwa na hasira ya kuchoma moto mtu anaefanya arrest bila utambulisho rasmi!
 
Kwamba Kupata Uniform na vitambulisho vya kugushi haiwezekani ? Au Polisi wenyewe hawawezi kuwa waharifu (Bad Apples)?; Au majambazi hawawezi kujifanya ni Polisi ?

In short the only solution ni kuacha kamatakamata, hata polisi wenyewe....
Mkuu, huwezi ukazuia kila kitu, ndio maana tumesema, hata magari wanayokuja nayo yawe Police branded na namba za usajiri za Polisi. La sivyo wananchi wakiwachoma moto wamejitakia!
 
Sawa,hapo kwenye mafanikio makubwa ilitokea wapi mkuu!
Na nyingine hii
 
Baada ya tukio laKiluvya, natoa wito tena Watanzania tuzuie utekaji, tujilinde wenyewe
 
1731487646707.png


Ikiwa sasa tumewajua, na tunajua pia Polisi hawatachukua hatua zozote, tufanyeje kama Watanzania?
 
Back
Top Bottom