Elections 2010 Watanzania tusikubari propagannda hizi! Ni hatari sana!

Elections 2010 Watanzania tusikubari propagannda hizi! Ni hatari sana!

Kwa kutoa hivyo vithibitisho naamini Watahatarisha amani na utulivu wetu tuliojijengea maana imeshasemwa wazi hali ni tete.

Hapo sasa! Vikiletwwa huenda watu tusitazamane usoni!
 
Thank you for this post but Tanzanians have grown now in strength than before in a fair ground they know to choose wisely and we have seen it this time and we shall see more of that in future. CCM will not continue to cover Tanzanians by a blanket of IGNORANCE!
 
....ni CDM na wanaCDM wanapambana na CUF au kinyume chake? kuna hoja imetolewa kwamba redio zetu (mfano radio Imam, Morogoro) zilikuwa zikipiga kampeni kwa base ya udini peupeeeeeeee vivyo hivyo misikitini na magazetu yetu mfano Al-Nnur. endeleeni na propaganda znu ila mtafika mwisho wenu tu. Namni naunga mkono hoja kwamba 'nipo tayari kula nguruwe kuliko kuipigia kura CCM'. Nguruwe nikimpika vizuri nitapata Protein (grade A) lakini CCM itaniendeleza umaskini.
 
Ni kweli ingawa pia tunapoingiza wachungaji kwenye siasa inadhihirisha na kuonyesha jinsi tulivyo. Ni kweli lakini pia makanisa yanapojitokeza hadharani na kuipigania chadema inadhirisha kuwa kina ajenda ya UDINI. Ni kweli lakini pia ZITO anapoandamwa sana ndani ya chama ni dhahiri udini unafanya kazi yake. ni kweli lakini pia unaposimamisha mgombea mwenza muislamu mbumbumbu (darasa la saba) ni kielelezo tosha cha kuonyesha waislam watakuwa wakubruzwa tu katika serikali ambayo ingeundwa na chadema. NA HUU NDIO UMAKINI WA VIONGOZI WA CHADEMA. Ni kweli pia hata wana JF wanaoshabikia chadema wana msimamo hasi dhidi ya Waislamu. Ni kweli lakini pia jinsi chadema ilivyojipanga kupambana na CUF inadhirisha na kuamsha maswali mengi. NA HII YOTE HAIHITAJI KUPIGIWA PROPAGANDA NA CCM. Ni ukweli usiofichika. Bado ni kweli hata kadiri tunavyokwenda inadhirisha uchanga wa wanasiasa wa chadema. Bado nasisitiza kuwa UBINAFSI NA UZANDIKI NA UKABILA PAMOJA NA KUKOSEKANA UZALENDO ni miongoni mwa vipaumbele vya viongoi wa chadema. Bado haya yote hayahitaji kupandikizwa na CCM.
Twende mbele turudi nyuma bado wanasiasa wa Chadema hawana vision ya Utaifa bali wanataka kutumia silaha na umasikini pamoja na katiba kufika Ikulu kwa gharama yoyote hata ikigharimu maisha ya watu wengi.
Ningeshawishika kidogo madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS ikiwa chadema wangekuja na DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. JE, KATIKA HILI CCM SI WATAONEKANA BORA ZAIDI ??
NACHANGIA HOJA.
Hivi mkubwa na wewe hutaki katiba mpya? Acha ushabiki usiokuwa na kichwa wala miguu
 
ndugu yangu hapo ni kweli kabisa kuna wakti mwingine hili suala la waislam kubezwa kebehi lipo hapa jf, na linaniumiza sana, unakuta mchangiaji mmoja (Muislam) amekosea au ni mtazamo wake tu, basi hapo tutatukanwa waislam wote na majina mabaya mabaya yote tutapewa. nafikiri hilo halijengi sana litabomowa na inatoa nafasi kwa adui kushambulia. tuwe kitu kimoja tabu njaa maradhi yote yetu, hospital kama hakuna dawa hakuna kwa wote, iman yangu kubwa wote wanaodai mabadiliko hawakufuata dini, ni hali ngumu ya maisha kila siku afadhal ya jana.
 
Wewe mtowa mada, hebu kwanza iedit hiyo post yako na uweke sawa kiswahili ulichoandika. Mnatuharibia hii lugha tamu. Mfano hata hicho kichwa cha habari ni "tusikubali" badala ya ulivyoandika "tusikubari".
 
Article nzuri.
Nyongeza: Tusikubali pia propaganda za Dr. Slaa kuwa kura zake zimeibiwa mpaka atuonyeshe vidhibiti.


Hata asipotuonyesha vidhibiti ,kwangu ilikuwa tosha tu pale nilipoona tume inatangaza na kusema ilikosea na kusoma matokeo tofauti kati ya Geita na Nyangwale,at the same time ikatuambia inafanya klazi ya kuhakiki shameless Tume na watendaji wake kwa kutokujua walilokuwa na fanya,not only that tume kutotangaza matokeo ya vituo kadhaa kwa upande wa Raisi is another weekness,siyo hivyo tu kuchelewesha bila sababu yoyote ni dhahiri kulikuwa na kitu flani,mwisho kutoruhusu transparent system was a big mistake,sihitaji vidhibiti zaidi ya hivyo.

Kitendo cha tume kutangaza system itakayotumika na kufanya tofauti ni big problem.Acheni propaganda zenu mtu kama wewe tunakujua umetokea wapi.Nawaambia hivi mwisho wenu sasa umefika,sidhani kwa Dk kukaa kimya inamaana hana vidhibiti i wish ningekuwa na uwezo wa kumpeleka Jk mahakamani ningefanya hivyo faster kwani siri naijua.

We muache tu hata Jeshi limemchoka linamlia timming aendeleee tu na safari zake aje aone.

Trend ni nzuri tunaomba wachangiaji wenye akili hata kama wanakosoa siyo vipofu.
 
mbona ni huyo huuyo dr. Slaa aliyetoa barua fake ya mipango ya ccm pale lakairo hotel? Hakuwa anahatarisha amani?? Si ni huyo huyo pia aliyevishutumu vyombo vya usalama wa taifa kuwa vimemuhujumu. Kuna hatari kuliko hiyo??
au ni ubabaishaji kwa kwenda mbele???
 
Wakati mwingine si vyema kukubali kuwa vipaza sauti vya wanasiasa. Turudi pia tuwaambie kuwa kile ulichokisema mmh kina walakini na pengine ni uongo. Suala la kura linahitaji analysis na dr. Slaa ni analytical mzuri na namheshimu sana.
Ana vyanzo vingi vya kupata taarifa vikiwemo wana usalama wake ambao pia naanza kuwatilia mashaka makubwa.

Anyway niliwahi kuandika kwenye post nyingine wiki tatu kabla ya uchaguzi haya yafuatayo;

1.0 political leaders always do "mistakes"!!
2.0 analytical leaders always do "blunders + bloodshed".

sasa naongezea kusema: "you need a wise political leader to control analytical leader from doing blunders"!!!

and i can presume "hon. Zito kabwe" can be one of wise and really intelligent leader in chadema!

Kwangu mimi nafunga mjadala.

Mkiniita pandikizi hayaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1!!!
Mkisema nimetumwa hayaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mkiniita mwenye siasa kali hayaaa!!!!!!!!
Mkiniita mdini hayaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Lakini mimi ni mzalendo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!mtanzania.
 
Naomba tusubiri uteuzi wa wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa ndo mtajua nani mdini kati ya Slaa na JK.
 
Nikiwa kama mtanzania wa kawaida ambae ninaipenda nchi yangu,sina budi nikitoa maoni yangu.
Nimejaribu kufatilia sana siasa za Tanzania tokea uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1995 kipindi cha kampeni. Nakumbuka uchaguzi wa mwaka huo chama kikuu cha upinzani kilikuwa ni Nccr mageuzi
ya akina Mrema against chama tawala ccm ambacho mgombea wake alikua Benjamini mkapa.

Ukiachilia vyama vyote vya upinzani wakati huo,chama ambacho kilikubarika na watu ni Nccr mageuzi
Ccm walipogundua kuwa Nccr ni hatari na nitishio kwao,wakaenda mafichoni,waliporudi wakaja na pro
paganda ya kuwa Nccr mageuzi ni chama cha kikabila [wakimaanisha wachaga] na maana ya NCCR ni
Ni Chama Cha Rabsha. Kwakua kipindi hicho baadhi ya watanzania wengi tulikuwa na mawazo mgando
tukainyima kura Nccr na Mrema wake. Tukaipa kura ccm na mkapa akashinda japo si kwa kishindo.

Uchaguzi wa mwaka 2000 ikatokea chama kingine chenye nguvu na sera mzuri against ccm nacho ni
CUF,kikiongozwa na mh.Lipumba kwa huku Bara na visiwani kikiwakirishwa na Seif sharif Hamadi.
Ccm kama kawaida yao walipoona CUF inakubarika na wananchi,wakaingia tena mafichoni, waliporudi
tu wakaja na bonge la propaganda ya kuwa CUF ni chama cha kidini [hapa walilenga uwislaam].

Haitoshi wakaagizia mapanga nje ya nchi na yakaja kwenye contena yakiwa yana bendera za CUF.
wakaviita vyombo vya habari kuja kushuhudia ugaidi wa Cuf! kumbe si kweli bali propaganda tu!.
Kwahiyo yale ya mwaka 95 yaliyomkuta Lyatonga na Nccr yake,ndio yaliyemkuta mh.Lipumba na
cuf yake. Watanzani tukaigopa Cuf kama ukoma na kura zote tukaipa ccm,na wakashinda tena kwa
propaganda zao

Uchaguzi wa mwaka 2005 nao ukaja na vitukovyake. kwanza wapinzani hawakuwa na nguvu kama
chaguzi zilizopita. kwahiyo ccm kama kawida yao wakazama mafichoni,walivyorudi huko wakaja na uo
ngo unaofanana na propaganda kwa wadanganyika [walikuja na vitu 3] ili tuwachague tena.
Kwanza walisema chagua ccm maisha bora kwa kila mtanzania.Pili wakasema mgombea wao [mh.kikwete] ni 'handsome'yaani ni mzuri ki umbo. Tatu wakasema kikwete ni chaguo La mungu. Wadanganyika tukaichagua ccm,na kikwete akashinda kwa kishindo.kumbe uongo mtupu!

Lakini mambo yaliyotokea ndani ya miaka hiyo mitano hakuna asiyejua! ni vurugu tupu hakuna cha
maisha bora wala babu yake maisha tamu! Badala yake tukashuhudia ufusadi wa kutisha na maisha
kuendelea kuwa magumu kwa watanzania tulio wengi.

Uchaguzi uliyopita wa mwaka huu 2010 ulikuwa wa aina yake kwa wananchi wengi kuwa na mwitikio.
Pamoja na vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi huo,chama ambacho kilikuwa na nguvu ya ajabu na kukubarika na wanchi kwa kasi ya ajabu ni Chadema ambacho kwenye kampeni zake kiliongozwa na
Dr Slaa na timu yake iliyo makini. Hakika hiki ni Chama cha upinzani ambacho hakijawai tokea Tanzania. Chama ambacho kilikuja na sera mzuri,viongozi imara,wasomi na wenye uchungu wa Tanzania na raia wake! Hakika waliichambua serikali ya ccm kuanzia utosini hadi unyayoni na watanzania tukaamka for first time.

Lakini kama kawada ya ccm,wakaenda mafichoni waliporudi huko wakaja na bonge la propaganda lenye sumu kali. Wakasema Chadema ni chama cha kidini [hapa walilenga ukristo]na ukabila.
Kwa watu kama sisi ambao tunazijua propaganda za ccm tukasema Nooo! thiz time we have to vote for change,na tukaipa kura chadema. Ila kwa wale waliokuwa teyari kuipa kula chadema wakati huo huo hawazijui propaganda za ccm 'hasa vijijini' waliposikia sumu za ccm wakabadilisha mawazo na wakaipa kura ccm au hawakwenda kabisa kupiga kura. kwahiyo ikawa faida na neema kwa ccm na
hasara kwa Chadema. ccm ikashinda tena japo si kwa kishindo kama chaguzi zilizopita.

Narudia tena, Chadema ni chama ambacho hakijawahi tokea Tanzania bara! kimetuonyesha kina
sera mzuri,uongozi imara,na kina future ya Tanzania tunayoitaka! kimepata wabunge wengi bara kuliko chama chochote cha upinzani. Ni chama ambacho kimekubarika pande zote za Tanzania bara!
Na isingekuwa propaganda za ccm,basi Chadema ingeshika Dola na leo ingekuwa story nyingine.

Hitimisho langu ni-
Watanzania tusikubari propaganda hizi za Ccm! Ni hatari sana hawa watu hasa wanapoona kuna chama cha upinzani makini na chenye uongozi imara,hapo wao wako teyari waivuruge nchi kwa
propaganda za sumu ili mladi waendelee kutawala! Camooon guys tuamkeni watanzania! hii ni
nchi yetu wote na tunawajibu ya kuipigania kwa manufaa ya walio wengi! Ahsanteni.

Nawakilisha.

Huwa nasema sisi Watanzania tuko kama madebe tupu! Kwenye debe tupu unaweza kutupa kila aina ya uchafu na ukakaa. Watanzania wengi wanadanganya kiraisi na wanakubali bila hata kuweka chembe ya akili (kujiuliza kwa nini wamekubali). Mimi mtu akiniletea porojo namwomba data na siyo data tu balia data anazoweza kuzi'verify'. Vinginevyo, nemeamua kujikomboa kutoka hao watu wanaotudanganya kila siku ili malengo yao yatimie.

Hebu ona wajinga wengine wanavyofanya:
1. Wameona, sikia, shuhudia Chadema wakilalamika na kupeleka malalamiko yao kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa kura zao zimechakachuliwa.
2. Tume haikujali na iliamua kuendelea na mchakato wa kutangaza matokeo as if hakuna malalamiko yoyote.
3. Baadaye walimtangaza Jakaya Kikwete kuwa ameshinda uchaguzi.
4. Chadema wakasema mfumo/mchakato uliotumika kumtangaza Kikwete kuwa rais hawakubaliani nao. Ila walijua rais akishatangazwa hakuna cha kushtaki mahakamani.
5. Wakaona ili wawasilishe ujumbe wao kwa umma na wafadhiri watoke nje ya Bunge mara tu rais atakapoanza kutoa hotuba na ndivyo walivyofanya.
6. Halafu baadhi ya Watanzania wanawalaumu kwa kufanya walivyofanya badala ya kulaumu chanzo cha tatizo kilikuwa nini! Mimi nawalaumu waliochakachua kura na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kupuuza malalamiko ya Chadema - hawa ndio wa kulaumiwa kwani ndio waliosababisha Chadema kuchukua hatua waliyochukua.
7. Sasa cha ajabu baadhi ya Watanzania wanaingia kwenye ushabiki wa kuwatetea wachakachuaji wa kura na kuwalaumu wanaolalamikia huo mfumo mbaya wa uchaguzi. Je, hiyo ndiyo akili?
 
I thnk wajmii we dont hve 2 be stupid,coz kukosoa ama kutofautiana mawazo siyo udini,,naona most yawanamember wanaudni kwelikweli..hzo sio hja zakutatua umaskni wetu.,mimi nadhni hoja kubwa hpa niaina ya viongozi 2liokuanao,that the problem of why?we are poor...so hoja nikudiscuss jinsigani 2naweza kuipata katiba mpya..hpe ndyo itakayotuletea viongozi bora..siyo bra viongozi,so achni kushamblia imani za wtu.
 
Uchaguzi umekwisha, mshindi kashatangazwa, kiongozi wa kambi ya upinzani kashapatikana, hafla ya kumpongeza rais imeshafanyika na hata kuhudhuriwa na viongozi machachari wa chadema mfano shibuda, sasa tunacholumbana mimi sikielewi, tuache malumbano tujenge taifa letu na sasa la kufanya ni kuelekeza nguvu zetu ktk katiba mpya.

Chadema tayari wameshaitambua serikali ya kikwete kwa kuhudhuria bungeni na kuunda serikali kivuli yenye kupata ruzuku toka serikalini, hivyo tusipoteze muda wetu kujadili jambo lisilowezekana la kushinikiza kutolewa kwa ushahidi wa uchakachuaji wa kura.
 
Nashukuru kwa michango yenu ambayo imejali maslahi ya Utaifa Zaidi kuliko udini. ingawa pia nashangazwa na michango yenu pahala pengine ambapo mnajidhirisha mlivyo na chuki dhidi ya dini zingine na hasa Uislamu. Binafsi sioni tatizo la nani atawale nchi hii. Hii ni nchi yetu sote. Pengine tatizo ni dhamira inayojitokeza wakati wa kufanya maamuzi MUHIMU NA NYETI na jinsi tunavyosifia Umakini wa viongozi tunao washabika bila kupima upande wa pili. Hebu tuendelee kujadili.

1.0 Suala la mgombea mwenza wa chadema kuwa mbumbumbu ingawa kweli kuna tatizo la kikatiba hapo je, hamkuona kama kumchagua huyo ilikuwa ni Kuwatenga Wazanzibari na Waislamu???. je, hamuoni kwa kufanya hivyo mumekosa kura muhimu za wenye kuyatazama majambo kwa uelewa mzuri??

2.0 Je, Suala la wana JF waliowengi wanaoshabikia Chadema kubeza waislamu hamuoni linahatarisha msingi wa umoja wa Taifa letu?. Je, Chadema inajipambanua vipi kitaifa? mdharau mwiba mguu huota tende! kalagabaho!!!

3.0 Je, suala la Chadema na wanachadema kupambana na CUF hamuoni haileti picha nzuri Kitaifa?

4.0 Madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS . Na BADO chadema wameshindwa kuleta DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja na ushee sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. UMAKINI WA VIONGOZI WAPAMBANAJI UKO WAPI???????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Haya mambo manne muhimu tujadili kwa kina bila ushabiki. Penye tatizo tuthubutu kusema. Nafahamu wazi CCM wamekuwa na tabia ya kupandikiza propaganda za kuuwa chama chenye nguvu. lakini pia naomba michango yenu katika haya mambo manne. je, CCM inahusika vipi?
Na kama ni kweli basi kuna tofauti gani kati ya CCM na CHADEMA?
Iam more RATIONAL than EMOTIONAL instigated!

Mkuu ninalo ombi doogo tu kwako, tafadhali soma tena hoja kama ilivyowakilishwa na mleta hoja halafu usipindishe tena mambo kuelekea kwenye maswala ya udini ujitahidi tu kuchangia. Jaribu sana kuepuka kutaja taja dini mahali popote. Halafu tujadili pamoja. Tafadhali sana jitahidi Mtanzania mwenzangu. Tujitoe kwa Taifa letu tu siyo dini zetu. Hapa JF anayekuja na hoja ya kudharau au kushambulia dini nyingine anastahili kupuuzwa tu wala asijadiliwe. Asante sana.
 
Naona kama ccm wameanza kufanikiwa kuwagawanya wadanganyika kwa hoja ya udini kwa vile
1. Tofauti ya Zitto na Chadema inajengewa hoja ya ukristo na uislamu zaidi kuliko kujadili issue ndani ya chama
2. Dr Slaa kugombea uraisi inaonekana alikuwa na sera ya kueneza ukristo na hivyo hawafai watanzania.
Kama hili litafanikiwa CCM chelea pina watatawala mpaka karne ya 22
 
tatizo la baadhi ya waislam wanaona kama kumpinga kikwete ni kuupinga uislam wakati mkapa alisakamwa zaidi yake na wla hisia za kidini hazikuwepo,watu wanaichukia ccm either rais awe mkristo au muislam...na hawaipendwi kwa sababu ya ufisadi wake..acheni upuuzi wa kfikiria dini kuliko taifa wakati dini zenyewe tuliletewa na watu weupe kutoka mashriki ya kati na ulaya tukaacha dini zetu...AMKA!!UMELALA
 
Mi ni muislam tena swala tano ila kuliko niishabikie au kuchagua ccm bora nile nguruwe japo hacheuwi.ccm ni kama nguruwe hakicheui kile chama wao ni kula tu.ikumbukwe pia nguruwe hula hadi wanae aliowazaa mwenyewe.same like happen to ccm wana sema eti elimu bure haiwezekani wakati wao walisomeshwa na hiyo hiyo ccm bure.SHAME ON YOU CCM NA TEAM NZIMA.

Nimekukubali kwa hilo,heshima kwako na ubarikiwe kwa kila jambo lako lolote utalofanya.
 
Back
Top Bottom