Watanzania tutakuwa wengi kwa kuhesabiwa kimakosa

Watanzania tutakuwa wengi kwa kuhesabiwa kimakosa

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Leo ni siku ya Sensa. Hata hivyo mpaka kunakucha leo bado sikuwa na taarifa sahihi za sensa. Sikujua leo nisitoke nyumbani au nikitoka niache nini na nini. Tabia yangu huwa sifungui tv wala redio nyumbani na kwenye simu siangalii sana ujumbe mpaka nione ni wa kampuni za simu wenye neno pesa.

Kwa namna hiyo wangenipatia kunielimisha kama wangetoa matangazo mitaani kwa muhtasari na kunielekeza nini cha kufanya leo. Bahati mbaya niliwahi kuona msafara wa magari unaotoka ofisi ya mkuu wa wilaya lakini zaidi ilikuwa ni kutaja siku ya sensa na kibwagizo. Mimi niko tayari kuhesabiwa. Wewe Je?

Kwa mara nyengine niliwahi kuona kikundi cha wangenguaji na yawezekana walilipwa kwa kazi hiyo. Nilikutana nao nje sokoni wakiwa wameshuka kutoka kwenye gari lao. Wanacheza kwa kurusha miguu, mikono na kukatika viuno bila kutoa ujumbe wowote.

Matokeo yake mpaka nawapita na kuendelea na safari sikusikia chochote cha kufanya siku ya sensa.

Nimesikia kwa wapita njia kuwa sensa itaendelea kwa siku 7. Siku ya kesho mpaka siku ya 7 wakipita sitakuwa na majawabu ya leo. Vilevile ama hawatonikuta hapa nyumbani tena au tutakutana kwengine mbali.

Mimi niko tayari kuhesabiwa,lakini nina wasi wasi ama hawatonihesabu au watanihesabu mara zaidi ya moja.
 
Usiogope mzee. Tutakukadiria. Kuna + au - tunaiweka katika idadi tutakayo ipata na tunahesabia mahala ulipoamkia tu.

Ngoja mvua ipungue tuanze kazi.
 
Sensa ni tofauti na bajeti. Most likely, mabeberu wanaitumia ili kukadiria wale vichwa vingapi next time kwa something like Covid-19 plandemic

mama D 🙂

 
Usiogope mzee. Tutakukadiria. Kuna + au - tunaiweka katika idadi tutakayo ipata na tunahesabia mahala ulipoamkia tu.

Ngoja mvua ipungue tuanze kazi.
We ngoswe mbona hufiki uanze kuhesabu
 
Usiogope mzee. Tutakukadiria. Kuna + au - tunaiweka katika idadi tutakayo ipata na tunahesabia mahala ulipoamkia tu.

Ngoja mvua ipungue tuanze kazi.
Mimi nimeamkia hapa.Wakija leo watanipata.Ikiwa hawakufika leo.Keshokutwa itakuwa nimesafiri atabaki mtoto nyumbani.Itakuwaje.
 
Sasa kina ana makinda ndio bosi unategemea nini badala ya kuchukua watu wenye taalamu wanampa mwanasiasa.
hii nchi connection tu ndio maana kila kitu ili mradi tu liende hakuna weledi
 
Leo ni siku ya Sensa. Hata hivyo mpaka kunakucha leo bado sikuwa na taarifa sahihi za sensa. Sikujua leo nisitoke nyumbani au nikitoka niache nini na nini. Tabia yangu huwa sifungui tv wala redio nyumbani na kwenye simu siangalii sana ujumbe mpaka nione ni wa kampuni za simu wenye neno pesa.

Kwa namna hiyo wangenipatia kunielimisha kama wangetoa matangazo mitaani kwa muhtasari na kunielekeza nini cha kufanya leo. Bahati mbaya niliwahi kuona msafara wa magari unaotoka ofisi ya mkuu wa wilaya lakini zaidi ilikuwa ni kutaja siku ya sensa na kibwagizo. Mimi niko tayari kuhesabiwa. Wewe Je?

Kwa mara nyengine niliwahi kuona kikundi cha wangenguaji na yawezekana walilipwa kwa kazi hiyo. Nilikutana nao nje sokoni wakiwa wameshuka kutoka kwenye gari lao. Wanacheza kwa kurusha miguu, mikono na kukatika viuno bila kutoa ujumbe wowote.

Matokeo yake mpaka nawapita na kuendelea na safari sikusikia chochote cha kufanya siku ya sensa.

Nimesikia kwa wapita njia kuwa sensa itaendelea kwa siku 7. Siku ya kesho mpaka siku ya 7 wakipita sitakuwa na majawabu ya leo. Vilevile ama hawatonikuta hapa nyumbani tena au tutakutana kwengine mbali.

Mimi niko tayari kuhesabiwa,lakini nina wasi wasi ama hawatonihesabu au watanihesabu mara zaidi ya moja.
Ilitakiwa ukihesabiwa unawekewa alama ya wino kama kwenye zoezi la kupiga kura..
 
Leo ni siku ya Sensa. Hata hivyo mpaka kunakucha leo bado sikuwa na taarifa sahihi za sensa. Sikujua leo nisitoke nyumbani au nikitoka niache nini na nini. Tabia yangu huwa sifungui tv wala redio nyumbani na kwenye simu siangalii sana ujumbe mpaka nione ni wa kampuni za simu wenye neno pesa.

Kwa namna hiyo wangenipatia kunielimisha kama wangetoa matangazo mitaani kwa muhtasari na kunielekeza nini cha kufanya leo. Bahati mbaya niliwahi kuona msafara wa magari unaotoka ofisi ya mkuu wa wilaya lakini zaidi ilikuwa ni kutaja siku ya sensa na kibwagizo. Mimi niko tayari kuhesabiwa. Wewe Je?

Kwa mara nyengine niliwahi kuona kikundi cha wangenguaji na yawezekana walilipwa kwa kazi hiyo. Nilikutana nao nje sokoni wakiwa wameshuka kutoka kwenye gari lao. Wanacheza kwa kurusha miguu, mikono na kukatika viuno bila kutoa ujumbe wowote.

Matokeo yake mpaka nawapita na kuendelea na safari sikusikia chochote cha kufanya siku ya sensa.

Nimesikia kwa wapita njia kuwa sensa itaendelea kwa siku 7. Siku ya kesho mpaka siku ya 7 wakipita sitakuwa na majawabu ya leo. Vilevile ama hawatonikuta hapa nyumbani tena au tutakutana kwengine mbali.

Mimi niko tayari kuhesabiwa,lakini nina wasi wasi ama hawatonihesabu au watanihesabu mara zaidi ya moja.
Usiwe na wasiwasi nakuhakikishia hao watu wamejipanga lazima utafikiwa
 
Ngoja tuone...
Sio tuone. Muhimu uhamasishaji wa sensa uendelee hii leo kwa nguvu zaidi. Yapite matangazo mitaani, na kila mtu mwenye simu apokee ujumbe hii leo kabla ya jioni ili kila mtu aelewe cha kutunza katika kumbukumbu zake.Na bora watu waambiwe waandike taarifa muhimu kwenye karatasi zao.Yabaki masuala ya ziada mpaka watakapofika hao maafisa wa sensa.
 
Back
Top Bottom